Saturday, June 08, 2013

KOREA MBILI ZAKUBALIANA KUANZA MAZUNGUMZO

Baada ya miezi kadhaa ya mvutano, baina yao nchi mbili za Korea zimekubliana kuyaanzisha tena  mazungumzo kwa mara ya kwanza baada ya muda wa zaidi ya miaka miwili.
Kwa mujibu wa wizara inayoshughulikia masuala ya  kuungana tena, wajumbe wa nchi hizo watakutana kwenye mji wa mpakani, Panmunjom.
Wajumbe hao watautayarisha mkutano wa ngazi ya mawaziri unaotarajiwa kufanyika Jumatano ijayo katika mji mkuu wa Korea ya Kusini, Seoul.
Mkutano rasmi baina ya nchi mbili za Korea ulifanyika  kwa mara ya mwisho mnamo mwezi wa Februari miaka miwili iliyopita.
Korea ya Kaskazini ilipendekeza hapo juzi kufanyika  mazungumzo hayo juu ya kuianzisha tena miradi ya kiuchumi ya pamoja.
Katika hatua nyingine ya kupunguza mvutano baina ya nchi mbili za Korea, Korea ya Kaskazini imeyaanzisha  tena mawasiliano ya simu na shirika la Msalaba Mwekundu la Korea ya kusini .
    

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO