Tuesday, December 18, 2012

WAHANGA WA MAUAJI MAREKANI WAZIKWA


Watoto  wawili  wahanga  wa  mauaji  ya  wiki  iliyopita katika  jimbo  la  Connecticut  nchini  Marekani  wamezikwa. Watoto wa kiume  wawili  wenye umri wa miaka  sita, Noah Pozner  na  Jack Pinto , walikuwa  miongoni mwa  watoto 20 waliouawa wakati  mtu  mwenye silaha  alipowafyatulia risasi  katika  shule  ya  msingi  mjini  Newtown Ijumaa iliyopita. Watu wazima sita  ambao  ni  wafanyakazi  wa shule  hiyo pia  wameuawa  pamoja  na mama  wa mshambuliaji  huyo.
Shambulio  hilo  la  silaha  limezusha  mjadala  kuhusu udhibiti  wa  silaha  nchini  Marekani, ambapo  maseneta wawili wakiungwa  mkono  na  kundi  lenye  ushawishi mkubwa  linalopendelea  umiliki  wa  silaha, wakitoa  wito jana  kuwapo  na  mabadiliko  katika  sheria  za  umiliki  wa silaha.
Wakati  hakutaja  moja  kwa  moja  mageuzi  katika  umiliki wa  silaha  wakati  wa  hotuba  yake mwishoni  mwa  juma, rais  wa  Marekani  Barack Obama  jana  alikutana  na makamu  wa  rais Joe Biden  pamoja  na  baraza  la mawaziri  kujadili  njia  za  kuchukua.
Msemaji  wa  rais  Obama  hakutoa  maelezo kamili  lakini amesema  mpango  wake  umekwenda  mbali  zaidi  ya udhibiti  wa  silaha.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO