Wednesday, December 19, 2012

OBAMA AUNGA MKONOO KUPIGWA MARUFUKU SILAHA

Ikulu  ya  Marekani  imesema  kuwa  Rais Barack Obama anaunga  mkono  juhudi  za  kurejesha  sheria  ya  kupiga marufuku sihala kali. Msemaji  wa  Ikulu hiyo, Jay Carney, amesema  kuwa  rais  anaunga  mkono pendekezo  la seneta  wa  chama  cha  Democratic,  Dianne Feinstein, kuirudisha tena sheria hiyo, baada  ya  mauaji  yaliyotokea mjini  Newtown, Connecticut. Carney  ameongeza  kuwa Obama  pia  ataunga  mkono  sheria  ya  kufunga  kile alichokieleza  kuwa  ni mapungufu  katika  mauzo  ya silaha. Alikuwa  akizungumzia  kuhusu  sheria  ambazo zinaruhusu  watu  kununua  bunduki  kutoka  kwa  wauzaji binafsi  bila  ya  kufanyiwa  uchunguzi   kuhusu  maisha yao. Watoto  20  na  watu wazima 6  waliuwawa  Ijumaa iliyopita   katika  shule  ya  msingi  ya  Sandy Hook na kuanzisha  upya  mjadala  kuhusu  udhibiti  wa  silaha nchini Marekani. Chama  chenye  ushawishi  mkubwa  cha wamiliki  wa  bunduki  nchini  Marekani  kimezungumza kwa  mara  ya  kwanza   jana,  na  kusema  kinataka kuchangia  kwa  dhati  katika  kuzuwia  mauaji  mengine  ya halaiki.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO