Wednesday, January 09, 2013

RWANDA YAPINGA KUTUMWA DRONE DRC


Rwanda imepinga hatua ya kutumia   ndege  zisizokuwa na  rubani  katika  uchunguzi  mashariki  ya  Congo  kama ilivyopendekezwa  na  umoja  wa  mataifa  hadi  pale patakapokuwa  na  tathmini   kamili  ya  matumizi  yake, ikisema  kuwa  haitapenda  Afrika  kuwa sehemu  ya majaribio  kwa  ajili  ya  upelelezi  wa  kutumia  vyombo  vya mataifa  ya  nje. Wajumbe  wamesema  kuwa  mkuu  wa ulinzi  wa  amani  wa  Umoja  wa  Mataifa  Herve Ladsous ameliambia  baraza  la  usalama jana katika  kikao  cha faragha  kuwa  ujumbe  wa  umoja  wa  mataifa  katika jamhuri  ya  kidemokrasi  ya  Congo  unapanga  kutumia ndege  tatu  ambazo  hazina rubani , katika  jimbo  la mashariki  ya  nchi  hiyo  lililokumbwa  na  mzozo.
Umoja  wa  mataifa  ulihitaji ndege  hizo  zisizokuwa  na rubani  kwa  ajili  ya  uchunguzi  katika  eneo  la  mashariki mwa  Congo  tangu  mwaka  2008.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO