Thursday, December 27, 2012

ISRAEL YARUHUSU MALORI YA BIDHAA KUINGIA GAZA


Israel imelegeza vikwazo juu ya bidhaa zinazoingizwa katika Ukanda wa Gaza. Hatua hiyo itaruhusu malori 20 yaliyojaza bidhaa za ujenzi kuingia katika ukanda huo kila siku, hii ikiwa ni mara ya kwanza tangu mwaka 2007.
Radio ya Israel imesema kwamba bidhaa hizo zitaanza kuingia wiki ijayo. Tangazo la radio hiyo pia limesema kwamba Israel imeruhusu kuingizwa kwa mabasi mapya 40 na malori 20 kwa matumizi ya kila siku katika ukanda wa Gaza. Uamuzi wa kuruhusu kuingizwa kwa vifaa vya ujenzi unaonekana kuwa sehemu ya makubaliano yasiyo rasmi, ambayo yalifikiwa baina ya Israel na chama cha Hamas chini ya usuluhishi wa Misri, na ambayo yalisimamisha mapigano makali yaliyoibuka mwezi Novemba mwaka huu kati ya Israel na Hamas.
Vikwazo vya Israel dhidi ya uingizwaji wa bidhaa za ujenzi ndani ya Ukanda wa Gaza viliimarishwa mwaka 2006, kufuatia mfululizo wa mashambulizi ya maroketi kutoka katika ukanda huo na kutekwa kwa mwanajeshi wake.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO