Tuesday, December 04, 2012

IRAN YAIKAMATA NDEGE YA MAREKANI ISIYOKUWA NA RUBANI

Iran imeikamata ndege ya Marekani isiyokuwa na rubani ambayo ilikuwa ikiruka katika eneo la anga la nchi hiyo. Ndege hiyo ilikuwa ikikusanya taarifa katika eneo la Bahari ya Ghuba na kuingia katika anga ya Iran wakati ilipokamatwa na kikosi cha jeshi la majini.


Jeshi la walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu hapa nchini limefanikiwa kukamata ndege ya kijasusi ya Marekani isiyo na rubani punde baada ya kuingia kinyemela katika anga ya Iran.
'Drone' hiyo ijulikanayo kama Scan-Eagle inasemekana kuwa na teknolojia ya kisasa zaidi ya kueza kuepuka rada lakini jeshi la Iran limeweza kugundua janjajanja za Washington na kuikamata ndege hiyo isiyo na rubani.
Wataalamu wa masuala ya kijeshi wamesema kuwa, Iran imeonyesha ustadi mkubwa kwa kuinasa ndege hiyo ya kijasusi na kwamba hiyo ni kengele ya hatari kwa Marekani kwamba uwezo wa kijeshi wa Iran ni mkubwa kushinda wanavyodhania.
Huko nyuma pia jeshi lilifanikiwa kuangusha ndege nyingine ya Marekani isiyo na rubani baada ya kuingia katika anga ya Iran bila idhini.
Huku hayo yakijiri, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Ramin Mehmanparast amekosoa njama mpya ya kuiwekea Iran vikwazo vipya akisema si mashinikizo wala vikwazo vitaipigisha magoti serikali ya Iran na kwamba mashindikizo na vikwazo hivyo ni kinyume cha sheria.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO