Tuesday, July 09, 2013

MRIPUKO WAUWA KADHAA LEBANON

Watu  kadha wamejeruhiwa  wakati  bomu  lililotegwa katika  gari  liliporipuka  katika  kitongoji  cha  kusini  mwa mji  wa  Beirut  leo, sehemu  ambayo  ni  ngome  kuu  ya kundi  la  wanamgambo  wa   Kishia  la  Hezboullah ambalo  limeingilia  kati  mapigano  katika   vita  vya wenyewe  kwa  wenyewe  nchini  Syria.
Wasi  wasi  umetanda  nchini  Lebanon  kufuatia  kundi hilo  la  wanamgambo  kuingilia  kati  mapigano  nchini Syria  wakisaidia  upande  wa  rais  wa  nchi  hiyo  Bashar al-Assad, ambaye  majeshi  yake  yanapambana  na  uasi uliodumu  miaka  miwili  sasa  ukiongozwa  na  Waislamu wa  madhehebu  ya  Sunni  ambao  ndio  wengi  nchini humo.
Wingu  la  moshi  mweusi  lilikuwa  linatoka  katika  jengo linaloishi  watu  wengi  katika  kitongoji  hicho  cha  kusini mwa  mji  mkuu  Beirut. Eneo  hilo  lenye  maduka  mengi huenda  lilikuwa  limejaa  watu  leo, siku  ya  mwanzo  ya mfungo  wa  Ramadhan.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO