Saturday, January 19, 2013

MTOTO WA MIAKA 7 NEW YORK AKAMATWA AKIWA NA BASTOLA


Viongozi wa shule moja ya msingi mjini New York nchini Marekani wamethibitisha kutiwa mbaroni mwanafunzi mmoja mwenye umri wa miaka saba akiwa ameficha bastola iliyojaa risasi. Gazeti la Huffington Post linalochapishwa Marekani limeandika kuwa, tukio hilo limetokea katika shule ya msingi ya Viaio iliyoko katika eneo la Far Rockaway mjini New York. Mara baada ya kujiri tukio hilo, uongozi wa shule hiyo ulichukua uamuzi wa kuifunga shule hiyo. Hata hivyo, uongozi wa shule ulikataa kutaja jina la mwanafunzi huyo na jinsi walivyoigundua silaha hiyo. Tukio hilo linatokana na maombi ya mara kwa mara yanayotolewa na wazazi na wananchi kutaka zichukuliwe hatua kali za kudhibiti uingizwaji  silaha mashuleni unaofanywa na wanafunzi au wahalifu kama ilivyotokea hivi karibuni kwenye shule ya msingi ya Sindy Hook, ambapo wanafunzi 20  na wafanyakazi 6 waliuawa. Tukio la kukamatwa silaha kwa mwanafunzi mwenye umri wa miaka saba, linaonyesha kuwa, viongozi wa Marekani bado hawajawa jaddi katika  kuzuia ubebaji silaha mashuleni, kinyume na madai yanayotolewa na Rais Barack Obama wa nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO