Saturday, August 25, 2012

ALLAAH AWANUSURU SYRIA NA MYANMAR (BURMA)


Kwa jina Lake Mwenyezi, Mola wetu Subhana,
Nawasalimu Wapenzi, Awalinde Maulana,
Yeye ndie Mkombozi, Peke Yake hana mwana,
Mungu Awaangamize, Manusayri makafiri.

Manusayri makafiri, Syria wanapigana,
Mashia hawa hatari, hawajui uungwana,
Wao wanapenda shari, wanapenda kuuana,
Mungu Awaangamize, Manusayri makafiri.

Ni maadui wa Sunni, yote yanaonekana,
Huwachinja Waumini, kwa silaha kila aina,
Silaha toka Irani, na Urusi na Uchina,
Mungu Awaangamize, Manusayri makafiri.

Waumini siku hizi, Syria wana shida sana,
Wamekuwa Wakimbizi, hata chakula hawana,
Wengine hawajiwezi, wanakufa tunaona,
Mungu Awaangamize, Manusayri makafiri.

Manusayri mashetani, makafiri wajalana,
Hawafungi Ramadhani, wala Kuhiji hapana,
Dini yao sio dini, na Pagani hufanana,
Mungu Awaangamize, Manusayri makafiri.

Allah Awape subira, watoto wanalizana,
Wanarusha makombora, kwa marefu na mapana,
Mabinti hutekwa nyara, nashindwa hata kunena,
Mungu Awaangamize, Manusayri makafiri.


                          


Kwingine ni Myanmari, wanapigwa Waumini,
Tunakuomba Qahari, Rudisha kwao amani,
Watoe kwenye hatari, wamo kwenye mtihani,
Mungu Awaangamize, Mabudha wa Myanmari.

Mabudha wa Myanmari, Burma jina la zamani,
Watose kwenye bahari, kama vile Fira’auni,
Uvunje yao kiburi, na vichwa virudi chini,
Mungu Awaangamize, Mabudha wa Myanmari.

Na tena bila futari, walifunga Ramadhani,
Na Wewe ndio Jabari, Unawaona Machoni,
Faraji wanasubiri, kutoka Kwako mbinguni,
Mungu Awaangamize, Mabudha wa Myanmari.

Umoja wa Mataifa, wananyamaza kwa nini?
Sababu wanaokufa, ni Waislamu yakini,
Twazijua zao sifa, na chuki kwa yetu dini,
Mungu Awaangamize, Mabudha wa Myanmari.

Tuamke Waislamu, na macho yafumbueni,
Imani iwe timamu, masikio zibueni,
Walimu na Maimamu, watoto wazindueni,
Mungu Awaangamize, Mabudha wa Myanmari.

Kweli nina wasiwasi, ndugu wapo hatarini,
Ninamuomba Mkwasi, Awalinde masikini,
Ombeni duaa upesi, kwenye Swalah ziombeni,
Mungu Awaangamize, Mabudha wa Myanmari.
ANNUUR 1031

Friday, August 17, 2012

MSAMU INAWATAKIA WANAFUNZI NA WAISLAM WOTE EID NJEMA NA KUWAPA MUONGOZO HUU JUU YA EID


'Iyd Taratibu Na Shari'ah Zake


 Imetafsiriwa na: Ummu Ummu Ayman

Sifa njema ni za Allaah, Bwana wa Ulimwengu, na rehma na amani zimshukie Mtume wetu Muhammad na Aali zake na Swahaba zake.

“'Iyd” ni neno la kiarabu linalomaanisha jambo la kitabia au ada, lenye kurudi na  kujirejea. 'Iyd au sikukuu ni alama au nembo inayopatikana katika kila taifa, ikiwa ni pamoja na mataifa yale yaliyotajwa katika vitabu vitukufu na yale ya waabudiao masanamu, pamoja na wengineo, kwa sababu kusherehekea sikukuu ni jambo la kimaumbile katika maumbile ya mwanaadamu. Watu wote wanapenda kuwa na matukio  maalumu ya kufanya sherehe, ambapo wanaweza kukukusanyika pamoja na kuonyesha furaha zao.

Sikukuu za mataifa ya makafiri zinaweza kufungamanishwa na mambo ya kidunia, kama kuanza kwa mwaka, kuanza kwa msimu wa kilimo, kubadilika kwa hali ya hewa, kuanzishwa kwa dola, kutawazwa kwa kiongozi, n.k. Zinaweza pia kufungamanishwa na matukio ya kidini, kama ambavyo nyingi ya sikukuu zinazowahusu Mayahudi na Wakiristo tu, mfano Alkhamiys ambayo wanadai kuwa meza maalum iliteremshwa kwa Yesu, Krismas, Mwaka Mpya, Siku ya kushukuriana, na sikukuu ambazo watu hupeana zawadi. Hizi husherehekewa katika nchi zote za Ulaya na Amerika ya Kaskazini hivi sasa, na katika nchi nyengine ambazo ukristo una nguvu, hata kama nchi yenyewe si ya kikiristo kiuhalisi. Baadhi ya wanaoitwa Waislam huweza kujiunga katika sikukuu hizi, kwa sababu ya ujinga au unafiki.

Wamagiani (Magians) nao pia wana sikukuu zao, kama Mahrajaan, Namrud n.k.

Ma-baatini (Miongoni mwa Mashia) wana sikukuu zao pia, kama ‘Iyd al-Ghadiyr, ambapo wanadai kuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amempa ukhalifa ‘Ali (Radhiya Allaahu ‘anhu) na maimamu kumi na moja   baada yake.


Waislamu Wanatambulika Kwa Sikukuu Zao

Maneno ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) "Kila Umma una sikukuu yake na hii ni sikukuu yenu"  yanaonyesha kuwa ‘Iyd hizi mbili ni maalumu kwa Waislamu tu, na kuwa hairuhusiwi kwa Muislam kuwaiga makafiri na washirikina katika jambo lolote ambalo ni maalumu ndani ya sherehe zao, iwapo kama ni chakula, nguo, kuwasha moto au matendo ya ibada.

Watoto wa Kiislam wasiruhusiwe kucheza katika sikukuu hizo za kikafiri, au kujipamba, au kujumuika na makafiri katika matukio hayo. Sikukuu zote za kikafiri au zilizozushwa ni haraam, mfano kama sherehe za Siku ya Uhuru, maadhimisho ya mapinduzi, miti ya sherehe za sikukuu au kutawazwa kwa kiongozi, siku za kuzaliwa, Sikukuu ya Wafanyakazi, Sikukuu ya Nile, Shamm an-Nasiym (sikukuu ya majira ya baridi ya Wamisri), siku ya walimu, na Maulidi ya Mtume (Kuzaliwa kwa Mtume).

Waislam hawana sikukuu ukiacha ile ya ‘Iyd al-Fitwr na ‘Iyd al-Adhw-haa, kwa sababu ya hadiyth iliyotolewa na Anas (Radhiya Allaahu ‘anhu) amesema: "Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuja Madiynah na watu walikuwa na siku mbili wakicheza na kufurahi.  Akauliza, "Ni siku gani hizi mbili?" Wakasema, "Tulikuwa tukicheza na kufurahi katika siku hizi  zama za ujaahiliyya" (zama za ujinga kabla ya Uislamu).  Mtume  (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema, "Allaah Amekupeni siku bora kuliko hizo, nazo ni siku ya ‘Iyd  Al-Adhw-haa na siku ya ‘Iyd Al Fitwr".  (Sunan Abi Daawuud 1134)


Yafuatayo ni maelezo kuhusu shari'ah na adabu za ‘Iyd mbili kwa mujibu wa Sharia ya Kiislam:

Ahkaamul-'Iyd (Shari'ah Katika 'Iyd)

Kufunga

Ni haraam kufunga katika siku za ‘Iyd kutokana na hadiyth ya Abu Sa’iyd al-Khudriy (Radhiya Allaahu ‘anhu), amesema kuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza kufunga katika siku ya Fitwr na katika siku ya Kuchinja (Adhw-haa). (Imeripotiwa na Muslim, 827)

Shari'ah Katika Swalah Za 'Iyd

Baadhi ya wanavyuoni wanasema kuwa Swalah ya ‘Iyd ni waajib, huu ni mtizamo wa wanavyuoni wa Kihanafi na Shaykh al-Islam Ibn Taymiyah (rahimahu Allaah). Wanasema kuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiswali Swalah zote za ‘Iyd na hakuacha kufanya hivyo hata mara moja. Wamechukua ushahidi katika ayah (yenye tafsiri),

"Basi swali na uchinje kwa ajili ya Mola wako Mlezi"  Al-Kawthar: 2

Yaani  Swalah ya ‘Iyd na kuchinja baada yake, ambayo ni amri, na kwa ukweli kuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliwaamrisha wanawake watolewe kuhudhuria Swalah ya ‘Iyd, na kwamba mwanamke aliyekuwa hana jilbaab aazime kutoka kwa ndugu yake

Baadhi ya wanavyuoni wanasema kuwa Swalah ya ‘Iyd ni Fardhu Kifaayah (fardhi yenye kutosheleza). Huu ni mtizamo wa Kihanbali. Kundi la tatu linasema kuwa Swalah ya ‘Iyd ni Sunnah iliyokokotezwa. Huu ni mtizamo wa Kimaalik na Kishaafi. Wanachukua ushahidi ya hadiyth ya Bedui inayosema kuwa Allaah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Hakufaradhisha Swalah yoyote kwa waja Wake zaidi ya zile Swalah tano. Kwa hiyo Waislam wafanye hima kuhudhuria Swalah ya ‘Iyd, hususan kwa kuwa maoni ya kuwa ni waajib yameegemea katika ushahidi wenye nguvu. Neema, baraka na malipo makubwa yanapatikana kwa kuhudhuria Swalah za ‘Iyd, na kwa ukweli kuwa mtu atakuwa anafuata mwendo wa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwa kufanya hivyo, basi inatosha kuwa ni changamoto.


Mambo Ya Lazima Na Wakati Wa Swalah Ya 'Iyd

Baadhi ya wanavyuoni wa Kihanbali wanasema kuwa sharti za Swalah ya ‘Iyd ni iqaamah lazima isomwe na ni lazima iswaliwe kwa jamaa. Baadhi yao wamesema kuwa sharti za Swalah ya ‘Iyd ni sawa na zile za Swalah ya Ijumaa, isipokuwa katika khutba, ambapo kuihudhuria si lazima. Wengi miongoni mwa wanavyuoni wanasema wakati wa Swalah ya ‘Iyd unaanza pale jua linapochomoza kwa masafa ya urefu wa mshale, kwa linavyoonekana kwa macho matupu, na unaendelea mpaka jua linapokaribia kuwa sawa sawa.


Maelezo Ya Swalah Ya 'Iyd

‘Umar (Radhiya Allaahu ‘anhu) amesema:  “ Swalah ya ‘Iyd Fitwr na al-Adhw-haa ni rakaa mbili zilizotimia, sio fupi fupi. Hii ni kwa mujibu wa maneno ya Mtume, na muongo ni mwenye kulaaniwa.”

Abu Sa’iyd amesema: “Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amekuwa akija katika pahala pa kuswalia katika siku za Fitwr na al-Adhw-haa, na jambo la mwanzo analofanya ni kuswali”.

Takbira inarejewa mara saba katika rakaa ya mwanzo na mara tano katika rakaa ya pili, Qur-aan inasomwa baada yake katika kila rakaa.

Imeripotiwa kutoka kwa A’ishah: Takbira ya al-Fitwr na al-Adhw-haa ni mara saba katika rakaa ya mwanzo na mara tano katika rakaa ya pili, mbali na Takbira ya rukuu. (imeripotiwa na Abu Daawuud; imesahihishwa na jumla ya isnaad)

Iwapo mtu amejiunga na Swalah amemuwahi Imaam wakati wa Takbira hizi za ziada, ni juu yake kusema “Allaahu Akbar” pamoja na Imaam, na halazimiki kuzilipa Takbira ambazo zimempita, kwa sababu (takbira hizo) ni Sunnah, sio waajib. Kuhusu nini kinatakiwa kisemwe baina ya Takbira, Hammaad ibn Salamah ameripoti kutoka kwa Ibraahiym kuwa "Waliyd ibn ‘Uqbah aliingia msikitini wakati Ibn Mas’uud, Hudhayfah na Abu Muusa wapo hapo, na akasema, “‘Iyd ipo hapa, nini natakiwa kufanya?” Ibn Mas’uud akasema: “Sema ‘Allaahu Akbar’, msifu na mshukuru Allaah, msalie Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na omba du’aa, kisha sema ‘Allaahu Akbar’, msifu na mshukuru Allaah, mswalie Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)….n.k.’ (Imeripotiwa na at-Twabaraaniy. Ni hadiyth sahihi iliyonukuliwa katika al-Irwaa’ na kwengineko).



Kusoma Qur-aan Katika Swalah Za 'Iyd

Imependekezwa (mustahabb) kuwa katika Swalah za ‘Iyd, imaam asome surat Qaaf (sura ya 50) na surat al-Qamar (sura ya 54), kama ilivyoripotiwa katika Swahiyh Muslim kuwa ‘Umar ibn Al-Khattwaab alimuuliza Abu Waaqid al-Laythi, “Nini Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akisoma katika [‘Iyd] al-Adhw-haa na al-Fitwr?” Akasema, “Alikuwa akisoma Qaaf, Wal-Qur-aan al-Majiyd [Qaaf 50:1] na Iqtarabat as-saa’ah wa’nshaqq al-qamar [al-Qamar 54:1].

Ripoti nyingi zinaonyesha kuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akisoma Surat al A’laa [87] na Suurat al-Ghaashiyah {88], kama ambavyo alivyokuwa akizisoma katika Swalah ya Ijumaa. An-Nu’maan ibn Bashiyr amesema:

"Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akisoma katika '‘Iyd mbili na siku ya Ijumaa Sabbih Isma Rabbikal-a'laa (Al-A'alaa 87:1) na Hal Ataaka Hadiythul-Ghaashiyah (Al-Ghaashiyah 88:1)"  Swahiyh Muslim 878

Samurah (Radhiya Allaahu ‘anhu) amesema "Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akisoma katika ‘Iyd mbili Sabbih Isma Rabbikal-a'alaa (Al-a'alaa 87:1) na Hal Ataaka Hadiythul-Ghaashiyah (Al-Ghaashiyah 88:1) Imesimuliwa na Ahmad na wengine ni Swahiyh [ Al-Irwaa 3/116]


Swalah Inaswaliwa Kabla Ya Khutbah

Moja ya shari'ah za ‘Iyd ni kuwa Swalah ni lazima iwe kabla ya khutbah, kama ilivyoripotiwa katika Musnad Ahmad kutoka katika hadiyth ya Ibn ‘Abbaas, ambaye ameshuhudia kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliswali kabla ya khutba siku ya ‘Iyd kisha akatoa khutba (Musnad Ahmad 1905.  Hadiyth hii pia iko katika Swahiyh mbili)


Yeyote Anayetaka Kuondoka Wakati Wa Khutbah Ameruhusiwa Kufanya Hivyo

‘Abd-Allaah ibn al-Saab amesema: "Nilihudhuria '‘Iyd pamoja na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na alipomaliza alisema, tutatoa khutba, kwa hiyo anayetaka kukaa (na kusikiliza) khutba basi akae na anayetaka kuondoka basi aondoke (Irwaa al Ghaliyl 3/96)


Swalah Isicheleweshwe Kwa Muda Mrefu

‘Abd-Allaah ibn Bishr, swahaba wa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), alitoka pamoja na watu siku ya al-Fitwr au al-Adhw-haa, na akaonyesha kutopendezwa kwa kuwa Imaam alikuja akiwa amechelewa sana. Akasema: "Wakati wa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) tungelikuwa tumeshamaliza wakati wa sasa" na huo ulikuwa wakati wa Tasbiyh” (Imesimuliwa na na Al-Bukhaariy).


Swalah Za Sunnah, Pahala Pa Swalah (Ya 'Iyd)

Hakuna Swalah za Sunnah ambazo zinaswaliwa kabla au baada ya Swalah ya ‘Iyd, kama alivyoripoti Ibn ‘Abbaas kuwa "Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akitoka katika siku ya ‘Iyd na akaswali rakaa mbili, bila ya chochote (Swalah yoyote) kabla au baada yake". Hali hii ni iwapo Swalah itaswaliwa pahala pa kuswaliwa au sehemu ya wazi. Hata hivyo, iwapo watu wataswali ‘Iyd msikitini, basi watatakiwa waswali rakaa mbili za Tahiyat al-Masjid (Swalah ya kiamkizi cha msikiti) kabla hawajakaa kitako.


Iwapo Watu Hawatokuwa Na Habari Ya 'Iyd Mpaka Siku Ya Pili

Abu ‘Umayr ibn Anas ameripoti kutoka kwa ‘ami yake miongoni mwa Answaar kuwa alisema: "Kulikuwa na mawingu na hatukuweza kuuona mwezi wa Shawwaal, kwa hiyo tukaanza siku kwa kufunga, kisha ukaja msafara mwisho wa siku na wakamwabia Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa wameona mwezi wa Shawwaal siku moja kabla, akawaambia watu waache kufunga na wakaenda kuswali ‘Iyd siku ya pili"  Imeripotiwa na Maimaam watano, ni Sahiyh; Al-Irwaa' 3/102

Iwapo mtu amekosa Swalah ya ‘Iyd, mtazamo ulio sahihi kuliko yote ni kuwa anaweza kuilipa kwa kuswali rakaa mbili.


Kuhudhuria Kwa Wanawake Katika Swalah Za 'Iyd

Hafswah (Radhiya Allaahu ‘anha) amesema:  "Tulikuwa tukiwazuia wasichana wenye hedhi kuhudhuria Swalah za ‘Iyd.  Kisha akaja mwanamke kukaa katika ngome  ya Banu Khalaf na akatuambia kuhusu dada yake.  Mume wa dada yake alihudhuria  vita kumi na mbili  pamoja na   Mtume  (na akasema) ,  Dada yangu alikuwa naye katika vita sita.  Akasema tulikuwa tukiwatendea walioumia na tukiwashughulikia wagonjwa.  Dada yangu alimuuliza Mtume kama kuna ubaya wowote kutokwenda kuswali ‘Iyd ikiwa hana jilbaab.  Akasema "mwache rafiki yake ampe moja wa jilbaab lake ili aweze kushuhudia  baraka za ‘Iyd na aone kujumuika kwa Waislamu"  Ummu 'Atwiyah alipokuja nilimuuliza umemiskia Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema hivyo?" Akasema "Baba yangu achinjwe kwa ajili yake" Na alikuwa hamtaji ila baada ya kusema "baba yangu achinjwe kwa ajili yake". "Nimemsikia akisema kuwa wasichana na wale wanaotawishwa  au wasichana waliotawishwa na wanawake wenye hedhi  ili washuhudie baraka za ‘Iyd na kujumuika kwa waumini.  Lakini wale wenye hedhi wakae mbali na sehemu ya kuswali" (Swahiyh Al-Bukhaariy)

Vijana wa kike (‘awaatik, mmoja ‘aatiq) ni wale waliokwisha vunja ungo au wako karibu na kufanya hivyo, au wamefikia umri wa kuolewa, au walio na thamani katika familia zao, au wasiofanyishwa kazi zisizo na heshima. Inaonekana kuwa wamekuwa wakizuiwa vijana hawa kutoka nje kwa sababu ya uovu uliojitokeza baada ya kizazi cha kwanza cha Uislam; lakini Swahaabah hawakukubaliana na hilo na wakaona kuwa shari'ah ya wakati wao lazima ibaki kama ilivyokuwa wakati wa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).

 “Jilbaab lake”- ametakiwa kuazima baadhi ya nguo ambazo hakuwa akizihitajia.

“Wanaotengwa/Wanaotawishwa”- ambao wanaowekewa paazia kipembeni mwa nyumba ambamo wari hukaa nyuma yake.

“Wanawake walio katika hedhi”- huyyadh, mmoja haaidh– hii inaweza kurejea kwa vijana wa kike waliofikia umri wa kukua, au wanawake waliomo katika siku zao na wasio tohara.

“Wanawake walio katika hedhi wanatakiwa wajitenge na Swalah – pahala penyewe” – Ibn al-Munayyir amesema:   "Sababu ya kujitenga na sehemu ya kuswali ni kuwa wakisimama pamoja na wanawake wanaoswali japokuwa hawaswali, itaonekana kuwa hawana heshima na Swalah au hawajali kwa hiyo ni bora kwao kuepuka kufanya hivyo"

Imesemekana kuwa sababu ya kutakiwa wanawake walio katika hedhi kujitenga na sehemu ya kuswalia ni tahadhari, kuwa wanawake wasije karibu ya wanaume bila ya sababu iwapo wao hawaswali, au wasiwaudhi wengine kwa damu au harufu yake.

Hadiyth hii inamtaka kila mmoja kuhudhuria Swalah ya ‘Iyd, na kushirikiana baina yao katika wema na ucha Mungu. Wanawake walio katika hedhi wasiachwe nyuma katika  kumtaja Allaah au sehemu njema kama mikusanyiko yenye madhumuni ya kutafuta elimu na kumtaja Allaah – ukiachia misikitini. Hadiyth hii pia inaonyesha kuwa wanawake wasitoke nje bila ya jilbaab.

Hadiyth hii inatuambia kuwa sio sawa kwa vijana wa kike na wanawake wanaotawishwa kutoka nje bila ya sababu inayokubalika. Inasema kuwa imependekezwa (mustahabb) kwa wanawake kuvaa jilbaab, na kuwa imeruhusiwa kuazimana nguo. Pia imeonyesha kuwa Swalah ya ‘Iyd ni wajibu.

Ibn Abi Shaybah pia ameeleza kuwa Ibn ‘Umar alikuwa akienda na yeyote anayeweza kwenda naye katika wanawake wa nyumbani kwake katika Swalah za ‘Iyd.

Hadiyth ya Umm ‘Atwiyah pia inaeleza sababu ya shari'ah hii, ni kuwa ili wanawake waweze kushuhudia baraka ya ‘Iyd, waone mkusanyiko wa Waislam, na wapate nao baraka na utukufu wa siku hii.

At-Tirmidhiy (Mwenyeezi Mungu Amrehemu) alisema katina Sunan yake, baada ya kutaja Hadiyth ya Umm 'Atwiyah, "baadhi ya 'Ulamaa wamechukulia Hadiyth hii na kuwaruhusu wanawake waende katika Swalah za ‘Iyd na wengineo hawakupendezewa.  Imeripotiwa kuwa 'Abdullah Ibn Al Mubaarak alisema, 'Sipendi  wanawake waende katika Swalah  za ‘Iyd siku hizi.  Na mwanamke akishikilia kwenda basi mumewe amwachilie kwenda  lakini anapokwenda avae nguo zake kukuuu kabisa  na asijipambe.  Na akishikilia kujipamba basi asitoke nje.   Na hali hii mume anayo haki kumzuia kutoka nje.  Imeripotiwa  kuwa bibi 'Aishah (Radhiya Allaahu ‘anhu) alisema, "Kama Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) angeliona hali za wanawake walivyo hivi sasa angeliwazuia kwenda misikitini kama vile wanawake wa Bani Israaiyl walivyozuiliwa"  Imeripotiwa kwamba Sufyaan Ath-Thawriy hakupendezewa wanawake kwenda kuswali Swalah za ‘Iyd.   (At-Tirmidhiy 495)

Umm ‘Atwiyah ametoa fatwa yake katika hadiyth iliyotajwa hapo juu, muda baada ya kufa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kufariki, na haikuripotiwa kuwa yeyote miongoni mwa Maswahaba amepingana na fatwa hii. Maneno ya ‘Aa’ishah (Radhiya Allaahu ‘anha), “Iwapo Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) angeona yanayofanyika kwa wanawake, angewazuilia kwenda misikitini”, hayapingi hii fatwa (alimradi tu wanawake wanatimiza masharti ya Kiislamu ya kutoka kwao nje)  Ni vizuri zaidi iwapo ruhusa itatolewa kwa wale wanawake wasiotoka kwa ajili ya kuwaangalia wanaume au kuangaliwa wao, ambao kuhudhuria kwao hakutopelekea uovu wowote na wasiokwenda kusongamana na wanaume mitaani au msikitini (yaani wanawake ambao kutoka kwao hakutosababisha fitna au kishawishi kwake au kwa wanaume).

Wanaume wawakague wanawake wao wanapotoka nje kwa ajili ya Swalah kuhakikisha kuwa hijabu zao ziko kamili, kwa sababu wao ndio “wachungaji” wenye jukumu kwa “machunga” wao. Wanawake wanatakiwa watoke wakiwa katika nguo zisizovutia, wasiwe wamejipamba au kujitia manukato. Wanawake walio katika hedhi wasiingie msikitini au sehemu ya kuswalia; wanaweza kungojea ndani ya gari, kwa mfano, ambapo wanaweza kusikia khutbah.


ADAAB ZA 'IYD

Kukoga

Moja ya heshima za ‘Iyd ni kukoga kabla ya kwenda katika Swalah. Imeripotiwa katika ripoti sahihi katika al-Muwatta’ na kwengineko kuwa ‘Abd-Allaah ibn ‘Umar alikuwa akikoga siku ya al-Fitwr kabla ya kuja pahala pa kuswalia. (al-Muwattwa’428)

Imeripotiwa kuwa Sa'iyd ibn Jubayr alisema "Mambo matatu ni Sunnah siku ya ‘Iyd;  kwenda kwa miguu   katika uwanja wa kuswali (MuSwallaa), kukoga, na kula kabla ya kutoka nje".  Hivi ndivyo alivyosema Sa'iyd ibn Jubayr na labda amejifunza haya kutoka kwa baadhi ya Maswahaba.

An-Nawawiy (Radhiya Allaahu ‘anhu) ametaja kuwa wanavyuoni wamekubaliana kuwa imependekezwa (mustahab) kukoga kabla ya Swalah ya ‘Iyd.

Sababu ya kuwa ni mustahab kukoga kabla ya Swalah ya Ijumaa na mikusanyiko mengine pia inahusika katika suala la ‘Iyd vilevile.



Kula Kabla Ya Kutoka

Mtu asitoke kwenda pahala pa kuswalia ‘Iyd al-Fitwr kabla ya kula tende, kwa sababu ya hadiyth iliyosimuliwa na Al-Bukhaariy kutoka kwa Anas ibn Maalik ambaye amesema:

"Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa hatoki asubuhi ya ‘Iyd Al Fitwr mpaka ale tende na alikuwa kila kwa hesabu ya witri. (Al-Bukhaariy, 953)

Imependekezwa (mustahab) kula kabla ya kutoka kwa sababu hii inahakikisha kuwa hatukuruhusiwa kufunga katika siku hiyo, na ni onyesho kuwa Swawm sasa imemalizika. Ibn Hajar (rahimahu Allaah) ameeleza kuwa hii ni kwa ajili ya kuwakinga watu kuendeleza Swawm na pia inamaanisha utii kwa Allaah (Subhaanahu Wa Ta’ala). (Fat-hul-Baariy, 2/446).

Iwapo mtu hatakuwa na tende, anaweza kufutari kwa chochote kilichoruhusiwa. Kwa upande mwengine, katika ‘Iyd al-Adhw-haa, imependekezwa mtu asile mpaka baada ya Swalah, ambapo mtu anatakiwa kula nyama ya mnyama mmojawapo aliyechinjwa (kwa ajili ya siku hii).



Takbira (Allaahu Akbar) Katika Siku Ya 'Iyd

Hii ni moja ya Sunnah kubwa kabisa ya siku hii, kwa sababu ya maneno ya Allaah (yenye tafsiri):

"......Mwenyezi Mungu Anakutakieni yaliyo mepesi wala Hakutakieni yaliyo mazito, na mtimize hiyo hisabu, na mumtukuze Mwenyezi Mungu kwa kuwa Amekuongoeni ili mpate kushukuru"  [Al-Baqarah 2:185].

Ad-Daaraqutniy na wengine wameripoti kuwa wakati Ibn ‘Umar alipokuwa akitoka katika ‘Iyd al-Fitwr na al-Adhw-haa, huwa anajitahidi kutoa Takbiyr mpaka anapofika pahala pa kuswalia, kisha kuendelea na Takbiyr mpaka aje Imaam.

Tendo la kupiga Takbira kutoka nyumbani hadi pahala pa kuswalia, na mpaka Imaam aingie, ni maarufu miongoni mwa Salaf (waliotangulia wema) na limeripotiwa na waandishi wengi kama Ibn Abi Shaybah, ‘Abdur-Razzaaq na al-Firyaabi katika kitabu chake Ahkaam al-‘‘Iydayn kutoka katika kundi la Salaf. Moja ya mfano wake ni ripoti kuwa Naafi’ ibn Jubayr alikuwa akitoa Takbira na alikuwa akishangaa kwa nini watu hawafanyi hivyo. Alikuwa akiwaambia watu, "Kwa nini hamfanyi Takbira? Ibn Shihaab Az-Zuhri kasema, "Watu walikuwa wakipiga takbira kuanzia wakati wanapotoka majumbani mwao hadi anapoingia Imaam".

Wakati wa kutoa Takbira katika ‘Iyd al-Fitwr unaanza usiku wa kuamkia ‘Iyd mpaka wakati Imaam anapofika kuongoza Swalah.


Maneno Ya Takbira

Ibn Abi Shaybah ameripoti katika al-Muswannaf kuwa Ibn Mas’uud (Radhiya Allaahu ‘anhu) alikuwa akitamka takbira katika siku za Tashriiq kama ifuatavyo: “Allaahu Akbar, Allaahu Akbar, laa ilaaha illa-Allaah, wa Allaahu Akbar, Allaahu Akbar wa Lillaahi’l-hamd (Allaah ni Mkubwa kabisa ….hakuna Mungu isipokuwa Allaah, Allaah ni Mkubwa kabisa, na sifa zote njema ni za Allaah)’. Ibn Abi Shaybah aliripoti haya mahala pengine katika isnaad hiyo hiyo, lakini ikiwa na pamoja na maneno “Allaahu Akbar” ikirejewa mara tatu.

Al-Muhaamili pia ameripoti kuwa Ibn Mas’uud alikuwa akisema : “Allaahu Akbar kabiyran, Allaahu Akbar kabiyran, Allaahu Akbar wa ajall, Allaahu Akbar wa Lillaahi’l-hamd (Allaah ni Mkumbwa kabisa, Allaah ni Mkubwa kabisa, Allaah ni Mkubwa kabisa, Allaah ni Mkubwa kabisa na Mtukufu, na sifa zote njema ni za Allaah)”. (al-Irwaa’, 3/126).


Kupongezana

Watu wanaweza kupeana pongezi na Salaam njema za ‘Iyd, bila ya kujali aina ya maneno. Mfano wanaweza wakaambizana, “Taqabbal Allaah Minnaa Wa Minkum (Allaah Azikubali [Swawm na ibada] zetu na zenu” au “‘Iyd Mubaarak” na mfano wa hayo katika Salaam zilizoruhusiwa.

Tendo la kupeana Salaam limekuwa maarufu wakati wa Maswahaaba na wanavyuoni kama Imaam Ahmad na wengine wameruhusu hilo. Kuna ripoti zinazoonyesha imeruhusiwa kuwapongeza watu katika matukio maalum. Maswahaba walikuwa wakipongezana wakati linapotokea jambo zuri, mfano pale Allaah Alipokubali toba ya mtu n.k.

Hakuna shaka kuwa kumpongeza mtu kwa namna hii ni moja kati ya namna ya heshima zaidi katika tabia njema na ni moja kati ya muamala mzuri sana wa jamii ya Waislam.


Kuvaa Vizuri Zaidi Siku Ya 'Iyd

'Abdullaah bin 'Umar (Radhiya Allaahu ‘anhu) amesema, 'Umar alichagua jubbah (nguo refu inayovaliwa juu ya kanzu) ambayo ilitengenezwa kwa hariri na ilikuwa ikiuzwa kwa bei ya takhfifu sokoni, aliileta kwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na akasema, "ewe Mtume nunua hii na uvae kwa ajili ya ‘Iyd na watakapokuja wageni"  Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema "Hizi ni nguo za yule ambaye hana sehemu akhera (imeripotiwa na Al-Bukhaariy 948)

Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikubaliana na mawazo ya ‘Umar (Radhiya Allaahu ‘anhu) ya mtu kuvaa vizuri zaidi, lakini alikataa na kupingana na mawazo ya kununua jubbah hilo kwa sababu lilikuwa limetengenezwa kwa hariri.

Al-Bayhaqiy ameripoti kuwa Ibn ‘Umar alikuwa akivaa nguo zake nzuri siku ya ‘Iyd, kwa hivyo wanaume wanatakiwa wavae nguo nzuri zaidi walizokuwa nazo wanapotoka kwa ajili ya ‘Iyd.

Kwa upande mwengine, wanawake, wajiepushe na mapambo wanapotoka kwa ajili ya ‘Iyd, kwa sababu wao wamekatazwa kuonyesha mapambo yao mbele ya wanaume wasio mahrim (wasio na uhusiano nao wa damu) zao. Mwanamke anayetaka kutoka ameharamishiwa kujitia manukato au kujionyesha kwa njia ya kushawishi mbele ya wanaume, kwa sababu yeye ametoka kwa ajili ya ibada tu. Je, unafikiria kuwa ni sahihi kwa mwanamke muumini kumuasi Yule Ambaye yeye (mwanamke) anatoka kwenda kumuabudu, na kwenda kinyume na amri Zake kwa kuvaa nguo za kuvutia zenye kumbana na za rangi zinazong’ara au kujitia manukano n.k?


Shari'ah Katika Kusikiliza Khutba Za 'Iyd

Ibn Qudaamah (Radhiya Allaahu ‘anhu) amesema katika kitabu chake cha al-Kaafi (uk.234):

Imaam anapotoa Salaam (mwisho wa Swalah) atoe khutba sehemu mbili kama khutbah ya Ijumaa kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alifanya hivyo.  Khutba ya ‘Iyd ni tofauti  na khutbah ya Ijumaa kwa mambo manne, jambo la nne ambali ni Sunnah na sio fardhi kusikiliza kwa sababu imeripotiwa kwamba 'Abdulla bin Al-Saa'ib alisema, "Nilihudhuria ‘Iyd na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)  na alipomaliza kuswali, alisema "tutatoa khutbah sasa kwa hiyo anayependa kukaa (na kusikiliza) akae na yeyote anayetaka kuondoka basi na aondoke".  

Katika al-Sharh al-Mumti’  ‘ala Zaad al-Mustanfi’ cha Ibn ‘Uthaymiin, 5/192, kinasema:

“Maneno [ya Ibn Qudaamah], ‘kama khutbah mbili za Ijumaa’ inamaanisha kuwa anatakiwa atoe khutbah mbili, hata kama kuna kutokubaliana katika jambo hili, kama ambavyo tumetaja hapo juu. Khutbah ya ‘Iyd, imeegemea katika  shari'ah zilizo sawa na za Ijumaa, hata katika nukta ya kuzungumza wakati wa khutbah hiyo ni haraam, lakini sio wajibu kuhudhuria, hali ya kuwa kuhudhuria khutbah ya Ijumaa ni wajibu, kwa sababu Allaah (Subhaanahu Wa Ta’ala)) Amesema:

"Enyi mlio amini! Ikiadhiniwa Swalah siku ya Ijumaa, nendeni upesi kwenye dhikri ya Mwenyezi Mungu, na wacheni biashara" Al-Jumu'aah :9

 Kuhudhuria khutbah ya ‘Iyd sio wajibu, na mtu anaruhusiwa kuondoka, bali iwapo atabakia, ni lazima asizungumze na yeyote. Hivi ndivyo muandishi alivyokusudia aliposema ‘kama khutba mbili za Ijumaa’. “

Mmoja wa wanavyuoni amesema: “Si wajibu kusikiliza khutba za ‘Iyd, kwa sababu kama ingelikuwa ni wajibu kuzihudhuria na kuzisikiliza basi ingekuwa ni haraam kuondoka. Lakini kwa kuwa imeruhusiwa kuondoka, basi si wajibu kusikiliza”.

Hata hivyo, iwapo mazungumzo yatawakera wale wanaosikiliza, ni haraam kuzungumza kwa sababu ya kero hizo, sio kwa sababu ya kutokusikiliza. Kwa msingi huu, iwapo mtu atakuwa na kitabu wakati Imaam anakhutubia, basi ameruhusiwa kukisoma, kwa sababu kufanya hivyo hakutomkera yeyote.


Mtu Kutoka Kwa  Njia Moja Na Kurudi Kwa Kutumia Njia Nyengine

Jaabir bin ‘Abd-Allaah (Radhiya Allaahu ‘anhu) ameripoti kuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akibadilisha njia siku ya ‘Iyd. (imeripotiwa na al-Bukhari, 986)

Imeripotiwa kuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akitoka kwa miguu, na alikuwa akiswali bila ya adhana wala iqaamah, kisha hurudi kwa kutumia njia nyengine tofauti. Inasemekana kuwa njia hizi mbili zitamtolea ushahidi siku ya Qiyaamah, kwa sababu siku hiyo ardhi itasema juu ya kila kitu kilichofanywa juu yake, zuri na baya. Vile vile inasemekana kuwa imefanywa hivi ili kuonyesha alama na utamaduni wa Kiislam katika njia zote mbili; kutoa ukumbusho wa Allaah; kuwavunja moyo wanafiki na  Mayahudi na kuwaogopesha kwa wingi wa watu walio pamoja nae; kutimiza mahitaji wa watu kwa kuwapa fatwa, kuwasomesha na kuwawekea mifano ya kuifuata; kuwapa sadaka wale wanaohitajia; au kuwatembelea jamaa zake na kukuza mahusiano yao.


Tahadhari Juu Ya Kufanya Maovu

Baadhi ya watu wanadhani kuwa Uislam unatuambia kukesha na kuswali usiku wa ‘Iyd, kwa kunakili hadiyth ya uongo inayosema "Yeyote atakayekesha usiku wa ‘Iyd moyo wake hautokufa siku ya kufa moyo wake"  Hadiyth hii imeripotiwa katika isnaad mbili moja ambayo ni dhaifu na ya pili ni dhaifu sana.  Uislam hautuambii kuutenga usiku wa ‘Iyd kwa kukesha na kusali; hata hivyo, iwapo mtu ana tabia ya kuamka na kusali usiku (Qiyaam), hakuna ubaya wa kufanya hivyo katika usiku wa ‘Iyd pia.
Mchanganyiko wa wanawake na wanaume katika maeneo ya Swalah, mitaani, n.k. Inasikitisha kuwa haya yanatokea sio misikitini tu, bali hata katika sehemu tukufu zaidi, al-Masjid al-Haram [Makkah]. Wanawake wengi, Allaah Awaongoze  wanatoka wakiwa hawajajisitiri, wamejipamba na kujitia manukato, wanaonyesha mapambo yao, wakati kuna mkusanyiko mkubwa katika msikiti huo. Hatari ya hali hii iko wazi kabisa. Kwa hiyo wale wahusika ni lazima wapange Swalah za ‘Iyd vizuri, kwa kuweka milango tofauti na njia tofauti kwa wanawake na wawacheleweshe wanaume kutoka mpaka wanawake wawe wameshatoka.
Baadhi ya watu wanajikusanya siku ya ‘Iyd kwa ajili ya kuimba na kufanya aina nyengine za ….burudani, na hii haikuruhusiwa.
Baadhi ya watu wanashereheka katika ‘Iyd kwa sababu Ramadhaan imemalizika na kuwa hawahitajiki tena kufunga. Haya ni makosa, waumini wanasherehekea ‘Iyd kwa sababu Allaah Amewasaidia wao kumaliza mwezi wa Swawm, sio kwa sababu ya kumalizika kwa Swawm ambayo watu wengine wanaichukulia kuwa ni mzigo.

Tunamuomba Allaah Azikubali ibada zetu na toba zetu. Allaah Ampe rehma Mtume wetu Muhammad.

MSIMAMO WA WAISLAMU KUHUSU SENSA 2012


JUMUIYA NA TAASISI ZA KIISLAMU TANZANIA
MSIMAMO WA WAISLAMU KUHUSU SENSA 12

Utangulizi:
Suala la sensa ya watu na makazi ktk Uislamu ni mas’ala yenye mafundisho kutoka kwa Qur’an 8:60 na
kutoka ktk Sunnah ya Mtume (swalla Allwaahu ‘alayhi wasallam) na Makhalifa waongofu.
Katiba ya Jamhuri Ibara ya 18 (1) na (2) inatambua haki ya wananchi kutoa na kupata habari;-
                  “18. -(1) Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje
                    mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote
                    bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati”.
                   “(2) Kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali nchini na
                    duniani kote ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi, na pia juu ya masuala
                     muhimu kwa jamii”.

Vile vile Umoja wa Mataifa unaelekeza jinsi ukusanyaji wa sensa za watu kwa mujibu wa dini zao
unavyopaswa uwe na kwa kutaja si tu dini za watu bali hata madhehebu zao kama dini ina
madhehebu.

Para 2.109 inasema “For census purposes, religion may be defined as either religious or spiritual belief
of preference, regardless of whether or not this belief is represented by an organized group, or
affiliation with an organized group having specific religious or spiritual tenets”.

Para ya 2.111 inasema “For the benefit of users of the data who may not be familiar with all of the
religions or sects within the country, as well as for purposes of international comparability, the
classifications of the data should show each sect as a subcategory of the religion of which it forms a
part. A brief statement of the tenets of religions or sects that are not likely to be known beyond the
country or region would also be helpful” ( www.unstats.un.org)


2. Historia ya mgogoro wa waislamu kutokushiriki zoezi la sensa 2012
Mgogoro uliopo baina ya serikali na waislamu kuhusu kuwekwa kipengelel cha dini haukuanza ghafla tu. Waislamu wameshiriki sensa zisizo na kipenghelel cha dini pasina malalamiko yoyote tangu ile 1978, 1988 na 2002. Hatukuw ana sababu yoyote kudai kiwekwe kipengele cha dini katika sense pamoja na kutambua kwamba takwimu za mwaka 1967 zilichakachuliwa na pia kuna takwimu feki juu ya idadi ya waislamu na wakristo zipo katika machapisho mbalimbali na mitandao mbalimbali.

Mtazamo wetu ulianza kubadilika tulipoanza kuona kalenda zenye nembo na bendera ya taifa zikiwemo zilizotiolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Takwimu za Bodi ya Utalii, shajara (diary) ya mwaka 2010 iliyotolewa na Wizara ya mambo ya Ndani n.k. zikionesha kwamba idadi ya wakristo nchini ni kubwa kuliko ya waislamu. Takwimu hizi zilimaanisha jambo moja tu- kwamba takwimu hizi zinatambulika kiserikali.

Mgongano wa kwanza kati ya waislamu kwa upande mmoja na serikali na Makanisa kwa upande mwingine kuhusu suala hili la sensa ya mwaka huu ni uliotokea katika mkutano ulioitishwa na idara ya takwimu White Sands Hotel Dar es Salaam ambapo viongozi wa Kikristo na Kiislamu walikutana kujadili maandalizi juu ya sensa.

Waislamu waliitaka idara ya ya takwimu kuthibitisha kama takwimu zilizotolewa na TBC1 siku ya tarehe
26 Aprili, 2012 kwamba wakristo ni wengi kuliko waislamu ambapo wakristo 52% na waislamu 32% na wapagani 16% ni sahihi au la. Mkurugenzi wa Idara ya Takwimu akasema takwimu hizo si sahihi kwa sababu serikali tangu 1967 haijaweka kipengele cha dini katika sensa yoyote ile baada ya hiyo.

Viongozi wa Kiislamu wakaonesha takwimu mbali mbali zilizopo katika maandiko na tovuti mbalimbali na kuitaka idara ya takwimu kwa kuwa inaonekana takwimu hizi za idadi ya wakristo na waislamu zinahitajika nchini na kimataifa, basi katika dodoso la sensa mwaka huu kipengele hicho kiwekwe.

Mkurugenzi wa Idara ya takwimu akasema serikali ilikiondoa kipengele hicho mwaka 1967 kwa ajili ya kuleta umoja wa kitaifa kwa hiyo haiwezi kukiweka. Waislamu walipinga hoja hiyo kwa kusema hakuna ushahidi wowote kwamba umoja wa kitaifa utatoweka kwa kuweka kipengele cha dini na kuna nchi nyingi tu duniani zinatoa takwimu za sensa kwa mujibu wa dini na wala amani haijatoweka.

Mfano Uingereza, India, Kenya, Ethiopia, Uganda, Malawi n.k. Kinachohatarisha amani si kuweka kipengele cha dini katika dodoso la sensa bali hizi takwimu za uongo kwamba watu fulani ni wengi kuliko wengine wakati hakuna sensa iliyofanyika kuhusu suala hili.

Katika mkutano huo wa White Sands, viongozi wa Kikristo wote waliunga mkono kutokuwekwa kipengele cha dini katika sensa. Waislamu walipohoji kama kuna hatari ya kuvunjika umoja wa kitaifa, mbona dodoso la sensa lina kipengele cha makanisa na misikiti? Kama kujua majumba hayo ya ibada hakuvunji umoja wa kitaifa, iweje kujua wafanya ibada au wenye kujinasibisha na majaumba hayo ya ibada kuvunje umoja wa kitaifa? Hakukuwa na majibu bali idara ya takwimu ikashikilia msimamo wake.


Mkutano wa Viongozi wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Dar es Salaam.
Baada ya mkutano wa viongozi wa dini na idara ya takwimu White Sands Hotel, na baada ya kuona msimamo wa serikali ni kutokuweka kipengele che dini, viongozi wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu wakakutana jijini Dar es Salaam tarehe 29 Juni, 2012 kujadili suala hili. Katika mkutano huo, umauzi ulifikiwa kuiandikia idar aya takwimu ombi rasmi la kuitaka iweke kipengele cha dini katika dodoso la sensa la sivyo waislamu hawatoshiriki. Jumuiya na Taasisi ziliandika barua hiyo tarehe 4 Juni, 2012 iliyosainiwa na viongozi wa Mumuiya na Taasisi za Kiislamu isipokuwa Bakwata na zilitoa hadi tarehe 20 Juni, 2012 idara hiyo iwe imefanya hivyo laa sivyo waislamu watasusia zoezi la sensa mwaka huu.

Mkutano wa Dodoma tarehe 11 Juni, 2012
Wakati tukisubiri majibu ya barua yetu kwenda idara ya takwimu, tukapata mwaliko wa idara hiyo tarehe 8 Juni, 2012 kwenda Dodoma kuhudhuria semina ya siku moja ya viongozi wa dini juu ya masuala ya sensa .

Katika semina hiyo, waislamu wakalileta tena suala hili mbele ya idara ya takwimu na likajadiliwa na pande tatu – wakristo, waislamu na serikali. Msimamo wa viongozi wa kikristo na serikali ukawa kama siku ya mkutano wa White Sands Hotel kwamba serikali haitoweka kipengele cha dini. Baada ya waislamu kutoa hoja zisizojibika, TBC1 ikalazimika kukanusha tena takwimu walizozitoa kama moja ya juhudi za kuwafanya waislamu waache msimamo wao.

Hatimaye viongozi wa idara ya takwimu wakakubali kuchukua maoni ya waislamu na kuahidi kuyafanyia kazi. Lakini wakati akifunga semina hiyo, Waziri Ofisi ya Rais Sera na Uhusiano Mhe.Stephen Wasira, alitoa msimamo wa serikali kwamba “serikali haiwezi kuweka kipengele cha dini kwa sababu haipangi maendeleo kwa kipengele cha dini!!!Huku waislamu wakijua kuwepo kwa MoU kati ya Makanisa na Serikali, serikali kupanga mipango ya maeneo ya ibada, makaburi n.k. kwa dini mbali mbali” Waislamu walipotaka kuhoji, waziri alikataa na kuwaambia “kama ninyi hamkuelewa somo wenzenu (wakristo) wameelewa”, kauli ya kejeli kwa masheikh na viongozi wa Kiislamu waliohudhuria pale.

Viongozi wa Kiisalamu waliohudhuria semina hiyo jioni ya siku hiyo wakakaa na kuandika barua ya pamoja kwa idara ya takwimu kupinga msimamo huo wa serikali na kauli za kejeli za Mhe. Wasira kwa viongozi wa Kiislamu. Barua hiyo ikasainiwa na viongozi wote wa wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu waliohudhuria semina hiyo ambao wanafikia 31 wakiwemo Bakwata.

Mkutano wa pili wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Dar es Salaam 13 Juni, 2012
Baada kurejea Dar es Salaam, masheikh na viongozi wa Jumuiya na Taasisi mbali mbali za Kiislamu walipokea taarifa ya wajumbe waliokwenda Dodoma na kuijadili ambapo paliamuliwa itolewe Press Release kwa vyomboo vya habari kusisitiza msimamo wa kutokushiriki sensa kwa kuwa serikali imepuuza madai ya waislamu pasina hoja za msingi.

Press Conference ikafanyika Makao makuu ya Bakwata Kinondoni na likatoka tamko rasmi la waislamu
kwamba hawatoshiriki sensa ya mwaka 2012 hadi yafuatayo yafanyike;-
                 1. Kipengelel cha dini kiwekwe katika dodoso la sensa.
                 2. Kuwepo na uangalizi wa pamoja kati ya waislamu na wakristo kwa kuwa tayari kila upande
                  unadai wao ni wengi kuliko upende mwingine.


Tamko la Mufti wa Bakwata kuwataka waislamu kushiriki sensa.
Katika hali iliyotarajiwa na wengi na isiyo ya kushangaza, Mufti wa Bakwata akaitisha mkutano na waandishi wa habari Makao Makuu ya Bakwata tarehe 24 Juni, 2012 na kuwataka waislamu kushiriki sensa kwa sababu haina tatizo.

Viongozi wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu wakalipokea tamko hili na kulipuuza kwa sababu tangu mwanzo Mufti wa Bakwata alitangaza kuunga mkono tu msimamo wa Jumuiya na Taasisi za Kiisalmu akiwa Tanga kwa hiyo maamuzi hayo ni maamuzi yake binafsi au san asana ni ya Bakwata tu. Jumuiya na Taasisi zikaamua kuendelea na msimamo wa awali wa kutokushiriki sensa na msimamo huu ukatolewa tarehe 27 Juni, 2012 mbele ya waandishi wa habari lamada Hotel Dar es Salaam.

Na huu ndio msimamo wa Jumuiya na Taasisi hadi hapo serikali iamue kutekeleza matakwa hayo mawili kabla ya muda wa sensa ijayo kuanza kwa mwezi mzima ili kuruhusu Jumuiya na Taasisi kutoa tena maelekezo kwa waumini wake kushiriki sensa. Kama hili halikufanyika ni wazi kwamba tutakuwa khiyari ila kutekeleza maamuzi ya viongozi wa Jumuiya na Taasisi.


3. Historia ya Sensa Tanzania
Sensa imefanyika hapa nchini mara nane tangu ukoloni- 1921, 1931, 1948, 1957, 1967, 1988, 1978, 2002 na inatarajiwa kufanyika tena mwaka huu 2012. Lengo la sensa ya watu na makazi ni kuiwezesha serikali na wananchi kujua idadi ya watu na hali za makazi yao na hivyo kusaidia mipango ya maendeleo ya serikali nay a jamii husika na hat akuwawezesha wayu kudai haki zao.

Ingawa jamii mbali mbali zinaweza kujihesabu zenyewe, bado sensa inayoendeshwa na serikali ndiyo inayotambulika kisheria kitaifa (credibile) na kimataifa. Ndiyo maana idara ya takwimu ya taifa ilikanusha takwimu hizo baada ya kutakwa na waislamu kutoa kauli juu ya takwimu mbali mbali za idadi ya waislamu na wakristo, ikiwemo ile iliyotolewa na TBC1 siku ya Muungano mwaka huu.

Sensa ya mwisho kuwa na kipengele cha dini ni ile ya mwaka 1967 ambayo kwa mujibu wa wanahistoria ilichakachuliwa kwa maslahi ya kisiasa kuonesha wakristo ni wengi kuliko waislamu (Wapagani 34.3%, Wakristo 33.5% na Waislamu 31.4%). Katika kitabu Globalization, modernization, and education in Muslim countries mwandishi Rukhsana Zia ameandika;-
           “However, according to the first post-independence census of 1967, Christians were 32 percent,  
            Muslims 30 percent ... Unfortunately, that controversial 1967 population census was the last one to
            show religious distribution in Tanzania”.

Kwa hiyo sensa ya mwaka 1967 ilikuwa na kipengele cha dini lakini takwimu, zake ambazo ndizo zilizoweka msingi wa takwimu za sasa zinazoonesha wakristo kuwa wengi kuliko waislamu, zilichakachuliwa kwa makusudi ili kuonesha kuwa wakristo ni wengi kuliko waislamu kuhalalisha dhulma mbali mbali ambazo waislamu wamekuwa wakifanyiwa katika elimu, madaraka, ajira, uchumi na huduma za jamii.

Madai ya waislamu kuwa pawekwe kipengele cha dini katika sensa hii ni juhudi za kudai haki na uadilifu utendeke kuhusu takwimu za idadi ya waislamu na wakristo nchini ili takwimu zisipotoshwe tena. Kwa hiyo msimamo wetu si wa kubahatisha hata kidogo, ni msimamo wa haki na unastahiki kuungwa mkono na wapenda haki wote.


5. Faida za kujua idadi ya wananchi kwa mujibu wa dini zao.
Faida ziko nyingi kwa sababu matumizi ya takwimu za idadi ya watu kwa mujibu wa dini zao ni mengi.
        i) Zitawezesha kuondoa utata uliopo na kujua takwimu za kweli. Taifa halipaswi kutegemea takwimu za
           uongo kuhusu idadi ya rai wake kwa mujibu wa dini zao.
       ii) Takwimu sahihi za watanzania kwa mujibu wa dini zao zitaiwezesha serikali makini kujua mahitajio
           halisi ya wana dini ingawa serikali haina dini. Katiba kusema serikali haina dini haina maana kwamba
           ndiyo isijishughulishe na mahitaji ya kidini ya raia wake. Ndiyo maana serikali imetoa misamaha ya
           kodi kwa mashirika ya dini ili yaweze kuhudumia wana dini wao.
      iii) Serikali hutenga maeneo mbali mbali kwa ajili ya majumba ya ibada na shughuli nyingine za kidini
           kama vile makaburi. Kwa kujua takwimu hizi, serikali itapanga vizuri mipango hiyo kwani itakuwa
           inazo takwimu halisi za idadi ya watu wake kwa mujibu ya dini zao. Kama serikali isipojua idaidi ya
           wafuasi wa dini fulani itawezaje kugawa maeneo hayo sawasawa kwa mujibu wa idadi ya wana dini
           mbali mbali? Ndiyo maana kwa kutumia takwimu feki zilizoko serikali hugawa maeneo makubwa
           makubwa kwa wakristo na waislamu kuambulia maeneo madogo tu.
      iv) Serikali mara nyingi inahimiza viongozi wa dini kuwaelimisha waumini wao juu ya masuala mbali mbali  
           kama vile uharibifu wa maadili, Ukimwi na VVU, madawa ya kulevya, ulinzi shirikishi n.k. Kama
           serikali itajua idaidi ya watanzania kwa dini zao itaweza kuelewa wka uhakika ni watu wangapi
           wanafikiwa na mipango ya serikali kupitia dini zao.

       v) Wawekezaji na wagenii mbali mbali wakiwemo watalii wanaotembelea Tanzania, kwa mujibu wa
           utaratibu wa kimataifa, hutaka kujua habari mbali mbali juu ya nchi yetu ikiwemo takwimu ya idadi ya
           watu, makabila yao, dini zao n.k. ili wajiandae kukabiliana na mazingira yetu ya kimaadili na
           kiutamaduni. Kujua takwimu rasmi zilizotolewa na serikali kutawasaidia wawekezaji na hata watalii
           kuwajua watanzania kwa mujibu wa dini zao.

     vi) Hali kadhalika, wana dini husika, ingawa kila dini inao utaratibuwa kujua wafuasi wake, watanufaika
          na takwimu za idadi ya watu kwa mujibu wa dini zao kwani takwimu zitakazotolea kwa mujibu wa
          sensa ya serikali zinapatikana kwa upana zaidi (comprehensive) kuliko zile zinazokusanywa na dini
          husika. Kwa hiyo zitasaidia hata viongozi wa dini kupanga mipango yao ya kuwahubiria watanzania
          maadili mema, kupinga maovu na uhalifu na hivyoo kuchangia amani iliyopo.


5. Kama Serikali haitoweka kipengele cha dini katika dodoso la sensa msimamo wetu ni nini?
Katika mazingira yaliyopo ambapo dodoso la sensa limeweka kipengele cha majumba ya ibada (kanisa alama ya Msalaba, msikiti alalama ya mwezi mchanga na nyota) na hata makaburi, ambayo kwa bahati mbaya alama yake ni misalaba mitatu (pengine kuwakilisha TEC, CCT na PCT) hakuna alama ya makaburi ya waislamu, tunahisi kwamba zoezi zima hili linafanyika kwa maslahi ya Kanisa.

Kwa mujibu wa hali tunayoiona na kwa mujibu wa takwimu zinazoonesha kwamba wakristo nchini ni wengi kuliko waislamu ambazo tayari zinatolewa na Makanisa na hata idara za serikali na mashirika ya nje ya nchi, tunaona kwamba kushiriki kwetu katika sensa hii kabla ya kipengele cha dini kuwekwa na kabla ya kuhakikisha kwamba mazingira ya kuchakachuliwa takwimu kama ilivyotokea 1967 hayajawekwa ni sawa na kujitia kitanzi wenyewe kwa kuhalalisha dhulma dhidi ya waislamu.

Iwapo serikali itaweka kipengele cha dini katika sensa na kuweka mazingira ya uangalizi wa pamoja wa waislamu na wakristo (observers) hata pasina kugharimiwa na serikali kufuatilia zoezi la sense kuanzia kuhesabu, kujumlisha na kutoa matokeo angalau mwezi mmoja kabla ya zoezi hili, tutaangalia uwezekano wa kushiriki katika zoezi la sensa mwaka huu.

6. Kuhusu zoezi la Vitambulisho vya Taifa
Jumuiya na Taasisi hazina kipingamizi chochote juu ya zoezi hili ingawa hadi sasa hatuna maelezo yoyote ya kina juu yake na tunachunguza mwenendo mzima kisha tutawaambia waislamu.Iwapo pia tutagundua udini katika zoezi hili, hatutasita kuwaambia waislamu juu ya dosari zilizopo. Hata hivyo hadi sasa kuna kipengele kilichoandikwa “Cheti cha Ubatizo/Falak…….” ambacho kwa kuwa kuna mialiko imetoka kuwaita masheikh na maimamu kwenye semina juu ya zoezi la vitambulisho vya taifa, tutaulizia huko.

Hali kadhalikak wasi wasi wetu ni kwamba huonda zoezi hili likatumika kuongeza idadi ya wakristo kwa sababu kielelezo kimojawapo kinachotumika ni cheti cha ubatizo wakati katika waislamu hakuna cheti ya utambulisho bali Shahada “Laa ilaaha illa-llwaahu Muhammadan Rasuulu-llwaahu” tu. Wenye vyeti ni wale waliosilimu tu.

Wabillahi Tawfiiq

Tuesday, August 07, 2012

Laylatul-Qadr- Vipi Tunaweza Kuupata Usiku Huu?

Tunaingia kumi la mwisho, kumi ambalo ndani yake kuna siku tukufu, siku ya Laylatul-Qadr, ambayo ibada yake ni bora kuliko ibada ya miezi elfu. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala: ﴿


 بِسْمِ اللّهِ الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ ﴾ إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةِ الْقَدْرِ - وَمَا أَدْرَاكَ مَا لَيْلَةُ الْقَدْرِ - لَيْلَةُ الْقَدْرِ خَيْرٌ مِّنْ أَلْفِ شَهْرٍ - تَنَزَّلُ الْمَلَائِكَةُ وَالرُّوحُ فِيهَا بِإِذْنِ رَبِّهِم مِّن كُلِّ أَمْرٍ - سَلَامٌ هِيَ حَتَّى مَطْلَعِ الْفَجْرِ 
KWA JINA LA ALLAAH MWINGI WA REHMA MWENYE KUREHEMU - Hakika Sisi Tumeiteremsha Qur-aan katika Laylatul Qadr, Usiku wa Cheo Kitukufu -Na nini kitachokujuulisha nini Laylatul Qadr?- Laylatul-Qadr ni bora kuliko miezi elfu - Huteremka Malaika na Roho katika usiku huo kwa idhini ya Mola wao Mlezi kwa kila jambo - Amani usiku huo mpaka mapambazuko ya alfajiri. [Al-Qadr: 1-5) 

 Vile vile dalili katika Hadiyth mbali mbali zimethibiti kuhusu Fadhila za usiku huu mtukufu, na jinsi Mtume (swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alivyokuwa hali yake katika siku hizi kumi za mwisho za Ramadhaan. 

 Baada ya kuzijua fadhila zake usiku huu mtukufu inakupasa Muislamu ujikaze katika siku kumi hizi za mwisho kuacha mambo yote yanayokushughulisha ya dunia na utumbukie katika ibada tu ili uweze kuupata usiku huo mtukufu, yaani ukukute wewe ukiwa katika ibada ili zihesabiwe ibada zako kama kwamba umefanya ibada ya miezi elfu. 


 Tukifanya hesabu miezi elfu hiyo ni sawa na umri wa miaka 83! 1000 ÷ 12 = 83.3 yaani miaka themanini na tatu na miezi mitatu takriban. Hivyo ikiwa Laylatul-Qadr imekukuta katika ibada ya aina yoyote, ikiwa ni Swalah (Qiyaamul-Layl), kusoma Qur-aan, kufanya aina za dhikr, kutoa sadaka, kulisha chakula, kuwasiliana na jamaa, kujielimisha au kuelimisha, kufanya wema kwa watu, yote hayo utaandikiwa kama umefanya hayo kwa umri wa miaka 83! 

Na juu ya hivyo ibada hiyo ya usiku mmoja tu ni bora zaidi kuliko ibada utakayoweza kufanya miaka 83 na miezi mitatu. Subhaana Allaah! Jihadhari ndugu Muislamu usije ukakukuta usiku huu mtukufu ukiwa katika maasi au katika sehemu ukiwa umeghafilika na ya dunia kama sokoni, magenge ya soga au michezo ya kupoteza wakati au kwenye televisheni ukiangalia misalsalaat, mipira na sinema zikakupita kheri zote za usiku huu. Utaona siku hizi Waislamu wengi wanashughulika kwenda madukani kutafuta nguo za 'Iyd khaswa kina dada wakiacha masiku haya yawapite wakiwa humo badala ya kuwa majumbani mwao au misikitini kufanya ibada na kutegemea kuupata usiku huu.

 Ni siku chache tu ndugu Waislamu ambazo zinakimbia kama upepo. Je, nani basi katika sisi atakayepuuza asiupate usiku huo? Na Nani katika sisi atafanya hima kuupata usiku huo? Kwani hatujui kama tutakuweko duniani mwakani kuzipata siku hizi au hata hatujui kama tutaikamilisha Ramadhaan hii. Basi tujitahidi kwa kukesha siku kumi hizi na kuamsha familia zetu ili iwe kheri yetu kukutana na usiku huo mtukufu tuweze kupata fadhila zake hizo ambazo ni sawa na kulipwa malipo ya umri mrefu kama tulivyoona hapo nyuma hata kama hatutoruzukiwa umri huo. 

 Mwenye Kuukosa Usiku Huu Amekula Khasara Kubwa: 

 Hakika mwenye kuukosa usiku huo atakuwa amenyimwa kheri zake na itakuwa ni khasara kuukosa usiku huu mtukufu kama anavyosema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):


 عَنْ أَبِي هُرَيْرَة رَضِيَ اللَّه عَنْهُ قَالَ : لَمَّا حَضَرَ رَمَضَان قَالَ رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ (( قَدْ جَاءَكُمْ شَهْرُ رَمَضَان شَهْرٌ مُبَارَكٌ اِفْتَرَضَ اللَّهُ عَلَيْكُمْ صِيَامَهُ تُفْتَح فِيهِ أَبْوَاب الْجَنَّة وَتُغْلَق فِيهِ أَبْوَابُ الْجَحِيم وَتُغَلُّ فِيهِ الشَّيَاطِين فِيهِ لَيْلَة خَيْرٌ مِنْ أَلْف شَهْر مَنْ حَرُمَ خَيْرهَا فَقَدْ حُرِمَ)) وَرَوَاهُ النَّسَائِيّ 

 Kutoka kwa Abu Huraryah (Radhiya Allaahu 'anhu) kwamba ilipofika Ramadhaan, amesema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Umekujieni mwezi wa Ramadhaan, ni mwezi wa Baraka. Imefanywa Swawm kwenu kuwa ni Fardh, milango ya Pepo hufunguliwa na milango ya moto hufungwa na mashaytwaan hufungwa. Umo katika mwezi huu usiku ulio bora kuliko miezi elfu. Atakayenyimwa kheri zake hakika kanyimwa haswa)) [An-Nasaaiy] Siku hiyo ni siku iliyoteremeshwa Qur-aan kutoka mbingu ya saba hadi mbingu ya kwanza kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu Wa Ta'ala): ﴿

 بِسْمِ اللّهِ الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ ﴾ حم - وَالْكِتَابِ الْمُبِينِ - إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةٍ مُّبَارَكَةٍ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ - فِيهَا يُفْرَقُ كُلُّ أَمْرٍ حَكِيمٍ

 KWA JINA LA ALLAAH MWINGI WA REHMA MWENYE KUREHEMU - Haa Miym - Naapa kwa Kitabu kinachobainisha - Hakika Tumekiteremsha katika usiku uliobarikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji - Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima. [Ad-Dukhaan: 1-4] Aya ya nne inayosema 'Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikma' kuwa kuna makadirio ya mwaka huo na yote yatakayotokea katika mwaka mzima. Kwa maana kwamba, siku ya Laylatul-Qadr, makadirio yote yaliyomo katika Al-Lawhum-Mahfuudhw (Ubao uliohifadhiwa) na huteremshwa haya makadirio na Malaika ambao wanaandika makadirio ya mwaka unaokuja yakiwa ni kuhusu umri wetu wa kuishi, rizki zetu, na yatakayotokea yote hadi mwisho wake.

 [Imesimuliwa na Ibn 'Umar, Mujaahid, Abu Maalik, Adh-Dhwahaak na wengineo katika Salaf – Ibn Kathiyr: 8:671] Kujikaza kufanya ibada: Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa inapoingia kumi la mwisho akijikaza kwa kufanya ibada kuliko siku zozote zingine: 

 عن عائشة – رضي الله عنها- قالت: " كان رسول الله – صلى الله عليه وسلم- يجتهد 
في العشر الأواخر، ما لا يجتهد في غيره" مسلم

 Kutoka kwa mama wa waumini bibi 'Aaishah (Radhiya Allaahu 'anha) kwamba: "Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akijitahidi katika kumi la mwisho kuliko alivyojitahidi katika siku nyingine zozote" [Muslim] Na katika Swahiyhayn (Al-Bukhaariy na Muslim): 

 عن عائشة رضي الله عنها، قالت: "كان رسول الله صلى الله عليه وسلّم إذادخل العشر شذ مئزره، وأحيا ليله، وأيقظ أهله ( وفي رواية) "أحيا الليل،وأيقظ أهله، وجدّ، وشدّ المئزر" رواه البخاري ومسلم،.

 Kutoka kwake pia mama wa waumini bibi 'Aaishah (Radhiya Allaahu 'anha): "Ilipokuwa inaingia kumi (la mwisho) Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikaza izaar (shuka) yake, akikesha usiku, na akiamsha ahli zake" (Na katika riwaaya nyingine) "Akikesha usiku, akiamsha ahli zake, akijitahidi na akikaza izaar yake" [Al-Bukhaariy na Muslim] Kwa Nini Umeitwa Laylatul-Qadr? Amesema Shaykh Ibn 'Uthaymiyn (Rahimahu-Llaah): 
 - Kwanza: Kutokana na uwezo nao ni utukufu kama vile kusema “fulani mwenye uwezo mkubwa" yaani mwenye hadhi au utukufu. 
 - Pili: Ni usiku ambao una makadirio ya mwaka mzima na huandikwa yote yatakayotokea mwaka huo, na hii ni Hikma ya Allaah (Subhaanahu Wa Ta'ala) na kuonyesha usanifu wa utengenezaji Wake na Uumbaji Wake. 
 - Tatu: Usiku huo una uwezo mkubwa kama alivyosema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((من قام ليلة القدر إيمانا واحتسابا غفر له ما تقدم من ذنبه)) متفق عليه ((Atakayesimama usiku wa Laylatul-Qadr kwa iymaan na kutaraji malipo, ataghufuriwa madhambi yake yaliyotangulia)) [Al-Bukhaariy na Muslim Sababu Ya Kupewa Waislamu Laylatul-Qadr:

 Sababu ya kupewa Ummah huu wetu wa Kiislamu siku hii tukufu ya Laylatul-Qadr ni kwamba: Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliona umri wa Ummah za mwanzo ni mrefu, na umri wa Ummah wake ni mfupi akapewa usiku wa Laylatul-Qadr uwe ni bora kuliko miezi elfu. [Muwatwtwaa 1/321 (Muhammad Fuad 'Abdul-Baaqy] Ibada Za Kufanya Masiku Kumi Haya Katika Kukesha: Qiyaamul-Layl:(Kisimamo cha usiku kuswali)

 ((من قام رمضان إيماناً واحتساباً غفر له ما تقدم من ذنبه)) متفق عليه

 ((Atakayesimama (Kuswali) Ramadhaan kwa iymaan na kutaraji malipo, ataghufuriwa madhambi yake yaliyotangulia)) [Al-Bukhaariy na Muslim] Kuosma Qur-aan: Khaswa kwa vile usiku wa Laylatul-Qadr ndio usiku ulioteremeshwa Qur-aan kama tulivyoona katika Aayah hizo za juu katika Suratul-Qadr na Suratud-Dukhaan. Vile vile Ramadhaan nzima inampasa Muislamu asome Qur-aan kwani ni mwezi ulioteremshwa Qur-aan kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala): 

 ((شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِيَ أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَى وَالْفُرْقَانِ))

 ((Mwezi wa Ramadhaan ambao imeteremshwa humo Qur-aan kuwa ni uongofu kwa watu, na hoja zilizo wazi za uongofu na upambanuzi)) [Al-Baqarah: 185] Na Jibriyl ('Alayhis-Salaam) alikuwa akimteremkia Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kila usiku wa Ramadhaan akimsomesha na kumsikiliza Qur-aan: "

كَانَ رَسُولُ اللَّهِ -صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ- أَجْوَدَ النَّاسِ وَكَانَ أَجْوَدُ مَا يَكُونُ فِي رَمَضَانَ حِينَ يَلْقَاهُ جِبْرِيلُ وَكَانَ يَلْقَاهُ فِي كُلِّ لَيْلَةٍ مِنْ رَمَضَانَ فَيُدَارِسُهُ الْقُرْآنَ" رواه البخاري

 Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa ni mbora (mwenye matendo mema) wa watu, na alikuwa mbora zaidi katika Ramadhaan kwa sababu Jibriyl alikuwa akimjia kila usiku wa Ramadhaan akimfundisha Qur-aan)) [Al-Bukhaariy] Kufanya I'tikaaf: Kutia nia kubakia msikitini kwa kufanya ibada tu humo kwani Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akifanya hivyo:

 عن عائشة – رضي الله عنها- قالت "كان النبي يعتكف في كل رمضان عشرة أيام؛ فلما كان العام الذي قبض فيه اعتكف عشرين يوماً - أخرجه البخاري

 Kutoka kwa mama wa waumini bibi 'Aaishah (Radhiya Allaahu 'anha) kwamba: Mtume (swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akifanya I'tikaaf kila Ramadhaan siku kumi, ulipofika mwaka wake wa kuaga dunia alifanya I'tikaaf siku ishirini" [Al-Bukhaariy] Kuomba Maghfirah: Kwani usipoghufuriwa madhambi yako basi ni hatari! 

 عَنْ أَنَس وَغَيْره أَنَّ النَّبِيّ صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ لَمَّا صَعِدَ الْمِنْبَر ثُمَّ قَالَ (( آمِينَ آمِينَ آمِينَ)) " قِيلَ يَا رَسُول اللَّه عَلَامَ مَا أَمَّنْت ؟ قَالَ (( أَتَانِي جِبْرِيل فَقَالَ يَا مُحَمَّد رَغِمَ أَنْف رَجُل ذُكِرْت عِنْده فَلَمْ يُصَلِّ عَلَيْك قُلْ آمِينَ فَقُلْت آمِينَ ثُمَّ قَالَ رَغِمَ أَنْف رَجُل دَخَلَ عَلَيْهِ شَهْر رَمَضَان ثُمَّ خَرَجَ فَلَمْ يُغْفَر لَهُ قُلْ آمِينَ فَقُلْت آمِينَ ثُمَّ قَالَ رَغِمَ أَنْف رَجُل أَدْرَكَ وَالِدَيْهِ أَوْ أَحَدهمَا فَلَمْ يُدْخِلَاهُ الْجَنَّة قُلْ آمِينَ فَقُلْت آمِينَ )) صحيح الترمذي و قال الشيخ الأباني حسن صحيح 

 Kutoka kwa Anas na wengineo kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipopanda juu ya minbar aliitikia ((Aamiyn, Aamiyn, Aamiyn)). Alipoulizwa kwa nini ameitikia hivyo akasema: ((Amenijia Jibriyl akasema: Ewe Muhammad, ole wake yule ambaye unapotajwa hakuswalii, hivyo sema Aamiyn. Nikasema Aamiyn. Kisha akasema: ole wake yule ambaye umeingia mwezi wa Ramadhaan kisha akatoka bila ya kughufuriwa, kwa hiyo sema Aamiyn. Nikasema Aamiyn. Kisha akasema: 

ole wake yule ambaye amewakuta wazazi wake au mmoja wa wazazi wake lakini wasimuingize Peponi. Hivyo sema Aamiyn. Nikasema Aamiyn)) [Swahiyh At-Tirmidhiy na kasema Shaykh Al-Albaaniy kuwa Hadiyth hiyo ina daraja ya Hasan Swahiyh] Du'aa Ya Kuomba Maghfirah Katika Siku Kumi Hizi Zakaatul-Fitwr Mwisho:

 عن عائشة رضي الله عنها أنها قالت يا رسول الله أرأيت إن وافقت ليلة القدر ما أدعو قال: ((تقولين: اَللَّهُمَّ إِنَّكَ عَفُوٌ تُحِبُّ الْعَفْو فَاعْفُ عَنِّي)) ابن ماجه و صححه الألباني

 Kutoka kwa mama wa waumini bibi 'Aaishah (Radhiya Allaahu 'anha) kwamba alisema "Ewe Mjumbe wa Allaah je, nitakapowafikiswha usiku wa Laylatul-Qadr niombe nini?" Akasema, ((Sema: Ewe Allaah Hakika Wewe Ndiye Mwenye Kusamehe Unapenda Kusamehe basi Nisamehe)) [Ibn Maajah na kaisahihisha Al-Albaaniy] Matamshi Yake: 

 Allaahumma Innaka 'Afuwwun Tuhibbul-'Afwa Fa'afu 'Anniy Kumkumbuka Allaah Kwa Aina Zozote Za Dhikr: Kwa Tasbiyh, Tahmiyd, Tahliyl, Takbiyr (kusema: Subhaana Allaah, Alhamdulillah, Laa Ilaaha Illa Allaah, Allaahu Akbar) Kuomba Du'aa: Kwa vile ni mwezi wa kuomba Du'aa pia kwani Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala Ameunganisha Aayah za kufaridhishwa Swawm na Aaya za kuhusu kuomba Du'aa:

 ((وَإِذَا سَأَلَكَ عِبَادِي عَنِّي فَإِنِّي قَرِيبٌ أُجِيبُ دَعْوَةَ الدَّاعِ إِذَا دَعَانِ فَلْيَسْتَجِيبُواْ لِي وَلْيُؤْمِنُواْ بِي لَعَلَّهُمْ يَرْشُدُونَ)) 

 ((Na waja Wangu watakapokuuliza khabari Zangu, waambie kuwa Mimi nipo karibu. Naitikia maombi ya mwombaji anaponiomba. Basi na waniitikie Mimi, na waniamini Mimi, ili wapate kuongoka)) [al-Baqarah: 186] Usiku Gani Khaswa Unapatikana Laylatul-Qadr?
 Hadiyth zimetaja siku kadhaa ambazo usiku huu mtukufu hutokea katika siku kumi za mwisho na haswa katika usiku wa witiri, zikiwa zimetajwa nyingine kuwa ni usiku wa siku ya ishirini na moja, au ishirni na tatu, au ishirni na tano au ishirini na saba kama ilivyokuja katika dalili zifuatazo:

 لحديث عائشة أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: ((تحروا ليلة القدر في الوتر من العشر الأواخر)) رواه البخاري 

 Hadiyth kutoka mama wa waumini bibi 'Aiashah (Radhiya Allaahu 'anha) kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Utafuteni usiku wa Laylatul-Qadr katika siku za witiri kwenye siku kumi za mwisho)) [Al-Bukhaariy] 

 وفي حديث ابن عباس رضي الله عنهما أن النبي صلى الله عليه وسلم قال: (( التمسوها في العشر الأواخر من رمضان ليلة القدر في تاسعة تبقى ، في سابعة تبقى ، في خامسة تبقى)) رواه البخاري 

 Hadiyth kutoka Ibn 'Abbaas (Radhiya Allaahu 'anhuma) kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Utafuteni usiku wa Laylatul-Qadr katika siku kumi za mwisho za Ramadhaan, katika (usiku wa) tisa, saba, na wa tano utakaobakia [mwisho wa Ramadhaan])) [al-Bukhaariy] Imaam Ahmad amerikodi kutoka kwa 'Ubaydah bin As-Swaamit kwamba alimuuliza Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu usiku wa Laylatul-Qadr akasema: 

 ((فِي رَمَضَان فَالْتَمِسُوهَا فِي الْعَشْر الْأَوَاخِر فَإِنَّهَا فِي وِتْر إِحْدَى وَعِشْرِينَ أَوْ ثَلَاث وَعِشْرِينَ أَوْ خَمْس وَعِشْرِينَ أَوْ سَبْع وَعِشْرِينَ أَوْ تِسْع وَعِشْرِينَ أَوْ فِي آخِر لَيْلَة ))

 ((Katika Ramadhaan, utafuteni siku kumi za mwisho, hakika umo katika siku za witiri, siku ya ishirini na moja, au ishirini na tatu, au ishirini na tano, au ishirini na saba, au ishirini na tisa, au usiku wa mwisho)) [Ahmad] Alama Zinazobainisha Laylatul-Qadr: Kwenye usiku huo kunakuwa na mwanga zaidi. Upepo siku hiyo hutulia, yaani siku hiyo hautokei upepo mkali. Hali ya hewa huwa nzuri. Nyoyo siku hizo huwa na utulivu na unyenyekevu zaidi kuliko siku nyingine. Baadhi ya watu wema huoteshwa usiku kama walivyokuwa wakioteshwa Maswahaba na Salafus-Swaalih (wema waliotangulia) Asubuhi Yake:

 حديث أبي بن كعب رضي الله عنه أنه قال : "أخبرنا رسول الله صلى الله عليه وسلم أنها تطلع يومئذ ٍ لا شعاع لها" رواه مسلم 

 Hadiyth kutoka kwa Ubay bin Ka'ab (Radhiya Allaahu 'anhu) kwamba: "Ametuambia Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa jua hutoka siku hiyo likiwa halina mishale (mikali)" [Muslim]

 (( ليلة القدر ليلة طلقة لا حارة ولا باردة ، تُصبح الشمس يومها حمراء ضعيفة)) صحيح ابن خزيمة 

 ((Laylatul-Qadr usiku ulio katika hali ya ukunjufu, usio na baridi wala joto, asubuhi yake jua huwa jekundu na dhaifu)) [Swahiyh Ibn Khuzaymah] 

 ليلة القدر ليلة بلجة (أي مضيئة) لا حارة ولا باردة ، لا يرمى فيها بنجم)) (أي لا ترسل فيها الشهب) رواه الطبراني ومسند أحمد 

 ((Laylatul-Qadr usiku wa kung'aa [yaani wenye mwanga] sio joto wala baridi, na vimondo (nyota za kufyatuliwa) hazitotumwa)) [At-Twabaraaniy na Ahmad] Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Atuwezeshe kukesha masiku haya kumi ili tujaaliwe kuupata usiku huu mtukufu tutoke katika Ramadhaan hii tukiwa tumeghufuriwa madhambi yetu yote na tumepewa fadhila za usiku huu mtukufu zinazolingana na kuongezewa umri wa miaka 83. Aamiyn