Sunday, June 30, 2013

UMOJA WA ULAYA WATAKA UFAFANUZI TOKA MAREKANI

Rasi wa bunge la Ulaya Martin Schulz amesema anahitaji maelezo ya kina kutoka kwa Marekani baada ya shutuma mpya za kijasusi dhidi ya nchi hiyo. Martin Schulz amesema anawasi wasi mkubwa na kufadhaishwa juu ya madai ya Marekani kuzifanyia upepelezi ofisi za Umoja wa Ulaya.
Jarida la habari  nchini  Ujerumani, Der Spiegel, limeripoti Shirika la Usalama la Taifa nchini Marekani limekuwa likizitegesha taasisi za Umoja wa Ulaya ili kupata taarifa ya shughuli zake.
Katika ripoti yake iliyochapishwa jana kwenye mtandao, jarida hilo limesema kwamba majasusi wa Marekani walitumia virusi vya kompyuta na kunasa mazungumzo ya simu katika kupata taarifa kutoka taasisi za miji ya Washington, New York na Brussels.
Nyaraka hizo zilitolewa na Edward Snowden, mfanyakazi wa zamani wa Shirika hilo, ambaye katika siku za karibuni amevujisha nyaraka za siri kuhusiana na programu ya kuwafuatilia raia wa Marekani
Martin Schulz sasa amesema iwapo taarifa hizo zitakuwa ni za ukweli zitasababisha taathira kubwa katika uhusiano kati ya Umoja wa Ulaya na Marekani.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO