Thursday, October 18, 2012

Assalaamu 'alaykum warahmatullaahi wabarakaatuh. 



YALIYOJILI MAHAKAMANI KWA SIKU YA LEO KUHUSIANA NA HABARI ZA SHAIKH PONDA NA WAISLAMU WOTE WALIOKAMATWA MBAGALA.

 Kutokana na mahojiano ya jana ya shaikh ponda aliachwa na kesi 2 ambazo bado hakuhojiwa ikiwa ni ya kidongo chekundu pamoja na sakata la Markaz chang'ombe.lkn cha ajabu leo hii amehojiwa swala la markaz tuu kisha kupelekwa mahakamani. Kitu kingine cha kushangaza ni kwamba kesi zote 4 alizosomewa kwamba zinamkabili hazikusikilizwa na wameshikilia habari ya markaz. Lkn kesi imehairishwa mpaka itakaposikilizwa tena tarehe 1 november kutokana na hakimu aliyekuwepo kusema hiyo kesi haishikilii yeye kwa hiyo asubiriwe hakimu aliyepangiwa hiyo kesi kwa ajili ya kutoa hukumu ya ponda pamoja na waislamu wengine 49 wanaoshikiliwa na polisi. Wakili wa shaikh ponda alipotaka dhamana akaambiwa kama ifuatavyo : vijana hao 49 dhamana itatolewa lkn si kwa wakati huu kwa vile bado haikupangwa, na hata wakipata dhamana itakuwa kwa masharti makali na magumu sana. Kwa upande wa Ponda ni kwamba hakuna kitu kinachitwa dhamana kwake yeye kwani ni maagizo kutoka kwa DPL. Wakili alipohoji kwa nini dhamana kwa upande wa ponda isiwepo akajibiwa ni kwa sababu ya usalama wa Taifa la Tanzania. Lakini wakili akataka ajue ni usalama gani ambao unahofiwa ponda akiwa nje ? Hakimu hakujibu chochote bali akamwambia hiyo ni taratibu iliyopangwa na sharia na usitake kujua zaidi, na kama unataka dhamana basi asubiriwe huyo hakimu aliyepangiwa hiyo kesi hadi atakapoisikiliza tarehe 1 november.



 WITO KWA WAISLAMU 



KUTOKANA na kunyimwa dhamana kwa shaikh ponda na waislamu wengine 49 waislamu wote wametakiwa kwa siku ya kesho ijumaa insha allah kuitumia vizuri ili kuhakikisha kwamba kama wanasheria hawakuona kipengele cha dhamana kwa sababu ya usalama wa Taifa,kuhakikisha wanawaonesha wanasheria kipengele cha dhamana kwa kutumia qur'an.Hivyo waislamu wote wa Dar es salaam tunatakiwa kwa swala ya Ijumaa ya kesho insha allah kuswalia misikiti ya mjini na baada ya hapo kuwaonesha wanasheria sehemu ya dhamana kama wao hawajaiona.So waislamu tujiandae kwani mkae mkijua kwamba ijumaa ya kesho kutakuwa hapatoshi Dar es salaam. HAYO YOTE YAMETOLEWA NA SHAIKH MAPEO PINDI WALIPOTOKEA MAHAKAMANI BAADA YA SWALA YA AL'ASWRI HII KTK MSIKITI WA MTAMBANI K/NDONI DAR ES SALAAM.




 PIA UMETANGAZWA UONGOZI AMBAO ULITEULIWA NA KIKAO CHA JANA BAADA YA SHURA YA MAIMAMU WA DAR ES SALAAM NI KAMA IFUATAVYO. 1.AMIR NI SHAIKH MAPEO AKISAIDIWA NA SHAIKH KONDO BUNGO. 2.ANAYESHIKA NAFASI YA SHAIKH PONDA NI OST. JAFFAR. NB: IDHAA MAATA SAYYIDU QAAMA SAYYIDU { PINDI ANAPOKUFA KIONGOZI ANASIMAMA KIONGOZI } CHA MUHIMU SAMI'INAAA WA-ATWA'ANAA.


 ASSALAAMU 'ALAYKUM WARAHMATULLAAHI WABARAKAATUH.







No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO