Wednesday, December 19, 2012

WAMAREKANI WALAUMIANA MASHAMBULIZI UBALOZI WA BENGHAZI


Ripoti rasmi kuhusiana na mashambulizi mabaya ya mwezi Septemba dhidi ya ubalozi mdogo wa  Marekani mjini Benghazi,  imegundua kuwa  kulikuwa  na  upungufu mkubwa  katika  hatua za  kiusalama  za  wizara  ya mambo ya  kigeni. Katika  tathmini  ambayo  inatoa  lawama  kali jopo  lililopewa  jukumu  la  uchunguzi  wa  tukio  hilo limeelezea  kuwepo kwa mapungufu kadhaa, ikiwa  ni pamoja  na  ukosefu  wa  watu  wenye  ujuzi  pamoja  na uongozi mbaya. Ripoti  hiyo  ina  mapendekezo  29, ambayo  yote  yamekubaliwa  na  waziri  wa  mambo  ya kigeni  wa  Marekani  Hillary Clinton. Katika  barua  kwa kamati  za  bunge  la  Marekani, amesema  kuwa ameelekeza  wizara  yake  kutekeleza yale  yaliyomo  katika ripoti  hiyo haraka  na  kwa  ukamilifu  wake. Maafisa wanne  wa  Marekani  waliuawa  tarehe  11  mwezi Septemba, ikiwa  ni  pamoja  na  aliyekuwa balozi  wa Marekani  nchini  Libya, Christopher Stevens.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO