Saturday, January 19, 2013

MADAKATARI WA UFARANSA WAZUIWA KUINGIA MALI


Kundi la Misaada la Madaktari wasio na Mipaka wa Ufaransa limeeleza kuwa timu yake ya huduma za kitiba imezuiwa kufika katika maeneo yaliyoathiriwa na mgogoro unaondelea sasa huko Mali. Taasisi hiyo isiyo ya kiserikali ya Ufaransa imesema kuwa imekuwa ikiwasiliana na maafisa wa Mali na raia wa nchi hiyo tangu Januari 14 na pia na serikali  na jeshi la Ufaransa  ili kuruhusiwa kutuma timu yake ya madaktari katika mji wa Konna huko katikati mwa Mali.
Kundi la Madaktari wasio na Mipaka la Ufaransa limesema kuwa timu yake ya madaktari imeshindwa kuhudumia majeruhi katika medani za vita licha ya kundi hilo kutoegemea upande wowote, tangu vikosi vya Mali na Ufaransa vianzishe oparesheni ya kijeshi huko Mali hivi karibuni. Januari 11 mwezi huu Ufaransa ilianzisha uingiliaji kijeshi huko kaskazini mwa Mali kwa kisingizio cha kutaka kuwazuia waasi kusonga mbele nchini humo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO