Saturday, March 30, 2013

WAISLAM WA UJERUMANI WATAKA MAPUMZIKO SIKU YA EID

Baraza la Waislamu nchini Ujerumani limeitaka serikali ya nchi hiyo kutoa mapumziko ya sikukuu za Idul Fitr na Idul Adhha kwa Waislamu nchini humo. Ayman Mazyek Katibu  Mkuu wa Baraza la Waislamu nchini Ujerumani ametoa pendekezo hilo kwa serikali ya nchi hiyo. Amesema kuwa, iwapo pendekezo hilo litakubaliwa bila shaka  umoja na mshikamano  utazidi kuimarika kati ya jamii ya nchi hiyo. Hata hivyo Guntram Schneider mkuu  wa jimbo la Nordrhein - Westfalen amepinga takwa hilo la Baraza la Waislamu nchini Ujerumani kwa madai kuwa, kutaka kutolewe ruhusa ya siku mbili kwa Waislamu kusherehekea sikukuu za Idul Fitr na Idul Adhha eti kutazorotesha uchumi wa nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO