Tuesday, November 27, 2012

KWA KIDATO CHA SITA NA WENGINE WA FORM FOUR

 Assalam Alaykum Warahmatul lahi wabarakatu.

Baraza la mitihani NECTA limetoa taarifa na vigezo kwa wanafunzi wenye sifa ya kufanya mtihani wa kidato cha sita 2013. Taarifa hizo rasmi wameshapelekewa wanafunzi na wazazi kwa upande wa Zanzibar. Miongoni mwa vigezo muhimu ili kuweza kuufanya mtihani huo ni kuwa na PASS TANO na pia kuwa na CREDIT TATU.


Hivyo jumuiya ya msamu kama mhusika katika kushauri masuala ya kielimu inapendekeza yafuatayo.

1. kwa wanafunzi wa shule za privates zikiwemo za KIDINI, kama Ubungo   Islamic High School, Ridhwaa Seminary na nyingine. Kama mwanafunzi aliingia kutokana na kuwa na D mbili au moja basi fanya haraka kuweza kujua kama atafanya mtihani huo au hatofanya.

2. Changamoto kwa wanafunzi ambao wapo KIDATO CHA NNE huu ni wakati wa kujipanga vizuri kwani wengi wanaoumia ni sisi waislam. Hii ni kutokana na kuwa katika baraza ni rahisi kuzikandamiza zaidi shule za kiislam kuliko za makafiri kutokana na kuwa wao wamejazana ndani ya baraza.

3. Mwisho tuondoe imani kuwa haiwezekani kupata katika mitihani, kwa mujibu wa wataalam wa masuala ya saikolojia 


inaonyesha kuwa imanu ya mtu katika suala huchochea zaidi utendaji wake. Hii ikimaanisha kuwa kwa wenye imani kuwa hawawezi daimahuwa hawawezi na huvunjika moyo na hata kujaribu huwa hawataki.

Insha Allah juhudi zinafanyika kwa baadhi ya wazazi wa kizanzibari wakishirkiana na waalimu wa wanafunzi wao ili kulipinga hili suala lakini ichukuliwe kama changamoto kwa wanafunzi na wazazi katika kuwaandalia mazinginra mazuri watoto wao waweze kusoma na hatimaye kufikia malengo yao.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO