Tuesday, January 08, 2013

KUTEULIWA KWA CHUCK HAGEL KWAZUA UTATA


Rais  wa  Marekani  Barack Obama  amemteua  Chuck Hagel  jana  kuiongoza  wizara  ya  ulinzi, na  hatua  hiyo inaelekea  kuzusha  mvutano  mkubwa  katika  hatua  za kumuidhinisha  wakati  wapinzani  kutoka  chama  cha Republican , wamesema  amekuwa  na  msimamo  mkali zaidi  kwa  Israel  na  amekuwa  na  mtazamo usio mkali dhidi  ya  Iran. Chaguo  la  Obama  kwa  John Brennan kuchukua  nafasi  ya  David Patraeus  kama  mkuu  wa shirika  la  ujasusi  la  Marekani  CIA  linaonekana  kuwa halitakuwa  na  matatizo  licha  msimamo  wa  kiongozi huyo katika  kuunga  mkono  mbinu  za  usaili  na  vita vinavyotumia  ndege zisizo na  rubani.Akimsifu Brennan rais Obama  amesema.
O-Ton Obama

Mabadiliko  ya  kikosi  cha  rais Obama  katika  idara  ya usalama  wa  taifa  yanaonekana  yataidhinishwa , lakini wabunge  waandamizi  wa chama  cha  Republican wameashiria  kuwa  haitakuwa  rahisi  kwa  Hagel  kupita licha  ya  kuwa  anatoka  katika  chama  hicho.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO