Sunday, December 30, 2012

JESHI LA MAJINI LA IRAN LAENDELEA NA MAZOEZI MAKALIA


Jeshi la Wanamaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran linaendeleza mazoezi makubwa ya kijeshi ambapo ndege zisizo na rubani pamoja na ndege za upelelezi na helikopta zimetumika katika luteka hiyo. Akizungumza na Shirika la Habari la Fars, Admeli Amir Rastegari ambaye ni msemaji wa maneva hiyo ameongeza Jumamosi ilikuwa siku ya pili ya mazoezi hayo ambapo jeshi la wanamaji lilionyesha mbinu zake katika kukabiliana na adui baharini. Mazoezi hayo ya Jeshi la Wanamaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran yaliyopewa jina la ‘Wilayat 91’ yalianza Ijumaa na yataendelea kwa muda wa wiki moja.  Luteka hiyo itafanyika katika eneo lenye ukubwa wa kilomita mraba milioni 1 kutoka Ghuba ya Uajemi hadi Bahari ya Hindi na Ghuba ya Aden. Mazoezi hayo yanajumuisha nyambizi, manoari, makombora, ndege zisizo na rubani na vita vya kielektroniki.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO