Thursday, December 27, 2012

BARIDI YAUWA WATU 128 RUSSIA


Watu wasiopungua 128 wamekufa kutokana na baridi isiyo ya kawaida nchini Urusi, ambayo imefika nyuzi 30 chini ya sufuri katika kipimo cha Celsius. Shirika la habari la Urusi, Interfax, limesema kuwa watu wengine takriban 900 wamepatiwa matibabu hospitalini kutokana na matatizo yaliyo na uhusiano na baridi. Wengi wa walioathirika ni wale wasio na makazi.
Huku hali hiyo ikijiri nchini Urusi, huko Marekani kimbunga kinachoambatana na barafu kutoka ghuba ya Mexico kimeipiga kanda ya maziwa makuu ya Marekani na kusababisha vifo vya watu saba na kukwamisha usafiri wa anga. Kitengo cha hali ya hewa nchi humo kimeonya kwamba uzito wa barafu unaweza kuangusha miti na miundombinu ya umeme. Tayari watu wapatao laki mbili hawana huduma ya umeme, na maelfu ya watalii wamekwama katika maeneo mbalimbali ya Marekani.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO