Friday, May 03, 2013

NDEGE YA JESHI LA MAREKANI YAANGUKA NA KUUA WANAJESHI


Ndege ya jeshi la Marekani imeanguka katika eneo la milima katika jimbo la Chuy nchini Kyrgyzstan. Maafisa wamesema kuwa watu watatu waliokuwa ndani ya ndege hiyo aina ya C-130, wote wanahofiwa kufariki. Ndege hiyo ilianguka muda mfupi baada ya kuruka kutoka uwanja wa jeshi la Marekani la Manas, ambao ni muhimu kwa operesheni za jeshi la nchi hiyo nchini Afghanistan.
Wizara ya Kyrgyzstan inayohusika na masuala ya dharura imesema kuwa hakuna aliyenusurika ajali hiyo, lakini taarifa za baadhi ya watu walioshuhudia ajali ya ndege hiyo zimeeleza kuwa rubani aliruka kwa kutumia mwavuli. Maafisa wa Marekani wamesema kuwa bado wanafanya uchunguzi kupata uhakika wa kile kilichotokea. Mwambata wa kijeshi wa Marekani nchini Kyrgyzstan aliripotiwa kutembelea eneo ilikotokea ajali hiyo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO