Thursday, December 27, 2012

WANAJESHI WA ISRAEL WAJIUA WENYEWE


Wanajeshi wasiopungua 237 wa utawala haramu wa Israel wamejiua katika nyakati mbali mbali katika kipindi cha miaka kumi iliyopita. Kwa mujibu wa nyaraka za siri za jeshi la Israel, kwa uchache wanajeshi 24 wa utawala huo hujiua kila mwaka.
Press TV imesema nyaraka hizo za siri zilitolewa kwa mara ya kwanza na mwanablogi wa Israel ambaye alikamatwa na polisi na kusailiwa. Mwanablogu huyo amesema idadi ya askari wa Jeshi la Israel waliojiua ni zaidi ya iliyotangazwa rasmi. Hivi karibuni Wizara ya Vita ya Israel ilikiri kuwa idadi ya wanajeshi wake wanaojiua ni zaidi ya wanaouawa vitani.
Jeshi la utawala haramu wa Israel limeshindwa kwa madhila mara kadhaa katika vita dhidi ya wanamapambano wa Palestina na Lebanon. Katika hujuma yake ya hivi karibuni dhidi ya Ukanda wa Ghaza, utawala haramu wa Israel ulilazimika kuomba usitishwaji vita baada ya jeshi lake kushindw akukabiliana na maroketi ya wapigania ukombozi wa Palestina.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO