Wednesday, March 27, 2013

WAPALESTINA WAZUILIWA KUSWALI KWENYE HARAM YA NABII IBRAHIM


Chuo Kikuu cha al Azhar nchini Misri kimelaani vikali hatua ya viongozi wa utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuwazuia Waislamu kuingia na kufanya ibada kwenye Haram tukufu ya Nabii Ibrahim AS na badala yake wamefungua milango kwa walowezi wa Kizayuni kuingia kwenye eneo hilo takatifu. Viongozi wa utawala wa Kizayuni wa Israel kuanzia leo na kesho wamewazuia Waislamu kufanya ibada zao kwenye eneo hilo tukufu na badala yake wamewaruhusu walowezi wa Kizayuni kwa kisingizio cha kuadhimisha sikukuu za Kiyahudi.
Chuo Kikuu cha al Azhar kimesisitiza kuwa, Haram takatifu ya Nabii Ibrahim AS ni msikiti kamili na wala hauna mfungamano na Mayahudi na hali kadhalika haupasi kuvunjiwa heshima kwa namna yoyote ile. Taarifa hiyo imetahadharisha juu ya kuongezeka vitendo vya kulivunjia heshima eneo hilo, suala ambalo imesema linaziumiza nyoyo za zaidi ya Waislamu bilioni moja na nusu duniani. Taarifa hiyo pia imewataka Waislamu wote duniani na Umoja wa Mataifa kuchukua hatua za kukomesha haraka uvamizi huo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO