Tuesday, January 15, 2013

JESHI LANIGERIA LAMTIA MKONONI KIONGOZI WA BOKO HARAM

Jeshi la Nigeria limemtia mbaroni Muhammad Zangina mmoja wa viongozi wa kundi la Boko Haram. Taarifa ya jeshi la Nigeria imesema, Zangina ametiwa mbaroni karibu na mji wa Maiduguri. Jeshi la Nigeria limesema kuwa, Zangina anatuhumiwa kuhusika ana mashambulio kadhaa ya kigaidi dhidi ya raia na vikosi vya polisi katika mji wa Maiduguri na kwamba, ametiwa mbaroni masaa machache kabla ya kutekeleza mpango wa mashambulio mengine katika mji huo. itakumbukwa kuwa, serikali ya Nigeria ilikuwa imetenga kitita cha dola laki moja na sitini elfu kama zawadi kwa atakayetoa taarifa za uhakika za kutiwa mbaroni Muhammad Zangina. Kundi la Boko Haram linatuhumiwa kuhusika na mauaji mengi yaliyofanyika nchini Nigeria, na wanachama wake wamekuwa wakisakwa kwa udi na uvumba na jeshi la nchi hiyo. Hadi sasa mamia ya watu wameshapoteza maisha yao na majengo kadhaa ya serikali na makanisa kuchomwa moto kutokana na mashambulio yanayofanywa na kundi hilo kaskazini mwa Nigeria.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO