Friday, July 12, 2013

MISRI KUCHUNGUZA MADAI KUHUSU MORSI

Waendesha mashitaka nchini Misri watachunguza madai kuhusu rais aliyeondolewa madarakani, Muhammed Mursi kwamba alitoroka jela wakati wa vuguvugu la mageuzi  la mwaka 2011, akisaidiwa na kundi la wanamgambo la  Wapalestina la Hamas. Mwendesha mashitaka mkuu wa Misri, Hesham Barakat amepokea ushahidi kutoka kwenye mahakama moja ya Ismailia, utakaotumika kama msingi wa uchunguzi utakaofanywa na waendesha mashitaka wa serikali kwamba Mursi na viongozi wengine zaidi ya 30 wa chama cha Udugu wa Kiislamu, walitoroka jela. Wakati huo huo wafuasi wa Mursi na wale wanaompinga wanatarajiwa kufanya maandamano baadae leo mjini Cairo. Hali hiyo inazusha wasiwasi wa kutokea ghasia kutokana na jeshi kumpindua kiongozi huyo. Wafuasi wa Mursi wataandamana mashariki mwa Cairo, huku wanaompinga wakiandamana kwenye uwanja wa Tahrir.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO