Saturday, January 19, 2013

MADEREVA WAENDELEA NA MGOMO NEW YORK

Madereva wa mabasi mjini New York, Marekani, wameendelea na mgomo wao kwa siku ya pili mfululizo. Madereva hao wameendelea na mgomo huo kulalamikia ukosefu wa usalama wa shughuli yao hiyo. Kufuatia mgomo huo, wazazi wamejikuta katika wakati mgumu, kutokana na kushindwa kuwapeleka watoto wao mashuleni. Taarifa zinasema kuwa, Meya wa mji New York Michael Bloomberg amesema kwamba, suala la kuweka usalama katika shughuli za madereva wa mabasi katika mji huo ni jambo lisilowezekana. Mgomo huo unafanyika katika hali ambayo siku kadhaa zilizopita mazungumzo kati ya viongozi wa mji wa New York na muungano wa chama cha madereva wa mabasi ya shule nchini Marekani, yalishindwa kufikia mwafaka kuhusiana na kuwepo kwa kiwango cha chini cha hali ya usalama katika shughuli za madereva hao. Muungano huo wa chama cha madereva mjini New York umesema kuwa, kuna uwezekano mkubwa kwa madereva hao kuacha kazi zao baada ya kumalizika kipindi cha mkataba wao mwezi Juni mwaka huu. Mauaji ya kiholela kwa kutumia silaha moto ni jambo la kawaida katika mitaa ya Marekani. Mara kwa mara kumekuwa kiripotiwa mauaji ya umati yakifanyika kwenye maeneo mbalimbali hasa mashuleni huko Marekani.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO