Saturday, June 29, 2013

IRAN NA RUSSIA KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA YA KIJESHI

Kamanda wa ngazi ya juu wa jeshi la majini la Russia amesema kuwa nchi yake na Iran zinachunguza mpango wa kufanya manuva ya pamoja katika bahari ya Caspian katika nusu ya pili ya mwaka huu. Iran na Russia mwaka 2009 zilifanya manuva ya kwanza ya pamoja ya baharini katika bahari ya Caspian iliyojumuisha meli za kivita 30. Katika manuva hayo yanayotarajiwa kufanywa katika nusu ya pili ya mwaka huu, maafisa wa jeshi la majini la Iran watavitembelea baadhi ya vituo vya kijeshi na bandari huko Russia na kufanya mikutano kadhaa na makamanda na viongozi wa ngazi za juu wa Russia. Tarehe 21 mwezi Aprili mwaka huu pia meli za kivita za Russia zilitia nanga katika bandari ya Bandar Abbas baada ya safari ndefu kutoka bahari ya Pacific.  

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO