Viongozi wa Israel wahusishwa na kifo cha Arafat 
Mkuu wa Kamati ya Palestina inayochunguza kifo 
cha Yassir Arafat amesema kuwa viongozi wa Israel walihusika kumuua kiongozi 
huyo wa zamani wa Palestina. Tawfiq al Tirawi amesema ushahidi uliopo ni wa 
matamshi yaliyotolewa na viongozi wa Israel waliosema kuwa Arafat lazima auawe 
ambapo Shaul Mofaz na Ariel Sharon walifanya mazungumzo na kutaka kuuliwa 
Arafat. Hivi karibuni Waziri wa Mawasiliano wa utawala wa Kizayuni alieleza kuwa 
yoyote anayetaka kuchunguza kifo cha Yassir Arafat ajue kwamba kufanya hivyo ni 
sawa na kutangaza vita na Israel. Mbali na waziri huyo, makumi ya maafisa wa 
kisiasa, usalama na kijeshi wa utawala haramu wa Kizayuni walisema kuwa Arafat 
ni lazima auliwe. Wapalestina wamekuwa wakisisitiza kwa miaka kadhaa sasa kuwa 
Yassir Arafat aliuliwa kwa sumu na Israel.
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment
TUPE MAWAZO YAKO