Sunday, April 21, 2013

SHUGHUI ZA UOKOAJI CHINA ZAKUMBWA NA CHANGAMOTO


Waokozi bado wanajaribu kuendelea na shughuli ya kutafuta manusura na miili zaidi katika eneo la milimani la Lushan Kusini Magharibi mwa China, baada ya tetemeko kubwa la ardhi lenye kipimo cha ritcher 6.6 kukumba eneo hilo hapo jana.
Huku hayo yakiarifiwa idadi ya waliofariki kutokana na tetemeko hilo lililosababisha maporomoko ya udongo imepanda na kufikia 203 huku watu wengine 11,800 wakiwa wamejeruhiwa vibaya. Tetemeko hilo liliharibu barabara na kukata mawasilianio ya simu na umeme katika eneo hilo.
Kwa sasa maelfu ya watu wanaendelea kukaa katika mahema wakiwa na hofu kubwa ya kurudi katika eneo hilo.Tetemeko kama hili lilitokea mwaka wa 2008 katika eneo hilo na kusababisha vifo vya takriban watu 70,000.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO