Friday, November 30, 2012

TAIFA HARAMU LA ISRAEL KUJENGA NYUMBA 3,000 ZA WALOWEZI

Siku moja baada ya Hadhara Kuu ya Umoja wa Mataifa kuikubalia Palestina kuwa mwanachama asiyekuwa dola kwenye Umoja huo, taifa haramu la Israel imetangaza mpango wake wa kujenga nyumba 3,000 za walowezi katika maeneo inayoyakalia ya Jerusalem Mashariki na kwenye Ukingo wa Magharibi. Licha ya uamuzi huo kuchukuliwa tangu zamani, lakini kutangazwa kwake leo kumetajwa kama ujumbe kwa Wapalestina, kwamba kupatiwa kwao uwanachama huo kwenye Umoja wa Mataifa, hakujabadilisha chochote kwenye sera za makaazi ya walowezi za Israel. Hapo jana, mabalozi wa Israel na Marekani kwenye Umoja wa Mataifa, waliwaambia wajumbe wa Hadhara Kuu ya Umoja huo, kwamba uamuzi wa kuipa uwanachama Palestina, ulikuwa bahati mbaya na kikwazo kwa juhudi za kutafuta amani ya Mashariki ya Kati.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO