Tuesday, December 18, 2012

RAIS WA UJERUMANI AZURU VIKOSI VYAKE AFGHANISTAN


Rais  wa  Ujerumani, Joachim Gauck, amefanya  ziara kuvitembelea  vikosi  vya  jeshi  la  Ujerumani  vilivyoko nchini Afghanistan. Gauck alikutana  na   vikosi  vya  jeshi hilo vilivyoko  katika  eneo  la  Mazar-e-Sharif, ambako kuna  kituo  kikubwa  katika  jimbo  hilo.
Amewashukuru  wanajeshi  hao  pamoja  na  wafanyakazi wa  kutoa  misaada  ambao  wanafanya kazi  kuleta  amani na  demokrasia  nchini  humo.
Jeshi  la  ulinzi  la  Ujerumani  limeanza  kupunguza wanajeshi  wake  nchini  Afghanistan, pamoja  na kuongeza  uwezo  wake  wa  jumla  wa  kushambulia. Helikopta kadhaa  chapa  Tiger zimepelekwa  hivi  karibuni katika  jimbo hilo, ikiwa ni  mara  ya  kwanza  kwa  majeshi ya Ujerumani  kusaidiwa  na  helikopta zake yenyewe.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO