Monday, November 26, 2012

ISRAEL YAJARIBU MTAMBO MWINGINE WA ULINZI


Israel imesema kuwa imefanikiwa kufanyia majaribio zana zake za ulinzi zinazokusudiwa kuzuia makobora yalio umbali wa kilomita 300.
Maafisa wa dola wamesema mtambo huo, kwa jina David's Sling au Manati ya Daudi, ulifanikiwa kuangusha kombora la kwanza katika jaribio lililofanyika wiki iliyopita.
Wakati utakapokamilika, mtambo huo utakuwa sehemu moja ya mfumo mkubwa wa ulinzi dhidi ya makombora ambao unashirikisha mtambo mwingine wa Iron Dome, ambao Wizara ya Ulinzi ya Israel inasema ulidungua mamia ya makombora ya kurushwa kwa roketi kutoka Gazi wakati wa mzozo wa majuma kadhaa yaliyopita.
Makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Israel na kundi la Hamas yalianza kutekelezwa Jumatano iliyopita baada ya siku nane za mapigano.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO