Monday, August 19, 2013

MAREKANI YAANZA MAZOEZI YA KIJESHI NA KOREA KUSINI

Korea ya Kusini na Marekani zimeanza mazoezi ya pamoja ya kijeshi yanayofanyika kila mwaka ambayo kwa kawaida Korea ya Kaskazini huyaona kama ni mazoezi ya kujiandaa kuivamia nchi hiyo. Mazoezi hayo ya kijeshi yanawahusisha wanajeshi 30,000 wa Marekani na 50,000 wa Korea ya Kusini na yamepangwa kuendelea hadi mwishoni mwa mwezi wa Agosti. Safari hii shutuma za Korea ya Kaskazini dhidi ya mazoezi hayo hazijakuwa za juu sana kutokana na kwamba nchi zote mbili za Korea zimekuwa zikielekeza juhudi zao katika kulifunguwa tena eneo la pamoja la viwanda ambalo lilifungwa hapo mwezi wa Aprili wakati wa mvutano wa kijeshi wa hivi karibuni katika Ghuba ya Korea. Baada ya duru saba za mazungumzo, nchi hizo mbili hasimu wiki iliopita zilikubaliana juu ya mpango wa kuanza tena kazi katika eneo hilo viwanda la Kaesong ambalo ni muhimu katika kuipatia mapato Korea ya Kaskazini.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO