Wednesday, December 19, 2012

KOREA KUSINI WACHAGUA RAIS

Upigaji  kura  umemalizika  hivi  sasa  nchini  Korea  ya kusini  katika  uchaguzi  wa  rais. Mgombea  wa  chama tawala  cha  kihafidhina  Park Guen-hye anapambana  na mgombea  wa  upinzani  Moon Jae In  kutoka  chama  cha Democratic United Party. Park ambaye  ni  mtoto  wa dikteta  wa  zamani nchini  humo  marehemu Park Chung-hee anapewa  nafasi  ya  ushindi  ambayo  hata  hivyo  ni finyu  katika  uchunguzi  wa  maoni  ambao  umechapishwa wiki  iliyopita. Iwapo  atashinda  atakuwa  kiongozi  wa kwanza  mwanamke  nchini  humo  ambako  wanaume bado  wanashikilia  nafasi  muhimu  za  madaraka. Lakini Moon, mwanasheria  wa  zamani  wa  haki  za  binadamu na  mtoto  wa  kiume  wa mkimbizi   kutoka  Korea  ya kaskazini  anasemekana  kujiongezea sana umaarufu katika  siku  za  hivi  karibuni. Upigaji  kura  umekamilika na, matokeo  ya  awali  yatatolewa  muda  mfupi  baadaye. Mshindi  wa  uchaguzi  huo  atachukua  madaraka mwishoni  mwa  mwezi  wa  Februari, akichukua  nafasi  ya rais  wa  sasa  Lee Myung Bak.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO