Saturday, January 19, 2013

15 WAFARIKI MAFURIKO INDONESIA


Mafuriko makubwa huko Indonesia yaliyosababishwa na mvua kali za siku kadhaa yameuwa watu wasiopungua 15 nchini humo. Watu wawili waliopoteza maisha yao huko Jakarta na wengine wanne wa familia moja huko Semaranga makamao makuu ya mkoa wa Java ni kati ya jumla ya watu 15 waliopoteza maishah yao kufuatia mafuriko hayo yaliyoikumba Indonesia hivi karibuni. Johan Freddy Afisa wa Idara ya Taifa ya Kushughulia Maafa ya Kitaifa  ameeleza kuwa ramani yao inaonyesha kuwa karibu asilimia 50 ya mji wa Jakarta uko chini ya maji. Ameongeza kuwa nyumba zisizopungua laki moja zimejaa maji na hivyo kusababisha watu elfu kumi kuwekwa katika makazi ya muda.  

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO