Saturday, December 29, 2012

HAKUNA MWENYE UWEZO WA KUIZUIA IRAN


Rais Mahmoud Ahmadinejad amesema kuwa, maadui hawana ubavu wa kuzuia harakati ya maendeleo na ustawi wa taifa la Iran. Dakta Ahmadinejad amezikosoa siasa za kindumakuwili pamoja na njama za maadui dhidi ya Iran na kusisitiza kuwa, taifa hili litaendelea kufanya harakati kuelekea ustawi na maendeleo na kwamba, maadui hawana ubavu wa kuzuia harakati hii.
Rais Ahmadinejad amesema, nguvu na uwezo wa taifa la Iran utashinda muamala mbaya wa maadui wa taifa hili. Ahmadinejad ameongeza kuwa, maadui wamekuwa wakiongea na taifa hili kwa lugha chafu na isiyo na adabu na kwamba, ukosefu wao huo wa adabu kwa taifa hili utawafanya maadui hao wajute. Amesema bayana kwamba, ni zaidi ya miaka 33 sasa ambapo taifa la Iran limesimama kidete mkabala na njama za maadui na hakuna wakati ambao maadui waliweza kulikwamisha taifa hili katika masuala mbaliambali.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO