WAASI WA KORDOFAN |
Saturday, January 12, 2013
SUDAN YAANGAMIZA WAASI 50 KORDOFAN KUSINI
Jeshi la taifa la Sudan limefanikiwa kuwaangamiza waasi zaidi ya 50 na kuwajeruhi makumi ya wengine katika jimbo la Kordofan Kusini. Jeshi la Sudan limeeleza kuwa, mapigano hayo makali kati ya jeshi la serikali na kundi la waasi wa 'Harakati ya Mapinduzi' linaloundwa na makundi manne ya waasi yalijiri umbali wa kilomita 15 kutoka eneo la Kadugli, lililoko katikati mwa jimbo la Kordofan Kusini. Kabla ya hapo siku ya Jumanne iliyopita, Umoja wa Mataifa ulitahadharisha kuwa, mapigano yanayojiri katika jimbo la Kordofan Kusini yataleta athari mbaya kwa wananchi wa eneo hilo na maisha ya wananchi hao yatakuwa hatarini.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment
TUPE MAWAZO YAKO