Friday, December 21, 2012

NJAMA ZA MAADUI ZIMEFELI MBELE YA TAIFA LETU

Rais Mahmoud Ahmadinejad wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, nguvu kubwa iliyoonyeshwa na wananchi wa Iran, imeweza kuzima njama zote za maadui. Akizungumza kwenye Kongamano la Wakuu wa Mikoa hapa nchini, Rais Ahmadinejad ameongeza kuwa, katika hali ambayo maadui wamekuwa wakiongeza mbinyo na mzingiro wao siku hadi siku, wananchi wa Iran wameweza kuonyesha nguvu na uwezo wao kwa kuwashinda  maadui. Ameongeza kuwa, wananchi wa Iran wamevibadilisha vikwazo vya upande mmoja vya nchi za Magharibi na kuwa fursa ya kupiga hatua za kimaendeleo hapa nchini. Rais Mahmoud Ahmadinejad amebainisha  uchaguzi wa rais uliopangwa kufanyika hapo mwakani na kuongeza kuwa,  wananchi wa Iran wanatakiwa kujitokeza kwa wingi  kwenye uchaguzi huo kama ilivyokuwa kwenye chaguzi zilizopita, na kamwe maadui hawawezi kuziathiri irada za wananchi wa Iran. Rais Ahmadinejad ameongeza kuwa, uchaguzi wa Iran umekuwa ukitoa  athari kubwa katika eneo la Mashariki ya Kati na ulimwengu mzima, kutokana umuhimu maalumu  uliokuwa nao.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO