Saturday, December 29, 2012

MISRI YATAKA KUIMARISHA UHUSIANO WAKE NA HIZBUL LAH

Balozi wa Misri nchini Lebanon Ashraf Hamdy amesema nchi yake inataka kujenga uhusiano imara na harakati ya muqawama ya Lebanon Hizbullah. Akizungumza katika mahojiano na gazeti la Lebanon la Daily Star Hamdy amesema huwezi kuzungumzia siasa nchini Lebanon pasina kuwa na uhusiano na Hizbullah. Katika kile kinachoonekana kuwa ni mageuzi makubwa ya sera zinazotafautiana na za utawala wa zamani wa dikteta Hosni Mubarak, balozi wa Misri nchini Lebanon amesisitiza kuwa serikali ya Rais Muhammad Mursi itafuata sera ya kuyanyooshia mkono kwa uzito sawa nchi na mirengo yenye ushawishi katika eneo ikiwemo Hizbullah ili kuweza kuwa na mawasiliano ya karibu na viongozi wa Lebanon. Aidha ameongeza kuwa tayari ameshakutana na viongozi wa idara ya kisiasa ya Hizbullah ili kuweza kufahamiana vizuri zaidi. 
Balozi wa Misri amefafanua kuwa Hizbullah imefanya kazi nzuri ikiwa ni harakati ya muqawama katika kulinda ardhi ya Lebanon na kwamba hatua ya harakati hiyo ya kupambana kuyakomboa maeneo ya nchi hiyo yanayokaliwa kwa mabavu na Israel ni halali na ni ya kisheria. Uhusiano wa Misri ya enzi za Mubarak na Hizbullah uliharibika zaidi mwaka 2008 katika vita vya siku 22 vya Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza, wakati Katibu Mkuu wa Hizbullah Sayyid Hassan Nasrullah alipoikosoa Cairo kwa kushindwa kuwasaidia Wapalestina

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO