Friday, November 30, 2012

IRAN YATISHIA KUJITOA NPT

Iran imetishia kujiondoa katika mkataba wa kimataifa unaopinga uendelezaji wa nyuklia, NPT, kama vinu vyake vya nishati hiyo vitashambuliwa. Mwakilishi wa Iran katika Shirika la Nguvu za Atomiki Duniani, IAEA, Ali Asghar Soltanieh ametoa msimamo wa nchi yake mjini Vienna, Austria akirejerea kitisho cha Israel kuvishambulia vinu vya nyuklia vya nchi hiyo ambacho sasa kimezidi kuongezeka. Ali amesema kuwa uwezekano wa bunge la Iran kuilazimisha serikali kuuzuia ukaguzi wa IAEA kwenye vinu vya nyuklia vya nchi hiyo na hata kujitoa kwenye NPT. Mkataba wa NPT unazuia nchi ambazo hazina silaha za nyuklia kuzitengeneza. Mataifa ya magharibi yana wasiwasi kuwa kujitoa kwa nchi hiyo kwenye NPT ni mwanzo wa kutengeneza silaha za nyuklia. Hata hivyo taarifa za IAEA zinasema kuwa huenda Iran imefanya utafiti kuhusu utengenezaji wa silaha lakini si kwamba  tayari wanazitengeneza. 

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO