Monday, January 21, 2013

DRONE YA MAREKANI YAUA RAIA NANE YEMEN


Watu wanane  wameuawa katika hujuma ya hivi karibuni ya ndege isiyo na rubani (drone) ya Marekani huko Yemen katika mkoa wa Marib. Walioshuhudia wanasema hujuma hiyo imejiri Jumamosi usiku katika bonde la Abeida . Maafisa wa Jeshi la Yemen wamethibitisha kutokea hujuma hiyo lakini hawakutoa maelezo zaidi. Mara kwa mara ndege zisizo na rubani za Marekani hutekeleza mashambulizi katika maeneo kadhaa ya Yemen kwa kisingizio cha kupambana na magaidi. Hata hivyo wahanga wakuu wa hujuma hizo za Marekani ni raia wakiwemo wanawake na watoto wasio na hatia. Marekani inatekeleza hujuma za ndege zisizio na rubani katika nchi kadhaa za Kiislamu kama vile Afghanistan, Pakistan na Somalia kwa kisingizio hicho hicho cha kupambana na ugaidi lakini wahanga wakuu huwa ni raia. Marekani imetangaza kuwa tayari kutumia ndege zake hizo za kivita huko Mali ambayo pia ni nchi ya Kiislamu. Wataalamu wanasema hujuma hizo za ‘Drone’ ni ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO