Monday, January 21, 2013

IRAN KUWASAIDIA WAISLAM WA MYANMAR


Jamhuri ya Kiislamu ya Iran itafungua kambi maalumu nchini Myanmar kwa lengo la kuwasaidia Waislamu wanaodhulumiwa nchini humo. Hayo yamedokezwa na Mansour Haqiatpour, Naibu Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama wa Taifa na Sera za Kigeni katika Bunge la Iran. Amesema kufuatia mazungumzo na wakuu wa Myanmar, Iran imeruhusiwa kuanzisha kambo katika jimbo la Rakhine ili kuwahudumia maelfu ya Waislamu wa kabila la Rohingya. Mapema mwezi huu wabunge kadhaa wa Iran walitembelea Myanmar kuchunguza hali ya Waislamu nchini humo na kutathmini njia za kuwasaidia. Karibu Waislamu 800,000 wa kabila la Rohingya nchini Myanmar wamekuwa wakikandamizwa na Mabudhaa wenye misimamo ya kufurutu mipaka. Mabudhaa hao wameteketeza moto vijiji na misikiti ya Waislamu. Aidha serikali ya Myanmar inatuhumiwa kuwa imekataa makusudi kuwasaidia Waislamu hao walio wachache nchini humo. Maelfu ya Waislamu wa kabila la Rohingya wameuawa na makumi ya maelfu ya wengine kuachwa bila makao katika miezi ya hivi karibuni.  

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO