Monday, August 12, 2013

WAFUASI WA MURSI BADI WAENDELEZA MAANDAMANO

Wafuasi wa Rais wa Misri aliyeondolewa madarakani, Mohamed Morsi wameweka kambi jijini Cairo na pia wamekuwa wakifanya maandamano kila siku nchini Misri kukemea mapinduzi yaliyofanywa dhidi ya morsi tarehe 3 mwezi Julai. Viongozi wa Serikali ya mpito iliyowekwa madarakani na Jeshi la nchi hiyo wamekuwa wakiwaonya Waandamanaji kuondosha kambi zao, lakini pia kukiahidi Chama cha Muslim Brotherhood kutafuta suluhu ya mgogoro wao iwapo watasitisha maandamano. Takriban watu 250 wameuawa tangu kuangushwa kwa Morsi na kushikiliwa, Mamlaka zikisema kuwa wana nia ya kuepuka vitendo vya umwagaji damu. Lakini wafuasi wa Morsi wameitisha Maandamano makubwa siku ya jumanne kushinikiza kurejeshwa madarakani kwa Morsi na kulikemea Jeshi la nchi hiyo.
 Kiongozi ndani ya Chama cha Muslim Brotherhood amesisitiza kuwa wanataka kutuma ujumbe kwa Viongozi wa mapinduzi nchini humo kuwa Watu wa Misri watajitokeza katika maeneo mbalimbali nchini humo. Hivi sasa nchini humo kunafanyika jitihada za kufanya mazungumzo ili kupatikana suluhu ya kisiasa, mazungumzo ambayo yanaelezwa kuwa huenda yasipokelewe na Chama cha Muslim Brotherhood. Utawala wa mpito nchini Misri umeweka mpango wa kuelekea mabadiliko uya nchini humo ambao umetangaza kufanyika kwa uchaguzi mpya mwaka 2014, na kutoa mwanya kwa Muslim Brotherhood kushiriki katika mabadiliko hayo.Jitihada mbalimbali zimefanyika ikiwemo kufika jijini Cairo kwa Wajumbe toka nchini Marekani,Umoja wa Ulaya, na nchi za kiarabu kwa lengo la kumaliza mzozo wa kisiaasa lakini jitihada zao hazikuzaa matunda.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO