Tuesday, January 15, 2013

KARZAI : KUONDOKA KWA WAGENI KUTAIMARISHA USALAMA

Rais Hamid Karzai wa Afghanistan amesema kuondoka majeshi ya kigeni nchini mwake kutapelekea kuimarika hali ya usalama na amani.
Rais Karzai amesema wanajeshi wa kigeni ndio chanzo cha kudorora hali ya usalama kutokana na jinsi wanavyoamiliana kikatili na wananchi wa Afghanistan. Amefafanua kwamba, kutokana na wenyeji kuwachukia wavamizi wa kigeni, makundi ya wanamgambo yamezidi kupata nguvu na uungaji mkono na hivyo kudhoofosha hali ya usalama. Hamid Karzai amerudi kutoka Marekani ambako Rais Barack Obama amemshinikiza akubali majeshi 9000 wa Marekani kubakia Afghanistan baada ya mwaka ujao wa 2014 ambapo majeshi yote ya kigeni yanapaswa kuondoka. Obama pia ametaka majeshi hayo yapewe kinga ya kisheria ili mwanajeshi yeyote wa Marekani asiweze kushtakiwa kwa makosa yoyote katika ardhi ya Afghanistan.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO