Monday, May 28, 2012

SHA'ABAAN - FADHILA ZAKE NA UZUSHI WA NISFU SHA'ABAAN

UZUSHI NA MAOVU MUHAMMAD BAAWAZIR

BismiLLaah WalhamduliLLaah Waswalaatu Wassalaamu ‘alaa RasuuliLLaah, wa ba'ad Mwezi wa Sha’abaan ni mwezi wa nane katika kalenda ya Kiislam. Na ni mwezi ambao upo katikati ya miezi miwili mitukufu; Rajab na Ramadhaan. Mambo ya kuzingatia katika mwezi huu ni kuweza kupambanua yaliyo sahihi na yaliyozushwa, kwani ingawa kuna fadhila zake mwezi huu lakini pia mengi yaliyoenea na yanayofanywa na watu, ni ya Upotofu.

Ni mwezi ambao Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alikuwa akifunga sana Swawm za Sunnah kama ilivyothibiti katika Hadiyth ifuatayo kutoka kwa Mama wa Waumini ‘Aaishah عنها رضي الله " كان رسول الله صلى الله عليه وآله وسلم يصوم حتى نقول لا يفطر، ويفطر حتى نقول لا يصوم، وما رأيت رسول الله استكمل صيام شهر إلا رمضان وما رأيته أكثر صياماً منه في شعبان" رواه البخاري ومسلم “Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alikuwa akifunga hadi tukadhani kuwa hatofungua kamwe, na alikuwa akiacha kufunga hadi tukadhani hatofunga tena. Sijamuona Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akifunga mwezi mzima kama alivyokuwa akifunga Ramadhaan, na sijamuona akifunga mara nyingi kama alivyofunga katika Sha’abaan” [Al-Bukhaariy na Muslim]

SWAWM NA FADHILA ZA MWEZI WA SHA'ABAAN

Juu ya kwamba Mtume الله عليه وآله وسلم صلى alikuwa akifunga mara nyingi zaidi katika mwezi wa Sha’abaan kuliko miezi mingine ukiondosha Ramadhaan, kama ambao unafungwa wote, hakuwahi hata mara moja kuufunga mwezi mzima wa Sha’abaan. Na ni jambo ambalo lenye kuchukiza kufanya hivyo kama wanavyotueleza wanachuoni kama kina Ibnul Mubaarak na wengi wengine, pia Swahaba mtukufu Ibn ‘Abbaas anasema ni makruhu kufunga mwezi mzima wa Sha’abaan kwani Mtume wa Allah hakufanya hivyo.

  Imepokewa kuwa Ibn ‘Abbaas عنهما رضي الله amesema: ‘‘Mtume wa Allaah صلى الله عليه وآله وسلم hakuwahi kufunga mwezi wowote kikamilifu isipokuwa Ramadhaan. [Al-Bukhaariy] Kukithirisha kwake Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ibada katika mwezi huu wa Sha'abaan, ni kutokana na maelezo yake mwenyewe alipoulizwa na Usaamah bin Zayd رضي الله عنه sababu ya kufunga sana katika mwezi huu alijibu: ((ذاك شهر تغفل الناس فيه عنه، بين رجب ورمضان، وهو شهر ترفع فيه الأعمال إلى رب العالمين، وأحب أن يرفع عملي وأنا صائم)) “[Sha'abaan] ni mwezi ambao watu hawautilii sana maanani, ulio kati (ya miezi miwili mitakatifu) Rajab na Ramadhaan, na ni mwezi ambao matendo yanapandishwa kwa Mola wa ulimwengu.

Nami napenda matendo yangu yapandishwe na hali nikiwa nimefunga” [An Nasaaiy, at-Targhiyb wat-Tarhiyb, uk. 425]. Hadiyth hii na Hadiyth nyengine za Mjumbe wa Allaah صلى الله عليه وآله وسلم zinahimiza kufanya amali njema pale watu wanapoghafilika na kumkumbuka Allaah na ‘Ibaadah, kama kumkumbuka Allaahسبحانه وتعالى katika sehemu za masoko, maduka na biashara zingine, ambapo watu wameshughulishwa na biashara zao na pia katika nyakati za matatizo.

  Mjumbe wa Allaah صلى الله عليه وآله وسلم amesema: “Ibaadah wakati wa matatizo (fitnah) ni kama uhamiaji (hijrah) kwangu” [Muslim] Faida na ubora wa kumuabudu Allaah سبحانه وتعالى wakati watu wameghafilika na kumkumbuka Allaah سبحانه وتعالى zimekuja kwa sababu ‘Ibaadah katika nyakati kama hizo ni ngumu zaidi kuliko kumuabudu Allaah سبحانه وتعالى wakati kila mtu amefungamana na ‘Ibaadah. Kufunga katika mwezi wa Sha'abaan ni mazoezi kabla ya Ramadhaan.

Hata hivyo, kufunga mwezi mzima wa Sha'abaan ni Makruhu (hakupendezi) na ni kinyume na Sunnah za Mjumbe wa Allaah صلى الله عليه وآله وسلم. Ibn 'Abbaas رضي الله عنهما amesema: “Msiutangulie Ramadhaan kwa (kufunga) siku moja au mbili, ila kwa wale tu wenye mazoea ya kufunga kila mara, na kwa hali hiyo hao wanaweza kufunga (siku hizo)” Al-Bukhaariy Pia imekatazwa kufunga katika mwisho wa Sha'abaan kwa nia ya kutozikosa siku za mwanzo wa Ramadhaan, isipokuwa kwa wale wenye tabia na mpangilio wa kufunga na ikawa siku za mwisho za Sha'abaan zimetokezea sambamba na siku ambazo mtu yule kawaida huwa anafunga, kama vile za Jumatatu na Alkhamiys au imemkuta akiwa anaendelea kulipa Swawm ya deni.

  Imeripotiwa katika Swahiyh Al-Bukhaariy kutoka kwa Abu Hurayrah رضي الله عنه kuwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amesema: “Kufunga katika mwisho wa Sha'abban kumekatazwa ili kuweka tofauti kati ya Swawm za Sunnah na Swawm za faradhi.” Vile vile ni kinga ya kuwakinga watu na kuanguka katika mtego wa Shetani, ambaye amewashawishi watu wa Kitabu kuongeza Swawm zaidi ya zile Allaahسبحانه وتعالى Alizowafaradhishia.

 Kwa sababu hiyo hiyo, imekatazwa pia kufunga siku ya ‘Yawmu Shakk”. Siku ya shaka ni ile siku ambayo watu hawana uhakika juu ya kuanza kwa Ramadhaan, kwa sababu ya hali ya mawingu kufunga na mwezi kutoonekana au sababu nyinginezo. Na Imaam Ibn Rajab رحمه الله amesema: ''Funga katika Sha'abaan ni bora kuliko funga katika masiku matakatifu (ambayo ni Dhul Qa'adah, Dhul Hijjah, Muharram na Rajab zilizotajwa katika Suratut Tawbah Aayah ya 36), na Swawm zilizo bora ni zile (zitambulikazo) ambazo ziko karibu na Ramadhaan, kabla au baada.

Hadhi na daraja ya Swawm hizi ni kama ya zile za Swalah za Sunnah za Rawaatib, ambazo huswaliwa kabla na baada ya Swalah za fardhi na ambazo huwa ni vijazilio vya upungufu wa zile Swalah za fardhi. Na hali kama hiyo ndiyo ile ile ya Swawm zitambulikazo ambazo huwa kabla na baada ya Ramadhaan, Kama ambavyo Swalah za Sunnah za Rawaatib zilivyo bora kuliko Swalah zingine za kujitolea (za Sunnah), na hivyo ndivyo Swawm zitambulikazo (zilizo katika miezi) ya kabla na baada ya Ramadhaan zilivyo bora kuliko Swawm nyinginezo.'' Taz. Latwaaif al Ma'arif fiyma li Mawaasim al'aam minal Wadhaaif, cha Ibn Rajab al Hanbaliy.

NISFU SHA'ABAAN: KUNA UKWELI WOWOTE?

Pamoja na ubora huo na daraja hiyo ya mwezi wa Sha'abaan, Mtume صلى الله عليه وآله وسلم hakuihusisha siku maalum katika mwezi wa Sha'abaan kufunga. Alikuwa akifunga kwa wingi iwezekanavyo lakini hakutueleza na wala hakuichagua siku ya tarehe 15 ya Sha'abaan kufunga kutokana na sifa zake alizozitaja hapo nyuma, ila tu ametaja Fadhila za usiku huu kutokana na hadiyth hii ambayo hata hivyo haikutaja kuwa kuna ibada maalum inapaswa ifanyike siku hii au usiku wake.

  عن أبي موسى الأشعري رضي الله عنه عن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: ((إن الله ليطلع في ليلة النصف من شعبان فيغفر لجميع خلقه إلا لمشرك أو مشاحن)) رواه ابن ماجة وحسنه الألباني في السلسلة الصحيحة Imetoka kwa Abu Muusa Al-Ash'ariy رضي الله عنه kwamba Mtume صلى الله عليه وآله وسلم kasema: “Allaah سبحانه وتعالى Hutokea Katika usiku wa 15 wa Sha'abaan, na Huwasamehe wote isipokuwa Washirikina na wale wenye uadui kwa wengine.” Ibn Maajah na imesemwa kuwa ni Hadiyth Hasan na Shaykh Al-Albaaniy.

Jambo la kushangaza ni kwamba wengi katika Waislam kwa uchache wa elimu na pia kwa kufuata mafundisho yasiyo sahihi ambayo amesingiziwa nayo Mtume صلى الله عليه وآله وسلم, wameitenga siku hiyo ya Nisfu Sha'abaan kufunga na kusimama kisimamo cha usiku na kusoma nyiradi mbalimbali ambazo wamezitunga na pia kusherehekea kwa namna mbalimbali. Sehemu nyingi ulimwenguni hufanya sherehe na Swawm pamoja na kuswali sana usiku kwa kuiadhimisha siku hiyo ambayo huamini ni ya aina yake.

Kuna waliyoipa jina la Shab-E-Baraat au Laylatul Bara-at (usiku wa kuachiwa huru [na moto], au wa kusamehewa) kama huko bara Hindi, Pakistan na Bangladesh. Na kwengine hujulikana zaidi kwa Nisfu Sha'abaan n.k. ambapo katika siku hiyo wanaamini kuwa ni siku ya kusamehewa kwani Allaah Anawaachia huru waja wake walio motoni kutokana na mojawapo ya Hadiyth zisizo sahihi zilizohusishwa na mwezi huu wa Sha'abaan kama hii “Mwenyeezi Mungu Anawaachia huru waja wake walio motoni kulingana na idadi ya nywele zilizo katika ngozi za mbuzi/kondoo wa Banu Kalb.”

Vilevile kuna imani potofu kabisa katika siku hii, ambapo kuna baadhi ya watu wanaamini kuwa kushuka kwa Malaika na Ruuh usiku huo kama ilivyo katika Suratul-Qadr Aayah ya 4, wao wameelewa maana yake ni kuwa Ruuh iliyokusudiwa katika sura hiyo ni roho za wale waliokufa! Na kwamba 'roho' hizo zashushwa na kurejea duniani na kukutana na wake wa wenye hizo roho na jamaa zao wengine. Na kwa sababu hiyo, wale wajane hupika vyakula bora vilivyokuwa vikipendwa na hao waume zao waliokufa kisha huviandaa na kusubiri ziara zao kutoka huko walipo.

  Baadhi ya watu pia huzuru makaburi katika siku hiyo na kuwaombea msamaha wale wote waliokufa mwezi wa Sha'abaan uliopita na huo walio nao. Katika Surah hiyo ya Al-Qadr ambayo watu hao wameifasiri na kuielewa kinyume, Allaah سبحانه وتعالى Anasema: }}تَنَزَّلُ الْمَلَائِكَةُ وَالرُّوحُ فِيهَا بِإِذْنِ رَبِّهِم مِّن كُلِّ أَمْرٍ{{ {{Huteremka (katika usiku huo wa Qadr) Malaika pamoja na Ruuh kwa idhini ya Mola wao kwa kila jambo}} Al-Qadr: 4.

Kwanza, Aayah hii huelezea Usiku wa Qadr (wa Cheo) ambao ni usiku wa mwezi wa Ramadhaan na sio wa siku au tarehe 15 ya Sha'abaan.

Pili, maana ya neno Ruuh katika Aayah hiyo ni Malaika Jibriyl, yaani watashuka Malaika pamoja na Jibriyl (pamoja na kwamba naye ni Malaika ila kutajwa kwake pekee bila kuingizwa katika kundi zima la Malaika hao, ni hadhi yake kuu) na sivyo kama wanavyodhani watu kuwa hiyo Ruuh ni roho za waliokufa (Taz. Tafsiri ya Ibn Kathiyr).

Vilevile itikadi ya kwamba roho za waliokufa zitarejea tena ulimwenguni si sahihi kutokana na mafundisho sahihi ya Qur-aan na Sunnah. Pia wengine wameuhusisha huo usiku wa katikati ya mwezi wa Sha'abaan na maneno 'Laylati-m-Mubaarakatin' (Usiku uliobarikiwa) yaliyo katika Aayah ya 3 katika Suratud-Dukhaan isemayo: }}إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةٍ مُّبَارَكَةٍ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ{{ {{Kwa yakini tumeteremsha (Qur-aan) katika usiku uliobarikiwa, bila shaka sisi ni waonyaji}} Ad-Dukhaan: 4 Wakifasiri huo usiku uliobarikiwa kuwa ni wa 15 Sha'abaan.

Lakini hiyo ni tafsiri potofu kabisa kwani inajulikana wazi bila shaka kuwa 'Laylatim Mubaarakatin' iliyokusudiwa hapo kwenye Surah hiyo ni usiku uliopo katika mwezi wa Ramadhaan. Na kama ilivyo wazi ni kwamba Qur-aan imeteremshwa katika mwezi wa Ramadhaan na si katika mwezi wa Sha'abaan na haswa hiyo tarehe 15.

Allaah سبحانه وتعالى Anathibitisha hilo katika Suratul Baqarah: }}شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِيَ أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَى وَالْفُرْقَانِ{{ {{Ni mwezi wa Ramadhaan ambao imeteremshwa (ndani ya mwezi huo) Qur-aan ili uwe uongozi kwa watu, na hoja zilizo wazi za uongozi na upambanuzi (wa baina ya haki na batili)...}} Al Baqarah: 185 Basi hayo wayasemayo baadhi ya watu kuwa usiku huo ni usiku wa kuamkia mwezi 15 Sha'abaan ambao pia wanauita 'Qismatur Rizq' (Mgao wa riziki) si maneno ya kweli, bali ni uzushi na upotofu uliozoeleka na ambao umeenezwa katika Dini hii tukufu na kuichafua na kuivuruga hadi imekuwa sasa ni vigumu sana kupambanua la batili na la haki katika Dini hii iliyokamilika na isiyo na haja ya nyongeza za waongezao.

Pia du’aa zisomwazo ndani ya usiku huo zina kila aina ya uzushi upinganao na Qur-aan, kama walivyobainisha Wanachuoni wa kutegemewa. Na hayo ya kujikusanya usiku huo na kusoma du’aa hizo na nyiradi mbalimbali ni jambo ambalo halimo katika mafunzo ya Kitabu chetu kitukufu na wala katika Sunnah Sahihi. Wanachuoni mabingwa wa fani ya Hadiyth wamebaini kuwa hakuna hata Hadiyth moja iliyo sahihi katika Hadiyth zilizozagaa ambazo zinazungumzia fadhila na utukufu wa mwezi wa Sha'abaan au haswa tarehe 15 ya Sha'abaan isipokuwa hiyo iliyotajwa juu ya kwamba

Allaah سبحانه وتعالى Hutokea usiku huo na kuwasamehe waja wake isipokuwa waliomshirikisha na wenye uadui. Na zaidi ni kuwa zote ima dhaifu au mawdhu'u (za uongo/ kutungwa). Wanachuoni mbali mbali kama Maimaam Ash-Shawkaaniy, Ibnul Jawziy, Ibnu Hibbaan, Al Qurtubiy رحمهم الله حميعا wamelaumu mno na kuzikana Hadiyth au mapokezi hayo yasiyo sahihi kuhusiana na Sha'abaan au siku hiyo ya Nisfu Sha'abaan.

 (Rejea vitabu vyao kama Al Fawaaidul Majmu'ah, Maudhu'aatul Kubraa na Tafsiyr al Qurtubiy). Katika baadhi ya Hadiyth za kutungwa ni kama zile zisemazo, “Katika siku hii (ya 15 Sha'abaan) Mwenyeezi Mungu Huwaachia huru watu kutoka katika Moto wa Jahannam idadi inayolingana na nywele zilizomo katika kondoo wa kabila la Banu Kalb.” Na Hadiyth hii Imaam At-Tirmidhiy anasema ni mbovu na dhaifu.

Na nyingine inasema: “Yeyote atakayeswali rakaa kumi na nne za Swalah katika usiku wa tarehe 15 ya Sha'abaan atapata ujira ulio sawa na kufunga Swawm na Hija ya miaka ishirini.”
na pia isemayo: “Kuwa ubora wa siku hii ni kwa sababu jaala ya mwanaadam ndiyo huwa katika siku hii, pia mipango ya mazazi na vifo hupangwa.”

Na riwaya dhaifu nyinginezo ni kama hizi:

 “Mwenyeezi Mungu tubarikie katika (mwezi wa) Rajab na Sha'abaan na tufikishie Ramadhaan.” • “Ubora wa mwezi wa Sha'abaan (kulinganisha na miezi mingine) ni sawa na ubora wangu kuliko Mitume wengine.”
• “Ukifika (Ukiwa) usiku wa Sha'abaan basi mswali usiku wake na mfunge mchana wake.” • “Masiku matano huwa du'aa hazirejeshwi; Usiku wa mwanzo wa Rajab, na Usiku wa Nisfu Sha'abaan, na Usiku wa Ijumaa, na Usiku wa ('Iyd) Al-Fitwr, na Usiku wa ('Iyd) ya Kuchinja.”
• “Amenijia Jibriyl ('Alayhis Salaam) na akaniambia kuwa huu Usiku wa Nisfu Sha'abaan Mwenyeezi Mungu Huwatoa kwenye Moto watu kwa idadi ya kila unyoya wa mbuzi/kondoo wa Banu Kalb.”
• “Ee 'Aliy, atakayeswali katika Usiku wa katikati ya Sha'abaan Swalah ya rakaa mia kwa kusoma Qul Huwa Allahu Ahad mara elfu moja, Mwenyeezi Mungu Atamkidhia mahitaji yake yote ya Usiku huo.”
• “Atakayesoma katika Usiku wa Nisfu Sha'abaan Qul Huwa Allahu Ahad mara elfu moja Mwenyeezi Mungu Atamtumia Malaika elfu moja watakaomjia kumpa bishara njema.”
• “Atakayeswali katika Usiku wa Nisfu Sha'abaan rakaa mia tatu akasoma katika kila rakaa Qul Huwa Allahu Ahad mara thelathini, basi atakuwa miongoni mwa kundi litakalopewa shafa’ah ikiwa ni katika watu waliostahiki Moto.”
• “Sha'abaan ni mwezi wangu.”
• “Atakayehuisha Usiku wa 'Iyd na Usiku wa Nisfu Sha'abaan hautokufa moyo wake siku zitakapokufa nyoyo.”
  • “Atakayehuisha Masiku matano, atapata pepo; Usiku wa Tarwiyah (katika Hajj), na Usiku wa 'Arafah, na Usiku wa siku ya kuchinja, na Usiku wa 'Iyd Al-Fitwr, na Usiku wa Nisfu Sha'abaan.” Hadiyth zote hizo hapo juu kwa matamshi hayo, hazina uthibitisho wowote wa usahihi wake kisheria. Kwa hiyo hakuna Hadiyth hata moja sahihi yenye kuthibitisha kuitenga au kuihusisha siku ya tarehe 15 ya Sha'abaan kufanya ‘Ibaadah maalum kama kufunga au kuswali Swalah za usiku (Qiyaamul Layl). Na kufanya hivyo ni uzushi na upotofu ambao unapingana na mafundisho ya kipenzi chetu Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم.

Ama kwa yule aliyezoea kuswali Swalah za Usiku kila mara basi haikatazwi kwake kuswali vilevile usiku huo, kisichofaa ni mtu ambaye hana ada ya kuswali Swalah za usiku lakini usiku huo akawa haukosi kwa kuamini kuwa una fadhila kubwa. Pia tunapata mafundisho kuwa kutenga siku maalum kwa ibada maalum ni jambo linalokwenda kinyume na sheria, isipokuwa lile lililotajwa au kufundishwa na Mtume صلى الله عليه وآله وسلم kama kufunga siku ya 'Ashuraa na siku ya ‘Arafah kwa asiye katika Hija ambazo ametubainishia sababu zake.

Lau kama hili la kufunga Nisfu Sha'abaan lingekuwa lina umuhimu na faida kwetu basi angetueleza na angelifanya yeye mwenyewe katika uhai wake. Na kama kuna siku bora katika wiki basi ni Ijumaa na ambayo imependekezwa kwetu kufanya matendo mazuri na pamoja na ubora wake huu Mtume صلى الله عليه وآله وسلم hakutuamrisha tufunge siku hiyo wala kuusimamisha usiku wake kwa Swalah.

 Na kama ingekuwa inaruhusiwa kama wafanyavyo hao wenye kutenga siku maalum kwa ‘Ibaadah na kuacha masiku yote yaliyobaki ya mwaka mzima, basi ingekuwa ni awlaa kwa Mtume wa Mwenyeezi Mungu صلى الله عليه وآله وسلم kutusisitiza tulifanye hilo katika siku ya Ijumaa kutokana na ubora wake. Lakini Mtume صلى الله عليه وآله وسلم hakufanya hivyo.

Mwenyewe Mtume صلى الله عليه وآله وسلم anasema: “Msitenge Usiku (wa kuamkia) Ijumaa kuutenga na usiku mwengine (wowote) kwa kuswali, na msitenge siku ya Ijumaa miongoni mwa masiku kwa kufunga, ila yule aliyezoea kufunga na funga yake ikaangukia siku hii [Ijumaa].” Muslim Na hili latuthibitishia wazi kuwa ‘Ibaadah na matendo yote mazuri hayafanywi katika siku fulani au usiku maalum tu na kuachwa nyingine, maana kufanya hivyo hakutatimiza wajibu wa Mja wa kumuabudu Mola wake.

Mja hupaswa kumuabudu Mola wake siku zote za umri wa maisha yake yote hadi atakapoiaga dunia, kwani ‘Ibaadah ni kusudio la msingi la kuumbwa kwake. Anasema Allaah سبحانه وتعالى: }}وَاعْبُدْ رَبَّكَ حَتَّى يَأْتِيَكَ الْيَقِينُ{{ {{Na umuabudu Mola wako hadi ikufikie hiyo yakini (Nayo ni mauti)}} Al-Hijr: 99. Na ndivyo ilivyokuwa ada ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم kumuabudu Mwenyeezi Mungu muda wote wa mwaka mzima, masiku yote, usiku na mchana alitumia katika kumtumikia Allaah وتعالى سبحانه.


UKUMBUSHO KATIKA SHA'ABAAN

Iwapo bado unahitajika kulipa Swawm za faradhi za Ramadhaan iliyopita, fanya haraka kulipa kabla ya Ramadhaan nyingine haijafika. Hairuhusiwi kuchelewesha Swawm zilizokosekana mpaka kufikia Ramadhaan inayofuata, isipokuwa katika hali ya ulazima (mfano udhuru unaokubalika ambao umeendelea baina ya Ramadhaan mbili). Mama wa Waumini 'Aaishah عنها رضي الله amesema,

“Ilikuwa nnazo siku za kulipa za Ramadhaan na sikuweza kuzilipa isipokuwa (katika mwezi wa) Sha'abaan.” Al-Bukhaariy Yeyote aliyekuwa na uwezo wa kulipa Swawm zilizompita/ zilizomfutu kabla ya Ramadhaan (ya pili) na asifanye hivyo, basi atalazimika kuzilipa baada ya Ramadhaan (ya pili), na zaidi analazimika kutubia na kumlisha maskini mmoja kwa kila siku iliyompita/ iliyomfutu. [Huu ni msimamo wa Maimam Maalik, Ash-Shafi’iy na Ahmad] na unaoonekana kuwa sahihi zaidi. Wa Allaahu A’alam

Wednesday, May 23, 2012

NEW PAGE OPENED

Assalam alaykum warahmatul lahi wabarakatu. Amma baada ya kumshukuru Mwenyezimungu na kumtakia Rehma na Amani Mtume wake napenda kuchukua nafasi hii kwa kuwaarifu kuwa kuna page mpya nimeifungua baada ya kusikiliza ushauri wa wadau mbalimbali juu ya uwekaji wa vitabu vya dini na kisekyula katika blog yetu. Jina la hiyo page imeandikwa BOOKSTORE iko shortcut yake upande wa kulia mwa Blog yetu na pia kwa mafunzo ya swala bonyeza kitufe kilichoandikwa HOW TO PRAY, na pia kwa masuala ya kusoma kwa wasomi kuna kitufe na picha isomekayo STUDY GUIDE AND STRATERGY kuna nakala mbalimbali ndani yake namna bora ya kusoma na kufanikiwa vizuri katika masomo yetu pia. Tunajitahidi kuweka vitu ambavyo vinahitajika kwa wakati uliopo na kama unaushauri wowote juu ya uboreshaji wa Blog yetu tunaomba mchango wako wa mawazo tuu kwa sasa na sio gharama yoyote.Kama ni mwalimu tunapokea vitabu au Notsi zozote za kufundishia katika softcopy ili wadau wengine wa mashuleni wafaidike nazo pia na kama wewe ni blogger mzuri zaidi basi pia tupe ushauri wako kuboresha blog yetu kwa ujumla. Tunapokea ushauri kwa njia ya email yetu assmohamm@gmail.com au kwa jnia ya kucomment katika habari yoyote nasi tutaiona pia. Maas salam

Thursday, May 17, 2012

WHAT DOES IT MEAN TO BE A MUSLIM TODAY?


Assalam Alaykum brothers and sisters in Imaan.

To be a Muslim today--or any day--is to live in accordance with the will and pleasure of Allah. Muslims often say, with joy and pride, that it is easy to be a Muslim since Islam is "the straight path" leading to paradise. What this means, in other words, is that the principles of Islam are simple and straightforward, free of ambiguities, confusions, inconsistencies or mysteries, and that comprehending them or living in accordance with them is not difficult. The assumption here is that if one somehow comes to "the straight path" by accepting Islam, which is Allah's last and final revelation to humanity, one will fairly effortlessly arrive at the destination which is a state of eternal blessedness in the presence of Allah. I must confess that I am totally amazed, and overwhelmed, by this assumption. To me, being a Muslim today--or any day--seems to be exceedingly hard, for to be a Muslim one has constantly to face the challenge, first of knowing what Allah wills or desires not only for humanity in general but also for oneself in particular, and then of doing what one believes to be Allah's will and pleasure each moment of one's life.
Probably you may be asking yourself why this article. Well, I thought I should raise this issue as per our culture of reminding each other, raising awareness and bring positive vision about Islam. This presentation is of personal perception and understanding of Islam and should not be taken as of Muslims in general or the other way round.
Okay, let’s go straight to the topic. I think to be a Muslim first and foremost, to believe in Allah, who is "Rabb al-'alamin": creator and sustainer of all peoples and universes. Integrated vision of the Qur’an does not separate belief in Allah and Allah's revelation ("iman") from righteous action ("'amal"), or regular remembrance of Allah ("salat") from regular discharge of one's financial and moral obligations to Allah's creatures ("zakat"). Thus, to be a Muslim means--in a fundamental way--to be both Allah-conscious and creature-conscious, and to understand the interconnectedness of all aspects of one's life, of the life of all creation and of our life in this transient world to life eternal.
In one hadith, prophets wife, Aisha (r.a) was asked about the prophet’s behaviour, she replied it was a Qur’an. The Prophet of Islam attained the highest degree of "'ubudiyat" (service of Allah) and became a model of righteous living not only as the spiritual and political leader of the Muslim "ummah", but also as a businessman, citizen, husband, father, friend, and a human being in general, and this is to say that that being a Muslim means more than seeking or worshiping Allah.
Being a Muslim is dependent essentially only upon one belief: belief in Allah, universal creator and sustainer who sends revelation for the guidance of humanity. Believing in Allah and Allah's revelation to and through the Prophet Muhammad, preserved in the Qur'an, is, however, not identical with accepting the "Shari'ah" as binding upon oneself.

IT IS A PERSONAL COMMITMENT.
To me being a Muslim today means taking a stand against those who insist that being a Muslim means following the trodden path and sanctifying tradition without subjecting it to serious reflection or critical observation. According to the holy Qur'an, Adam was elevated even above the celestial creatures on account of his capability to "name" things, i.e., to form concepts or to exercise the rational faculty (Surah 2: Al-Baqarah: 30-34) in one of the most significant passages of the Qur'an( Surah 33: Al-Ahzab: 72) we are told that Allah offered the "trust" of freedom of will to all creation but only humanity accepted it. What this says to me is that it is not only a right of Muslims, but also their duty--and indeed their glory--to think and to choose.
Being a Muslim today means not turning away in hatred or anger from those who regard Muslims as adversaries but engaging in dialogue with them in a spirit of amity and goodwill.31 Being a Muslim today means paying serious heed to the Qur'anic teaching that Allah, universal creator and sustainer, who cares for all and sends guidance to all, has decreed diversity for a reason, as the following passage tells us: "O men! Behold! We have created you out of a male and a female, and have made you into nations and tribes, so that you might come to know one another. Verily the noblest of you in the sight of God is the one who is most deeply conscious of Him. Behold, God is all-knowing, all-aware."1 What this passage says to me is that we should be mindful both of our unity and our diversity, that one of the basic purposes of diversity is to encourage diverse groups and persons to know one another, that a person's ultimate worth is determined not by what group he or she belongs to but how Allah-conscious he or she is.

Being a Muslim today means taking serious note of the Qur’an imperative, "Let there be no compulsion in religion, (Surah 2: AI-Baqarah: 256), knowing that the right to exercise free choice in matters of belief is unambiguously endorsed by the Qur'an, which says: "The Truth is/From your Lord:/ Let him who will/Believe, and let him/Who will, reject it." (Surah18:AI-Kahf: 29). Being a Muslim today also means realizing that by merely professing Islam we do not attain to Paradise, and that Muslims have no special claim upon Allah's grace, for the Qur'an tells us:

Those who believe (in the Qur'an)
And those who follow the Jewish (scriptures),
And the Christians and the Sabians,
Any who believe in God
And the Last Day,
And work righteousness,
Shall have their reward
With the Lord; on them
Shall be no fear, nor shall they grieve2

Finally, to me being a Muslim today--and always--means being on a journey, both external and internal, toward attaining a state of peace which is the goal of Islam. However, peace is not merely the absence of conflict, even as health is not merely the absence of sickness. YES, that’s it. According to the perspective of the Qur'an, peace is a positive state of safety or security in which one is free from anxiety and fear. It comes into being when human beings honoring the divine imperative to live justly, learn to be just to themselves and to others. Constant striving is required to overcome the fragmentation to which most human beings are subjected in the technological age and also to eliminate sexism, racism, classism, and all forms of totalitarianism which lead to the injustices and inequities which characterize the world in which we live. To engage in such striving (which the Qur'an calls 'jihad fi sabil Allah": striving in the cause of Allah) is the purpose of a Muslim's life.
                 
1 This passage (Surah 49: AI-Hujurat: 13) is taken from The Meaning of the Qur'an, translated by Muhammad Asad (Dar AI-Andalus, Gibraltar, 1980) p.793.
2 The Holy Qur'an, pp.33-34 (Surah 2: AI-Baqarah: 62) and The Holy Quran p.265 (Surah 5: AI-Ma'idah: 69).
              source used: MUHIMBILI UNIVERSITY sunshine articles

Wednesday, May 02, 2012

MSAMU PLAN FOR 2012 - 2013

                                          OPEN DOCUMENT TO MSAMU COMMUNITY.
                                                                      BACKGROUND

MSAMU is a short form for Muslim students association of Muhimbili University.
  It was established in 2007 before which used to exist as a branch of Muslim student’s association of university of Dar es salaam, MSAUD.
As an organization it has members, constitution, and the office.
  Members include all students currently enrolled in Muhimbili University.  Leaders are elected annually from among the members. The patron is Prof. Kareem Manji who is also currently a dean of school of medicine, MUHAS.
Our office is used as library located at the Muhimbili mosque (Masjid Rrahman), where it is open twenty four hours every day for reading and some meeting purposes.

                                                                       OUR VISION:

   MSAMU is a strong, self-dependent association with its own assets and capable of providing health related services to the Islamic society of Tanzania in the light of Qur’an and Sunnah.

                                                                     OUR MISSION:

  To be an association that helps Muslim students of Muhimbili University fulfilling their dual roles at the university, being for both students and a Muslim’s who can attain the good pleasure of Allah (SWT) in order to gain salvation in this life and the Hereafter.

 This is an open document to each and every member of the society that highlights where are we going as MSAMU, objectives and future plans. Aim is to create awareness and inviting opinions and suggestions so that we can work together and efficiently as a team to reach our fundamental goals and objectives.

                                                                     CHALLENGES:

- Development of any society depends on youths and scholars. MSAMU as one of the youth’s association of scholars is responsible for his Islamic society. For many years Muslims have remain behind and unable to full utilize their potentials as scholars which has led us to a poor non promising society. It is a time to wake up and start thinking about our community and serve it, everybody in his/her position is responsible.

  Taking this into account, we plan some ideas that can initiate changes and improvements to successful achieve and bring about developments of Muslims in University and society as the whole.
 We suggest that MSAMU should find an immovable permanent asset of its own so that it becomes a self-dependent and stable association. Our future plan is to have pieces of land that can be used for health related services to the society like building hospitals, research institutes or schools of health related sciences.

  To start with, our aim is having at least piece of land of ten (10) acres by the end of March 2013. To accomplish this, MSAMU has appointed some members making a group of eight people who will volunteer in finding the places where we can buy lands, and so far they have managed to identify four areas, Mlandizi, Chanika, Mkuranga and Bagamoyo. In these areas acres of land costs between three and four hundred thousand shillings.

We believe that, the above plan can be achieved in the following means:
1) By members giving out their ideas, opinions and support through taking active self-involvement and full participation in the program. Each member should take responsibility in accomplishing our own development in Islamic community.
2) Increasing percentage of people paying MSAMU annual fees from the current 38% to about 65% beginning in the next academic year 2012/2013. 30% of these fees may be used for the mentioned developmental strategies, while the rest is being used for running other routine activities of the association.
3) To find means of increasing our income, one of our plan is opening a full equipped stationery that will be working to serve the association.
4) To introduce production of T-shirts with MSAMU logo that will be sold to the members at reasonable price to boost our income generation starting from the coming MSAMU day event.
5) Involving different stakeholders in our society including former members of the association, Muslims of different positions in a Muhimbili University and Hospital Community and other individuals in our society and Islamic Organizations to actively participate in socio-economic development of MSAMU.

We are looking forward to receive your opinions and contributions. Please for any suggestions, contribution or clarification you can contact;
1. YAAQUB ABDALLAH                 +255 717 056 503
2. BAKARI MSONGAMWANJA      +255 717 963 033
3. SHAABAN  B. SEIF                          + 255 778 340 066/ + 255 653 400 662
4. HUSEIN   THABIT                          + 255 777 347 871
5. NASEEB SHEMNDOLWA              + 255 718 520 048/+ 255 754 624 757

Alternatively you can post it through a suggestion box in the MSAMU library, facebook group MSAMU MUHIMBILI HOSPITAL or through email address msamu2012@hotmail.co.uk  or comment in our blog msamu2000.blogspot.com
Prepared by:
1. SHAABAN   BAKAR  SEIF
2. ABDALLA    NASOUR ABDALLA
3. ABBAS         AYOUB    KATAMBI   
4. HUSSEIN     THABIT    RASHID
5. MASUMBUKO MBWANA   KIMICHA
6. AMINI    MBARAQ   LINGONGO
7. MAJID   ADAM    MPANGODI
8. KALANJE ABDUL-RAHMAN MOHAMMED

Thursday, April 19, 2012

THE QURAN ON SEAS AND RIVERS:

Modern Science has discovered that in the places where two different seas meet, there is a barrier between them. This barrier divides the two seas so that each sea has its own temperature, salinity, and density.1 For example, Mediterranean sea water is warm, saline, and less dense, compared to Atlantic ocean water. When Mediterranean sea water enters the Atlantic over the Gibraltar sill, it moves several hundred kilometers into the Atlantic at a depth of about 1000 meters with its own warm, saline, and less dense characteristics. The Mediterranean water stabilizes at this depth2 (see figure 13). Figure 13:

Figure 13 (Large)


The Mediterranean sea water as it enters the Atlantic over the Gibraltar sill with its own warm, saline, and less dense characteristics, because of the barrier that distinguishes between them. Temperatures are in degrees Celsius (C°). (Marine Geology, Kuenen, p. 43, with a slight enhancement.) (Click on the image to enlarge it.) Although there are large waves, strong currents, and tides in these seas, they do not mix or transgress this barrier.

The Holy Quran mentioned that there is a barrier between two seas that meet and that they do not transgress. God has said:

                         He has set free the two seas meeting together. There is a barrier between them.   
                          They do not transgress. (Quran, 55:19-20)

But when the Quran speaks about the divider between fresh and salt water, it mentions the existence of “a forbidding partition” with the barrier. God has said in the Quran:

                         He is the one who has set free the two kinds of water, one sweet and palatable, and
                         the other salty and bitter. And He has made between them a barrier and a
                        forbidding partition. (Quran, 25:53)

One may ask, why did the Quran mention the partition when speaking about the divider between fresh and salt water, but did not mention it when speaking about the divider between the two seas? Modern science has discovered that in estuaries, where fresh (sweet) and salt water meet, the situation is somewhat different from what is found in places where two seas meet. It has been discovered that what distinguishes fresh water from salt water in estuaries is a “pycnocline zone with a marked density discontinuity separating the two layers.”3 This partition (zone of separation) has a different salinity from the fresh water and from the salt water4 (see figure 14). Figure 14:


Figure 14 (Large)

Longitudinal section showing salinity (parts per thousand ‰) in an estuary. We can see here the partition (zone of separation) between the fresh and the salt water. (Introductory Oceanography, Thurman, p. 301, with a slight enhancement.) (Click on the image to enlarge it.) This information has been discovered only recently, using advanced equipment to measure temperature, salinity, density, oxygen dissolubility, etc. The human eye cannot see the difference between the two seas that meets, rather the two seas appear to us as one homogeneous sea. Likewise, the human eye cannot see the division of water in estuaries into the three kinds: fresh water, salt water, and the partition (zone of separation).

REFERENCES:
(1) Principles of Oceanography, Davis, pp. 92-93.
(2) Principles of Oceanography, Davis, p. 93.
(3) Oceanography, Gross, p. 242. Also see Introductory Oceanography, Thurman, pp. 300-301.
(4) Oceanography, Gross, p. 244, and Introductory Oceanography, Thurman, pp. 300-301.

Tuesday, April 10, 2012

RE-APPLICATION PROCEDURE INTO HIGHER EDUCATION INSTITUTIONS IN ACADEMIC YEAR 2012/2013

The Tanzania Commission for Universities (TCU) hereby informs applicants who applied in the academic year 2011/2012 through the Central Admission System (CAS) but did not report to their selected institutions for various reasons and wish to re-apply in this academic year 2012/2013 that they will not be able to re-apply unless one writes to TCU and indicate the following:
1. The name of the institution and the programme you were selected;
2. Reasons for failing to report to the institution you were selected;
3. Index numbers and years of completion of both ‘O’ level and ‘A’ level secondary education.
4. Your preparedness to deal with the challenge(s) which made you fail to report to the institution where you were selected.

NB: Note that only applicants who will submit their letters requesting for re-application will be allowed to re-apply.

All letters should be submitted to TCU before 30th March 2012 and be addressed to:
Executive Secretary
Tanzania Commission for Universities
P. O. Box 6562
DAR ES SALAAM.
For more information contact TCU through:
Tel No.: (255) (22) 2772657
Fax: (255) (22) 2772891
Email: es@tcu.go.tz
Website: www.tcu.go.tz
Issued by
TCU Executive Secretary

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UENDESHWAJI WA UDAHILI - ELIMU YA JUU KWA MWAKA WA MASOMO 2012/2013

UTANGULIZI
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (‘Tanzania Commission for Universities’-TCU) ikishirikiana na Baraza laTaifa la Elimu ya Ufundi (‘National Council for Technical Education’ - NACTE) pamoja na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi Elimu ya Juu (Higher Education Students Loans Board) inapenda kuutarifu umma kuhusu utaratibu wa kujiunga na vyuo vya elimu ya juu kwa mwaka wa masomo 2012/2013 kupitia mifumo ya “Pre-entry”, “Mature Age Entry”, “Equivalent Qualifications” na mfumo wa pamoja wa udahili (‘Central Admission System’) na utaratibu wa mikopo kama ifuatavyo:

MFUMO WA UDAHILI KUANZIA MWAKA 2012/13

1.1 Utaratibu wa Kuendesha Program za “Pre-entry” na “Mature Age Entry”
Kuanzia mwaka huu 2012, vyuo vyote vitakavyotaka kuendesha mafunzo ya awali kabla ya mwombaji kustahili kudahiliwa ili kuweza kujiunga na programu za elimu ya juu (pre-entry programmes) pamoja na kuendesha mitihani ya kupitia mfumo wa “Mature Age Entry” vinatakiwa kuwasilisha programu hizo Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) au Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) kwa uhakiki na kupata kibali. Programu hizo ni lazima ziendeshwe kwa muda wa mwaka mmoja. Hali kadhalika kwa upande wa mitihani kupitia mfumo wa mature entry, Tume kwa ushirikiano na Baraza, kwa pamoja wataandaa na kuratibu utaratibu wa mitihani katika vituo maalum kikanda ili vyeti vitakavyotolewa viwe na ulinganifu unaostahili na hatimaye kuweza kutumika katika udahili wa sifa linganishi katika vyuo mbalimbali.
Vyuo vinatakiwa kuandaa programu za mifumo ya “Pre-entry” na “Mature Age Entry” na kuziwasilisha Tume na Baraza ili zihakikiwe kwani mwaka wa masomo kwa kusudi hili utaanza mwezi Agosti 2012/2013. Kwa utaratibu huu, watakaofanya mafunzo hayo watatakiwa kufanya mitihani yao na kujiunga na masomo ya elimu ya juu katika mwaka wa masomo 2013/2014.
Kwa taarifa hii, mwaka 2012/13 hakutakuwapo na udahili wa wanafunzi kwa mfumo wa “Pre-Entry” na “Mature Age Entry”.

1.2 Utaratibu wa Udahili Kupitia Mfumo wa Pamoja (Central Admission System)
Waombaji watakaopitia mfumo wa pamoja wa udahili (CAS) wamegawanyika katika makundi manne, ambapo waombaji wa kundi (i), (ii) na (iii) watatambuliwa kama “Direct Applicants” na kundi (iv) watatambuliwa kama “Indirect Applicants”

(i) Waliohitimu elimu ya sekondari kidato cha sita katika kipindi cha miaka miwili iliyopita pamoja na wale watakaohitimu mwaka huu.
(ii) Waliohitimu mafunzo ya diploma ya elimu ya ufundi (NTA level 6) kutoka vyuo vinavyotambulika na NACTE miaka miwili iliyopitapamoja na wale watakaohitimu mwaka huu;
(iii) Waliohitimu mafunzo ya Diploma ya Ualimu (kutoka vyuo vinavyotambulika) katika kipindi cha miaka miwili iliyopita pamoja na wale watakaohitimu mwaka huu.
(iv) Waombaji ambao sio wa moja kwa moja (Indirect Applicants) ni wote waliohitimu kidato cha sita, Diploma ya Elimu ya Ufundi(NTA level 6) na Diploma ya Ualimu katika kipindi cha zaidi ya miaka miwili iliyopita (kuanzia 2009 kurudi nyuma).

1.2 Waombaji Watakaowasilisha Maombi yao Moja kwa Moja Vyuoni
Waombaji watakaowasilisha maombi kupitia vyuo husika ni wenye sifa linganishi (Equivalent Qualifications) yaani wenye vyeti vya Astashahada na Diploma ambazo hazitambuliwi moja kwa moja na NACTE. Ili kukamilisha udahili, wanashauriwa kuwasiliana na NACTE ili vyeti vyao vitambuliwe na kusajiliwa kabla udahili haujaanza.
Vyuo vinavyofundisha programu mbalimbali katika ngazi ya Astashahada na Diploma ambavyo havina usajili wa NACTE/NECTA vinatakiwa kuwasilisha matokeo ya wanafunzi wao NACTE haraka iwezekanavyo ili matokeo hayo yaweze kutumika katika utambuzi wa vyeti vya wanafunzi husika.

2. MUDA WA UDAHILI KWA MAKUNDI MBALIMBALI
Muda wa maombi wa kuwasilisha maombi ya udahili kwenye CAS umegawanyika katika makundi matatu kama ifuatavyo:

(i) Kundi la Kwanza – (1 Aprili mpaka 30 Aprili 2012)
Waombaji wote waliomaliza kidato cha sita, Diploma ya Elimu ya Ufundi (NTA level 6), na Diploma ya Ualimu kuanzia mwaka 2011 kurudi nyuma wataanza kuomba udahili kuanzia Aprili 1, 2012 hadi 30 Aprili 2012.

(ii) Kundi la Pili
Waombaji wote watakaomaliza kidato cha sita, Diploma ya Elimu ya Ufundi na Diploma ya Ualimu mwaka 2012 wataanza kuomba udahili baada ya matokeo yao ya mitihani kutangazwa na vyombo husika. Hakuna mwanafunzi atakayesajiliwa kwa kutumia matokeo ya muda (provisional or expected results).

(iii) Kundi la Tatu
Waombaji wote ambao ni raia wa Tanzania waliosoma nje ya nchi au wenye vyeti ambavyo si vya mfumo wa elimu ya Tanzania (mfano:Cambridge, Bacclaureate, n.k). Waombaji wa kundi hili wanashauriwa kuomba udahili mara matokeo yao yatakapotangazwa na watatakiwa kupeleka vyeti vyao Baraza la Taifa la Mitihani (“National Examinations Council of Tanzania – NECTA”) au Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (National Council for Technical Education - NACTE) kwa ajili ya kulinganisha alama zao za matokeo au kupata ithibati kabla ya kuanza kuomba udahili. Hakuna wanafunzi watakaodahiliwa kwa matokeo ya muda.

3. UTARATIBU WA MIKOPO
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu kwa mamlaka iliyopewa kisheria itatoa mwongozo na utaratibu wa utoaji wa mikopo mwezi Februari 2012. Miongozo hii itachapishwa katika vyombo vya habari na kusambazwa kwenye vyuo vyote vya elimu ya juu nchini na Ofisi za Posta na kwa Wakuu wa Elimu kila wilaya. Maombi ya mikopo kwa mwaka wa masomo 2011/2012 yataanza kupokelewa ifikapo mwezi Machi 2012na mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 30 Juni 2012. Utaratibu huu utahusu waombaji wote wapya na wale walioko masomoni katika vyuo vya elimu ya juu.

4. HITIMISHO
Tunapenda kuwajulisha waombaji wote kuzingatia muda wao wa udahili kama ulivyoainishwa katika tangazo hili. Muda ukiisha hawataweza kuomba hadi mwaka wa masomo 2013/2014. Pia waombaji wote wanashauriwa kufuata taratibu za mikopo kam zitakazotolewa na Bodi ya Mikopo ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza katika swala hili
Maelezo zaidi na ufafanuzi kuhusu udahili na mikopo wa 2012/13 yanapatikana katika tovuti zifuatazo:

Tume ya Vyuo Vikuu; www.tcu.go.tz
Baraza la taifa la elimu ya ufundi; www.nacte.go.tz
Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Elimu ya Juu; www.heslb.go.tz

IMETOLEWA NA OFISI YA: Katibu Mtendaji, Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania, S.L.B 6562, Dar es Salaam. Barua pepe (e-mail)es@tcu.go.tz

Thursday, March 01, 2012

MUONGOZO KWA WAHITIMU KIDATO CHA NNE.

Wala msilegee, wala msihuzunike, kwani nyinyi ndio wa juu mkiwa ni Waumini quran(3:139).

Huzuni ikipitiliza humpelekea mtu kukata tamaa na kutoona thamani ya maisha na hata kufikia hatua ya kunywa sumu au kujiua wakati furaha ikizidi humfanya mtu akasahau majukumu mengine mazito yaliyo mbele yake.

Matokeo ya kidato cha nne yaliyotangazwa hivi karibuni yamewaacha wanafunzi na wazazi wengi kwenye majonzi huku wachache wakiwa na furaha. Hii ni kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi waliomaliza kutofanya vizuri katika mitihani yao.

Katika matokeo hayo, kati ya watahiniwa 426,314 waliofanya mtihani huo Oktoba mwaka jana, ni wahitimu 33,577 sawa na asilimia 9.98 waliopata daraja la kwanza hadi la tatu. Wahitimu 146,639 sawa na asilimia 43.60 walipata daraja la nne na 156,089 sawa na asilimia 46.41 walifeli kabisa kwa kuambulia daraja la sifuri.

Vyovyote iwavyo, matokeo haya si ya kujivunia kwani yanatoa fursa finyu kwa vijana wetu kuweza kujiendeleza.

Pamoja na hilo, kubwa ni kuangalia namna bora ya kusonga mbele kwa wale ambao hawakufanya vema wakijipanga upya kuangalia ni yepi ya kufanya ili kuweza kusonga mbele baada ya jitihada zao zilizotangulia kutofanikiwa wakati wale waliofaulu vizuri wakiweka mipango na mikakati madhubuti itakayowawezesha kuendelea zaidi.

Jambo la kwanza analopaswa kulitambua mwanafunzi ni kukubali matokeo aliyoyapata. Kuukana ukweli huu hakutakuwa na msaada kwake. Ni wazi zinaweza kuwapo kasoro za hapa na pale katika masuala ya usahihishaji lakini mchango wake katika matokeo ya jumla unaweza usiwe mkubwa sana. Hata hivyo, endapo itathibitika kuwa kuna hujuma za makusudi dhidi ya wanafunzi au shule fulani zilizopelekea wanafunzi kufeli au kufutiwa matokeo, ni vema suala hilo likafuatiliwa kwa kina na taasisi husika ili haki itendeke.

Kwa muhtasari, matokeo ya kidato cha nne unaweza kuyagawa katika makundi ya daraja la kwanza, daraja la pili, daraja la tatu, daraja la nne na daraja sifuri. Aidha unaweza kuyagawa katika makundi manne - walio na sifa za kuendelea na kidato cha tano na vyuo vya ufundi; walio na sifa za kujiunga na vyuo vya ualimu lakini hawana sifa za kuendelea na kidato cha tano na vyuo vya ufundi; walio na sifa za kujiunga na vyuo vingine; na waliofeli kabisa ambao wanakosa sifa za kuendelea na masomo ya kidato cha tano na vyuo kwa vigezo vya ufaulu wa kidato cha nne.


KUJIUNGA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA UFUNDI

Awali ya yote ifahamike kuwa wanafunzi wanaochaguliwa moja kwa moja kujiunga na kidato cha tano au vyuo vya serikali ni wale wanaotoka shuleni (school candidates).

Kadhalika wanafunzi wanaochaguliwa moja kwa moja katika vyuo vya ufundi mfano Dar es Salaam Institute of Technology (DIT), Mbeya Institute of Science and Technology (MIST), Arusha Technical College na kama hivyo, huwa na sifa sawa na wale wanaochaguliwa kuijunga na kidato cha tano katika michepuo ya sayansi. Idadi ya wanafunzi hawa huwa si kubwa sana.

Mwanafunzi aliyefaulu kwa daraja la kwanza au la pili ana nafasi kubwa ya kuchaguliwa kuendelea na masomo ya kidato cha tano au chuo cha ufundi katika shule na vyuo vya serikali. Aidha hata baadhi ya wahitimu waliopata daraja la tatu wana nafasi nzuri ya kuchaguliwa. Si tukio la kawaida mwanafunzi aliyepata daraja la nne kuchaguliwa kujiunga kidato cha tano au chuo cha ufundi.

Mara nyingi changamoto wanayokuwa nayo wanafunzi waliofaulu kwa viwango vya juu ni aina ya michepuo na shule za kuendelea nazo. Ni jambo la kawaida kukuta kijana akifaulu masomo mengi na kisha kusoma mchepuo ambao hana mapenzi nao sana. Hili husababishwa na mazingira ya ujazaji fomu za michepuo ya kuendelea nayo baada ya kuhitimu masomo. Hutokea kuwa mchepuo anaoupenda sana ana shaka ya kufanya vizuri na hivyo kuchaguwa michepuo mingine. Ama kwa upande wa shule, hutegemeana na nafasi, ufaulu wa wanafunzi na idadi ya wanafunzi walioomba katika Shule husika.

Baadhi ya wanafunzi wanapokosa michepuo au shule walizoomba huhangaika na kutumia muda mwingi wakitaka kubadilisha. Uzoefu unaonyesha kwamba ni sehemu ndogo za sana ya wanafunzi hao ambao hufanikiwa. Ushauri wetu ni kwamba endapo kijana atachaguliwa katika shule asiyoipenda na hakuna sababu za kiafya za kumfanya asiende katika shule hiyo pengine kutokana na hali ya hewa, au kachaguliwa mchepuo asioupenda na familiya yake haina uwezo wa kumsomesha shule binafsi, basi atulizane katika hicho alichopata na ajikite zaidi katika masomo kwani anaweza pia kufanikiwa katika fursa hiyo aliyoipata.

MASOMO KABLA YA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO (PRE FORM FIVE).
Changamoto nyingine ambayo huwakuta vijana wa kundi hili ni kuanza kusoma tuisheni za masomo ya kidato cha tano kabla ya uchaguzi kufanyika. Utata wa jambo hili ni kama tulioueleza hapo juu wa mwanafunzi kuchaguliwa mchepuo tofauti kabisa na masomo anayosoma. Kwa mfano kuna kijana tunayemfahamu akisoma masomo ya mchepuo wa Economics, Geography na Mathematics (EGM) lakini akachaguliwa mchepuo wa History, Kiswahili na Language (HKL). Tofauti iliyoje! Katika hilo inashauriwa kuwa kama mwanafunzi hana hakika ya kusoma katika shule binafsi, asianze masomo hayo mpaka baada ya uchaguzi wa kidato cha tano kufanyika. Na ikibidi kujisomea asome vitu vya jumla kama masomo ya lugha, kompyuta nk.
KUJIUNGA NA SHULE BINAFSI
Kwa wale waliokwisha amua au lazima wasome katika shule binafsi, ni muhimu kufanya utafiti juu ya ubora wa shule hizo kitaaluma, maadili na stadi nyingine za maisha. Aidha ni muhimu kufuatilia juu ya kiwango cha ada, muda wa kuchukuwa na kurejesha fomu za maombi, tarehe ya usaili na ya kufungua shule. Hutokea mwanafunzi akapoteza muda na hatimaye kuhangaika kutafuta shule wakati shule nyingi zimeshasimamisha kupokea wanafunzi.

Kuna wanafunzi waliopata daraja la tatu ambao hawatapata nafasi ya kujiunga na kidato cha tano. Hata hivyo vijana waliopata daraja la tatu na sehemu ndogo ya waliopata daraja la nne huwa wanapata sifa na wanaweza kujiunga na kidato cha tano katika shule binafsi endapo uwezo wa familiya unaruhusu. Hii ni kutokana na kanuni za Wizara ya Elimu ambazo zinamruhusu mwanafunzi kuendelea na masomo ya kidato cha tano endapo amefaulu katika kiwango cha angalau alama C kwa masomo matatu au zaidi hata kama masomo aliyofaulu hayatengenezi mchepuo wowote mfano Civics, Biology na English huku akiwa amepata alama D au chini yake katika masomo mengine. Endapo familiya itamudu kumsomesha kidato cha tano kati shule binfasi, ni vema kijana akapata ushauri wa wazazi, walimu na wazoefu wengine juu ya mchepuo stahiki unaomfaa. Mara nyingi wanafunzi wa aina hii huwa wanashindwa kutofautisha baina ya matashi ya nafsi na uwezo binafsi wa kimasomo. Kwamba kijana tuliyemtaja hapo juu asome mchepuo wa CBG au HGL ni suala linalohitaji tafakuri pamoja na mhusika.

KUJIUNGA NA VYUO VYA UALIMU
Kuna wanafunzi waliopata daraja la tatu na hata daraja la nne ambao hawatachaguliwa kujiunga na kidato cha tano lakini watachaguliwa kujiunga na vyuo vyuo vya Ualimu. Kwa mujibu wa kanuni zilizopo sasa, kiwango cha ufaulu cha mwisho kuchukuliwa ni daraja la nne na pointi 28. Pamoja na kujaza nafasi za masomo ya Ualimu ngazi ya cheti, mwanafunzi atapaswa kuomba rasmi nafasi hizo kupitia Wizara ya Elimu baada ya matokeo kutoka na nafasi kutangazwa rasmi. Aidha kutokana na uchache wa nafasi katika vyuo huwa si wote walio na sifa wanaoweza kuchaguliwa. Wanafunzi wenye sifa lakini hawakuchaguliwa katika vyuo vya serikali, wanaweza kujiunga na vyuo binafsi vya ualimu endapo uwezo wa familiya kiuchumi unaruhusu.

KUJIUNGA NA VYUO VINGINE.
Wapo vijana ambao licha ya kuwa na sifa za kuchaguliwa katika vyuo vya ualimu, huwa hawachagui au hawaendi hata baada ya kuchaguliwa kwasababu zao binafsi. Kama uwezo wa familiya unaruhusu na inaona kusoma ualimu si kipaumbele cheo, haina tatizo. Hata hivyo, ni vema kuangalia fursa zilizopo na uwezo wa familiya kiuchumi. Kijana anapaswa kufahamishwa na kufahamu kuwa si busara kwa familiya yenye uwezo duni wa kiuchumi, kama zilivyo familiya nyingi za kitanzania, kumsomesha kijana katika ngazi hii kwa gharama kubwa wakati kuna wengi wanahitaji kuendelezwa kitaaluma katika familiya.

Wale wote waliokosa nafasi ya kujiunga na kidato cha tano, vyuo vya ufundi au vyuo ualimu, fursa pekee waliyonayo ni kujiunga na vyuo vingine vinavyotoa kozi mbalimbali katika ngazi ya cheti katika Biashara, Utawala, Ufundi, Afya, Kilimo, Mifugo, Uvuvi, Maendeleo ya Jamii, nk. Vyuo kama Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Usimamizi wa Fedha (IFM), Uhasibu (TIA), Kodi, Utumishi wa Umma, Serikali za Mitaa (LGTI), Ardhi, Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Ukutubi na Uhifadhi Nyaraka, Mahakama, Ustawi wa Jamii, Elimu ya Watu Wazima, ni mifano michache katika ya vyuo vingi vilivyopo. Changamoto kubwa katika vyuo hivi ni uwezo wa kuzimudu gharama za mafunzo hayo. Hata hivyo, mara nyingi gharama za mafunzo katika vyuo vya Serikali kama Afya, Kilimo, Ufugaji, Ufundi, Uvuvi, nk huwa nafuu sana kuliko vyuo binafsi.

WANAFUNZI WALIOFELI KABISA
Mwanafunzi aliyefeli kabisa na kupata daraja la sifuri, hana fursa yoyote katika zote zilizotajwa hapo juu. Hata hivyo anakuwa amepata cheti cha kuhudhuria masomo (leaving certificate) ambacho huwa na msaada fulani katika maisha kwani kuna wakati huhitajika vijana waliomaliza kidato cha nne bila kujali ufaulu wao.

Pia kuna fursa zinazohitaji vijana waliomaliza shule ya msingi ambazo bado zinaweza kutumiwa na vijana hawa. Kwa mfano kuna fani mbalimbali zinazotolewa na vyuo vilivyo chini ya VETA ( vya serikali na binafsi) kama ufundi, udereva, usafi, utunzaji bustani, ushonaji, upishi nk ambazo zinaweza kutumiwa vema na vijana ambao hawakufaulu mitihani ya kidato cha nne.

Ni muhimu kutaja hapa kwamba si wale tu waliofeli ndio wanaoweza kuzitumia fursa za mafunzo ya VETA bali hata wale waliopata daraja la nne na hata daraja la tatu ambao ama hawakupata fursa za kuchaguliwa kidato cha tano au familiya zao hazimudu kuwasomesha katika shule au vyuo vya kujilipia.
KURUDIA MITIHANI

Wanafunzi wengi wanaofanya vibaya katika mitihani yao, jambo la haraka linalowajia vichwani ni kurudia mitihani. Ndio maana siku hizi vituo vinavyotoa mafunzo kwa wanaorudia mitihani vimekuwa vikiongezeka kila kukicha. Ni kwakuwa soko linakuwa na wateja wameongezeka.

Pamoja na kuunga mkono na kuheshimu juhudi za wanaotoa mafunzo hayo, tungependa tutanabahishe kwamba ili kuepusha upotevu mwingi wa muda na pesa, ni vema mwanafunzi akawa akijiandaa kurudia mitihani huku akijifunza ujuzi mwingine. Uzoefu unaonyesha kuna wanafunzi wanaorudia mitihani na matokeo yao kuwa mabaya kuliko ya mwaka uliotangulia. Aidha kuna wanafunzi waliorudia mitihani zaidi ya mara moja na bado hawakufanikiwa kupata alama C (credits) tatu au zaidi walizohitaji ili wajiunge na kidato cha tano.

Endapo mwanafunzi atajiandaa kurudia mitihani huku anapata ujuzi mwingine mfano udereva, ufundi,nk anakuwa katika nafasi nzuri ya ajira hata asipofaulu mitihani yake anayorudia. Ni uzuri ulioje endapo atapata vyote - credits na huku ana cheti cha ujuzi wake.

Jambo hili linawezekana endapo kijana ataugawa vizuri muda wake chini ya muongozo wa familiya. Kwa mfano asubuhi anakwenda chuoni kupata ujuzi na jioni anakwenda tuisheni kwa ajili ya kurudia mitihani. Aidha endapo mwanafunzi hatofanikiwa kupata credits, anaweza kuanza kazi huku ajiandaa taratibu kurudia mitihani yake. Wengi wamefanikiwa kwa utaratibu huu.

KUKATA RUFAA JUU YA MATOKEO
Wapo wanafunzi ambao wanakuwa hawakuridhika na matokeo waliyopata wakiamini hawakutendewa haki katika usahihishaji pengine kwa kuzingatia rekodi za matokeo yao katika mitihani ya shuleni au kwa jinsi walivyofanya mitihani.

Kwamba hatupingi jambo hili ndivyo pia tungependa kusisitiza kuwa wakati kijana akikusudia hilo ni vema akaendelea na mipango mingine ya kujiendeleza kama tulivyoitaja hapo juu. Hii ni kwasababu ni wanafunzi wachache sana ambao matokeo yao hubadilika baada ya mitihani yao kusahihishwa upya. Aidha anaweza kupoteza muda mwingi akisubiri hatma ya rufaa yako na kisha majibu kuja asivyotarajia.
UFADHILI WA MASOMO
Hutokea wanafunzi waliopata nafasi za masomo katika shule binafsi au vyuo vinavyohitaji kujilipia wakawa hawana uwezo wa kujisomesha na hivyo kuhangaika huku na kule kutafuta ufadhili. Ukweli ni kuwa ni wachache sana ambao hufanikiwa. Hii ni kutokana na kutokuwa na taasisi rasmi zinazotoa ufadhili katika viwango hivi ya elimu nchini.

Pamoja na kutokatishana na tamaa, ni vema kijana anapokuwa katika hali hiyo kutafuta shughuli itakayokuwezesha kujenga nguvu za kiuchumi na kisha kuweka akiba kwa ajili ya kujisomesha. Unaweza kuweka malengo ya kusoma huku ukifanya kazi. Endapo shughuli zako hazikupi fursa ya kusoma huku ukifanya kazi, unaweza kuahirisha kusoma hadi kipindi fulani baada ya kujiimarisha kiuchumi. Endapo hilo litakuwa gumu kulitekeleza, familiya iangalie uwezekano wa kuuza sehemu ya rasilimali ilizo nazo ambazo hazitaithiri familiya nzima endapo zitauzwa.

Tuhitimishe kwa kusema, matokeo vyovyote yawavyo hayawezi kuwa ndio mwisho wa maisha. Siku zote wanaofanikiwa ni wale wanaotazama mbele huku wakijifunza kwa yaliyowatokea. Walofaulu washukuru huku wakijipanga; waliofanya vibaya wasubiri huku wakijifuza. Tumia vizuri kila fursa unayoipata bila kujali udogo wake. Jifunze kwa wengine, uliza, pata miongozo kwa waliokutangulia, na amini kuwa ipo siku utafanikiwa. Washindi huwa hawaachi, na wenye kuacha huwa hawashindi.

Imetolewa na:

Kitengo cha Elimu - Jumuiya ya Wataalam wa Kiislam Tanzania (TAMPRO)

TAMPRO imeandaa kitabu kinachoonyesha orodha ya vyuo ambavyo mhitimu wa kidato cha nne na kidato cha sita anaweza kujiunga, muda wa kujiunga, sifa za kujiunga na gharama za masomo. Kitabu hicho kitatoka hivi karibuni inshaAllah.