Tuesday, February 28, 2012

FORM SIX NA FORM FOUR

Assalam alaykum warahmatul lahi wabarakatuh.
Ndugu zangu napenda kuwataarifu kuwa muda wa kujaza form/ kuapply katika mavyuo kwa ndugu zetu wa form six na form four umefika na baadhi ya mavyuo wameshatoa form watu wajaze.
Cha muhimu ni kuwahi kufuatilia hizo form na kujaza kabisa mapema ili tusijeanza kukimbizana baadae. Pia kwa form six jambo lingine ni kuwa TCU karibu wanaanza kufungua ukumbi watu wapply hilo nalo tulifuatilie mapema nalo ili kama kuna kasoro turekebishe kabla ya ya siku ya mwisho ya kuapply.
Pia kwa ndugu yeyote anayesoma hii nakala basi ni vizuri pia awafikishie waislam wengine hususani waliomaliza form six.
Katika hii blog kuna post ya November mwaka jana inawebsite ya TCU kwa ajili ya watu kuitumia na kuangalia mavyuo ambayo yapo chini ya TCU, pi kuna wizara ya afya watu wadownload form na kujaza na kuzifikisha panapo husika. Kwa maswali zaidi kwa wale wa Dar es salaam ni bora wafike makao makuu yetu ambayo ni MUHIMBILI CHUO CHA AFYA wafike msikitini na kuulizia AMIR AU KATIBU wa jumuiya ya wanafunzi wa kiislam na hapo atatupata wahusika tukiwa na detail ambazo zinaweza kukufaa wewe au ukafikisha kwa wengine na wale wa mikoani bado hatujawa na wajumbe rasmi ila unaweza kuwasiliana nasi kwa njia ya simu(kuna nakala imeandikwa form six na form four ya NOvember pia chini kabisa kuna majina na namba za simu, facebook tafuta MSAMU MUHIMBILI tuma ujumbe wako, au katika hii blog tuma kwa njia ya comment na tutajaribu kushughulikia kadri ALLAH atavyotuwezesha. Pia kuna chuo kipo njia ya tegeta AL- MAKTOUM COLLEGE OF ENGINEERING AND TECHNOLOGY nao pia wanatoa form za kujiunga.
Shime waislam tukumbushane sisi kwa sisi kwani makafiri wenzetu wanamavyuo yao hata wakikosa vya serikali wanakwenda kusoma vyuo vyao lakini sisi bado tuko nyuma hivyo insha allah tujitahidi kukumbusha kufuatilia haya masuala kwani faida ipo ingawa unaweza usiione kwa macho ya karibu.
INSHA ALLAH ALLAH ATUFANIKISHIE HILI NA MENGINEYO MAASSALAM.

1 comment:

  1. Shukrani ndugu wacha tufuatilie na waislam wengine kama kuna news kama hizi basi zitumeni tujuzane insha allah

    ReplyDelete

TUPE MAWAZO YAKO