Thursday, February 28, 2013

IRAN YAIKOSOA VIKALI FILAMU YA ARGO


Waziri wa Utamaduni na Mwongozo wa Kiislamu wa Iran amekosoa vikali tuzo ya Oscar kutunukiwa filamu ya ARGO ambayo imetayarishwa huko Hollywood dhidi ya taifa la Iran. Dakta Muhammad Husseini amesema kuwa, Wamarekani wamefanya propaganda kubwa ndani ya filamu hiyo dhidi ya Iran na kusisitiza kwamba watengeneza filamu wa Kiirani walioshiriki katika filamu hiyo pia wana kesi ya kujibu.
Dakta Husseini amesema kuwa, filamu ya Argo ambayo imetangazwa kuwa filamu bora kabisa duniani mwaka 2013 na kupewa tuzo ya Oscar, ni dhaifu mno katika upande wa kiusanii. Amesema hatua ya kupewa tuzo ya Oscar filamu ya Argo iliyo dhidi ya Iran inaonyesha kuwa, Hollywood imeshindwa kwenye siasa za tasnia ya filamu.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO