Wednesday, November 28, 2012

Viongozi wa Israel wahusishwa na kifo cha Arafat

Mkuu wa Kamati ya Palestina inayochunguza kifo cha Yassir Arafat amesema kuwa viongozi wa Israel walihusika kumuua kiongozi huyo wa zamani wa Palestina. Tawfiq al Tirawi amesema ushahidi uliopo ni wa matamshi yaliyotolewa na viongozi wa Israel waliosema kuwa Arafat lazima auawe ambapo Shaul Mofaz na Ariel Sharon walifanya mazungumzo na kutaka kuuliwa Arafat. Hivi karibuni Waziri wa Mawasiliano wa utawala wa Kizayuni alieleza kuwa yoyote anayetaka kuchunguza kifo cha Yassir Arafat ajue kwamba kufanya hivyo ni sawa na kutangaza vita na Israel. Mbali na waziri huyo, makumi ya maafisa wa kisiasa, usalama na kijeshi wa utawala haramu wa Kizayuni walisema kuwa Arafat ni lazima auliwe. Wapalestina wamekuwa wakisisitiza kwa miaka kadhaa sasa kuwa Yassir Arafat aliuliwa kwa sumu na Israel.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO