Gazeti la Al Jamhuriyyah la Lebanon limeandika kuwa, hivi karibuni Harakati 
ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon ilifanya manuva kubwa ya 
kijeshi iliyowashirikisha wapiganaji shupavu wa harakati hiyo wapatao elfu 
10.
Gazeti hilo limeendelea kuandika kuwa, manuva hiyo imefanyika kwa minajili ya 
kujiweka tayari kwa chokochoko zozote za utawala wa Kizayuni wa Israel na 
yalifanyika katika maeneo kadhaa ya kusini na mashariki mwa Lebanon.  
Aidha gazeti hilo limeandika kuwa, manuva hayo yalifanyika kwa muda wa siku 
tatu. Manuva hayo yaliyowashirikisha vijana wenye umri wa miaka 16 hadi 20 
yanahesabiwa kuwa ya kwanza na ya aina yake ambayo yamewahi kufanywa na 
Hizbullah katika maeneo yaliyochini ya udhibiti wake.

Pia katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Lebanon Hizbullah 
ameuonya utawala wa Kizayuni wa Israel kwamba utakabiliwa na tsunami ya 
makombora yenye nguvu zaidi kuliko Fajr 5 katika miji yote ya Palestina 
inayokaliwa kwa mabavu ukiwemo Tel Aviv, iwapo utawala huo khabithi utaanzisha  
tena chokochoko dhidi ya ardhi ya Lebanon. Akizungumza na waumini waliokuwa 
wakiomboleza Ashura ya Imam Hussein AS kusini mwa Beirut, Sayyid Hassan 
Nasrullah amehoji kuwa, utawala wa Israel umetiwa kiwewe na makombora machache  
tu ya Fajr 5 yaliyorushwa na wapiganaji wa Hamas wa Kipalestina, vipi utaweza 
kustahamili kishindo cha  maelfu ya makombora yenye nguvu zaidi ya Hizbullah 
yatakayokita kwenye miji yote ya utawala huo? Katibu Mkuu wa Hizbullah ameongeza 
kuwa, utawala wa Israel unaelekea kusambaratika kwani kwa muda mrefu umekuwa 
ukiingiwa na kitete mbele ya wanamuqawama.
 
No comments:
Post a Comment
TUPE MAWAZO YAKO