Wednesday, December 26, 2012

MALI YAPINGA KUINGIA MALI KIJESHI

Serikali ya Tunisia imetangaza kuwa, inapinga aina yoyote ya uingiliaji kijeshi nchi za kigeni huko Mali. Hayo yamesemwa na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Tunisia Ali al Aridh alipokutana na Waziri mwenzake wa Mambo ya Ndani wa Algeria Dahou Oueld Kablia na kuongeza kuwa, nchi yake inapinga suala hilo kwa kuwa uingiliaji kijeshi katika nchi hiyo ya Afrika, utaharibu zaidi hali ya nchi hiyo. Amesema kuwa, Tunisia ina mitizamo ya pamoja na nchi jirani yake Algeria kuhusiana na mgogoro wa Mali na kwamba, kwa mara kadha zimekuwa zikipinga hatua ya uingiliaji wa madola ya kigeni katika juhudi za kumaliza mgogoro wa nchi hiyo. 
Amesisitiza kwamba, mgogoro wa Mali lazima utatuliwe kwa njia za kisiasa na kiusalama. Jana Waziri wa Mambo ya Ndani wa Algeria aliyekuwa safarini nchini Tunisia, alikutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa nchi hiyo Hamadi al Jabali. Siku ya Alkhamisi iliyopita, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilipitisha muswada uliopendekezwa na Ufaransa kuhusu uingiliaji kijeshi nchini Mali.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO