Monday, January 21, 2013

RUSSIA YAANZA MAZOEZI MAKUBWA YA KIJESHI SYRIA


 Russia imeanza kufanya mazoezi makubwa zaidi ya jeshi lake la majini katika bahari za Mediterranean na Bahari Nyeusi karibu na maji ya Syria ambayo inakabiliwa na mashambulizi ya magenge ya waasi. Hayo ni mazoezi makubwa zaidi ya Jeshi la Majini kuwahi kufanywa na Russia kwa makumi ya miaka. Taarifa rasmi ya Wizara ya Ulinzi ya Russia imesema kuwa, luteka hiyo ya kijeshi inafanyika katika utaratibu wa Vikosi vya Ulinzi vya Russia wa mwaka 2013 wa kujiimarisha kiulinzi na kuzingatia zaidi suala la kufanya kazi kwa pamoja vikosi vya nchi hiyo kutoka makundi mbalimbali ya manowari zake zinapokuwa kwenye maji ya mbali.
Maneva hayo ya Jeshi la Majini la Russia yataendelea hadi tarehe 29 mwezi huu wa Januari kwa kufanya mazoezi mbalimbali na kujaribisha silaha na mbinu tofauti za kivita. Russia inazilaumu nchi za Magharibi kwa kuchochea mauaji na uasi nchini Syria ambayo imekuwa ikishuhudia machafuko tangu katikati ya mwezi Machi 2011. Raia wengi na maafisa usalama wa serikali ya Syria wameuawa katika machafuko hayo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO