Wednesday, December 26, 2012

MATAMSHI YA MAREKANI JUU YA UGAIDI MZURI NA MBAYA YAKOSOLEWA

Sergei Lavrov Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema ugaidi ni ugaidi tu akisisitiza kuwa hatua ya nchi za Magharibi ya kuugawa ugaidi huko Syria katika mafungu mawili yaani ugaidi mzuri na mbaya inatilia shaka madai ya nchi hizo kuhusu demokrasia. Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema ni jambo lilisokubalika kwa nchi za Magharibi kuwaunga mkono magaidi huko Syria. Amesema nchi za Magharibi zimeugawa ugaidi katika mafungu mawili yaani ugaidi mzuri na mbaya na kwamba hatua hiyo haikubaliki kabisa. Amesema hivi na hapa ninamnukuu " Iwapo tutafuata mantiki hiyo basi kuna uwezekano ikatutumbukiza katika hali hatari zaidi si tu katika eneo la Mashariki ya Kati, bali katika pembe nyingine za dunia pia," mwisho wa kunukuu. Lavrov amesema si jambo jipya kwa nchi za Magharibi kuamua kuugawa ugaidi katika mafungu mawili. 

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO