Monday, January 21, 2013

UFARANSA IMEANZISHA MCHEZO HATARI MALI

Gazeti la New York Times linalochapishwa nchini Marekani limeandika kuwa Ufaransa imeanzisha mchezo hatari nchini Mali. Gazeti hilo limeongeza kuwa vita vya Mali ni kitu ambacho hakikutarajiwa na Rais wa Ufaransa Francois Hollande, kwa sababu Paris ilitarajia kuwa mashambulio yake ya hivi karibuni huko Mali yangevifanya vikosi vya wapinzani virudi nyuma lakini badala yake uingiliaji huo umerefusha na kuzifanya tata zaidi operesheni za kijeshi na harakati za kidiplomasia kiasi cha kuwafanya wakosoaji wa Hollande waufananishe mgogoro wa Mali na vita vya Vietnam au Afghanistan. Wakati huohuo Rais wa zamani wa Ufaransa Giscard d'Estaing naye pia amemtahadharisha Rais wa nchi hiyo Francois Hollande na hatari ya operesheni ya kijeshi nchini Mali. Giscard d'Estaing amesema yeye anaitakidi kwamba operesheni ya aina hiyo itaibua hisia za chuki na uadui miongoni mwa raia wa Mali. Aidha ametahadharisha juu ya kile alichoeleza kuwa ni kudhihiri kwa ukoloni mpya.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO